Thursday, January 26, 2012

MAKAMU JAJI MKUU KENYA ASIMAMISHWA KAZI.1/

NAIROBI, KENYA.
        Rais wa Kenya Mh.Mwai Kibaki amemsimamisha kazi makamu jaji mkuu wa nchi hiyo bi. Nancy Baraza kufuatia tuhuma za kutishia maisha kwa kutumia silaha zinazomkabili na kuunda jopo maalum la kumchunguza.
         Bi.Baraza anatuhumiwa kumtishia kwa bastola mlinzi wa duka moja bi. Rebbecca Kerubo siku ya mkesha wa mwaka mpya kufuatia kukosekana kwa maelewano kati yao.Taaria kutoka ikulu imesema Bi.Baraza hatoendelea na majukumu yake ya kimahakama mpaka hapo uchunguzi utakapokamilika na kkuonekana hana tuhuma, ambapo kwa wakati huu aliosimamishwa atakuwa akilipwa nusu mshahara.
Taarifa hiyo imemtaja Jaji mkuu mstaafu wa Tanzania Bw.Augustino Ramadhan kama mwenyekiti wa Jopo hilo na  wengine ni Prof Judith Behemuka, Philip Ransley, Surinder Kapila, Beuttah Siganga, Grace Madoka na Prof Mugambi Kanyua wenye nafasi kama wajumbe.


No comments:

Post a Comment