Thursday, November 29, 2012

KILI STARS YAFUNGWA NA BURUNDI

UGANDA,
Timu za soka Tanzania, Kilimanjaro Stars na Timu ya Taifa ya Burundi zimekabiliana vikali na katika mchezo wa pili wa leo kwenye mashindano ya Chalenji CECAFA katika uwanja wa Namboole nchini Uganda.
Matokeo ya mchezo huo Burundi imeibamiza Kilimanjaro Stars kwa bao 1-0 kupitia bao lililofungwa kwa njia ya penati katika kipindi cha pili.http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2011/11/Kilimanjaro-Stars.jpg?width=650


Matokeo hayo yanaiweka Kilimanjaro katika shinikizo la kushinda mchezo wake na Somalia kwa magoli mengi ili waweze kusonga mbele.
Katika mchezo wa awali Somalia imeondolewa katika mashindano ya mwaka huu ya soka kuwa ni taji la Afrika Mashariki na kati CECAFA inayoendelea jijini Kampala Uganda.
Sudan walipata bao lao la ushindi katika dakika ya 86 kipindi cha pili kupitia mchezaji Mohammed Farid baada ya vijana hao kujaribu kutafuta bao la mapema bila ya mafanikio.
Ikilinganishwa na mchuano wa kwanza dhidi ya Burundi walikofungwa mabao 5 kwa 1,Somalia ilicheza mchezo wa hali ya juu huku ikishika kiwango cha kati na pia kushambulia lango la Sudan lakini umaliziaji haukuwa mzuri.
Kocha wa Somalia Mganda Sam Ssimbwa alikuwa amesema hapo awali kuwa alitarajia kikosi chake kingefika katika awamu ya nusu fainali baad aya kukinoa kikosi hicho kwa wiki mbili.
Sudan nayo ilianza mchuano wao wa ufunguzi kwa kusuasua baad aya kuchanagwa na Tanzania kwa mabao mawili kwa bila.
 

Saturday, November 17, 2012

MAPADRE WAPIGWA RISASI IRINGA

http://www.wavuti.com/uploads/3/0/7/6/3076464/4805172_orig.jpg?288
IRINGA-TANZANIA 
Watu saba wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha za moto wamevamia Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani mkoani hapa linaloongozwa Rais wa Baraza Kuu la Maaskofu wa kanisa hilo (TEC), Askofu Tacius Ngalalekumtwa na kisha kupora fedha zaidi ya Sh.milioni 2.5 na kuwajeruhi kwa risasi mapadre wawili.

Tukio hilo limekuja siku moja tu baada ya watu wengine wanaosadikiwa kuwa majambazi kuvamia Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa mjini ambao walipora vitu mbalimbali na kumjeruhi kwa risasi mlinzi wa kanisa hilo.

 

Katika tukio la uvamizi wa kanisa la Parokia ya Isimani, mapadre waliojeruhiwa kwa kupigwa risasi ni Padre Angelo Burgio raia wa Italiano, na Helman Myala ambaye ni paroko wa kanisa hilo aliyejeruhiwa kwa kupigwa mapanga sehemu kadhaa za mwili wake.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Hospitali ya Mkoa, Padre Angelo Burgio, alisema walivamiwa na watu saba walikuwa na silaha za moto na za jadi majira ya saa 4:30 usiku ambao walivunja milango ya kuingilia ndani.

 “Waliotuvamia walikuwa saba wakiwa na bunduki, virungu, nondo na mapanga wakatuamuru tuwaoneshe pesa zilipo, wakaanza kunipiga kwa virungu huku mmoja akiniwekea bunduki tumboni kisha wakachukua zaidi ya Sh. 2,500,000,”alisema Padre Burgio.

Alisema mwenzake Padre Myala walinyang’anya kiasi cha Sh.1,300,000 na simu za mikononi.

Hata hivyo alisema hajui mali zingine zilizochukuliwa kwa kuwa baada ya kuvamiwa na kuumizwa hawakupata nguvu tena za kuweza kukagua vitu vingine.

“Kwa kweli sijui uharibifu mwingine kwa sababu baada ya kuvamiwa na kuumizwa hatukupata nguvu tena ya kuweza kukagua vitu vingine ndipo tulipokimbizwa na wasamalia wema hospitalini” alisema.

Kaimu wa Mganga Mkuu wa hospitali ya Mkoa wa Iringa Dk.Gwanchele Faustine amekiri kupokea majeruhi hao majira ya saa 7 usiku.

“Tumepokea majeruhi wawili usiku ambao ni Mapadre wa Kanisa katoliki Padre Angelo Burgio na Padre Helman Myala, Padre. Angelo amepigwa risasi upande wa kushoto na kutokea upande wa kulia lakini kuna risasi zingine zipo kifuani tunamuandaa aingizwe kufanyiwa upasuaji sasa hivi” alisema Dk.Faustine.

Hata hivyo alisema pamoja na matibabu wanayoendelea kupata hali zao zinaendelea vizuri.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kihorogota, Costantino Kihwele, alisema vijana wameingia kwenye msako kila sehemu na kufanikiwa kumkamata kijana mmoja anayesadikiwa kuwa ni mmoja wa tukio hilo akiwa na bunduki.

“Kuna kijana mmoja amekamatwa na vijana wa Isimani ambao waliamua kuingia msituni kufanya msako lakini jina lake nitakwambia kadiri tutakavyokuwa tunaendelea na msako” alisema.

Katika hatua nyingine, Dk. Faustine alisema mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa jana hali yake bado ni mbaya.

“Mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa na kufikishwa hapa bado hali yake ni mbaya na bado tunaendelea kumhudumia” alisema.

Juzi Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa lilivamiwa na kuvunjwa milango na watu wasiojulikana huku mlinzi Bathlomeo Nzigilwa akijeruhiwa kwa risasi.

Akitoa maelezo juu ya tukio hilo kanisani hapo, mhuduma wa Kanisa hilo Sista Lucy Grace Mgata alisema aligungua kuwa kunauvamizi umefanyika alfajiri alipofika kanisani hapo kwa ajili ya kufungua milango ya Kanisa tayari kwa Ibada ya Misa za kila siku zinazoanza saa 12:00 asubuhi.

“Nilifika hapa saa 11:40 alfajiri kwa ajili ya kufungua milango na kufanya maandalizi kwa ajili ya misa lakini nilipoukaribia mlango huo nikakuta mlinzi amekaa kwenye kiti huku kichwa chake kikiwa kimeinamishwa chini na kufunikwa kofia nikajua amelala lakini milango ikawa wazi.

Sista Mgata alisema alipomkaribia mlinzi huyo alikuta damu inamtiririka na ndipo alipokwenda kutoa taarifa kwa padre.

Alisem pamoja na kuvunjwa na uharibifu wa Kanisa hilo, ofisi ya parokia nayo ilivunjwa huku vitabu, mafaili mbalimbali pamoja na nyaraka mbalimbali zikiwa zimechanwa na kuvurugwa ovyo kiasi cha kutotamanika.

Mavazi ya ibada na vifaa mbalimbali vya ibada vimeharibiwa vibaya, Taberenakulo ndogo nayo ikiharibiwa, msalaba kuvunjwa pamoja na Hostia Takatifu kutupwa kila mahali.

Sista Mgata alisema kuwa kuliwa na hela za watumishi wa artare walizokuwa wakichangishana kwa ajili ya matumizi ya umoja wao pamoja na hela za chama cha kitume cha utume wa Fatima zimechukuliwa japo bado hazijajulikana jumla yake huku funguo za teberenakulo kubwa wanayohidhi Ekaristi Takatifu zikipoea.

Kwa upande wake Katekista Agustino Luhama mhudumu wa ofisi ya Parokia alisema hela anazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa nawavamizi hao ni zaidi ya shilingi laki tano.

“Hela ninazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa ni zaidi ya Sh. 500,000 lakini zingine sijapata idadi kwa sababu nilikuwa sijazijumlisha na zingine nilizipokea juzi kutoka kwa waamini mbalimbali” alisema Kat. Luhama.

Padre Aloyce Mdemu ambaye pia ni Makamu wa Askofu wa jimbo hilo alisema bado ni mapema kujua thamani ya uharibifu uliofanyika kwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi wa vifaa vingine na maeneo mengine ambayo huenda hayajagundulika.

Kufuatia matukio hayo ambayo yamelenga makanisa, hali hiyo imezua hofu kubwa kwa wananchi wa mkoa wa Iringa mbao wamekuwa wakijiuliza kuna jambo ambalo limejificha kwa kuwa siyo jambo la kawaida kuvamiwa kwa makanisa na kujeruhi mapadre.


TRENI YAGONGANA NA BASI MISRI NA KUUA WATOTO 50-WAZIRI WA USAFIRI AJIUZULU

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02401/Egypt-train-crash_2401756c.jpgCAIRO-MISRI,         Ajali hiyo imetokea leo saa mbili asubuhi kwa saa za huko katika jimbo la Asyutu kusini mwa Misri. Gavana wa jimbo hilo Yahya Kishkik pamoja na maofisa kadhaa wamekwenda kwenye eneo la ajali na kutaka kuunda haraka kamati ya uchunguzi. Pia ametoa salamu za rambirambi kwa familia za watu walioathirika huku akisihi itolewe fidia kwa watu waliofariki na kujeruhiwa.
Treni moja nchini Misri imegongana na basi la shule na kusababisha vifo vya watoto 50.

Wakati huohuo Habari zaidi zinasema kutokana na ajali hiyo, waziri wa usafiri nchini humo Mohamed Rashid el-Matin amejiuzulu kuonesha uwajibikaji baada ya ajali hiyo ambayo serikali ndiyo inalaumiwa kutokana na kuwa na miundo mbinu mibovu ikikumbukwa ajali kubwa ya treni mwaka 2002 ambapo watu 360 walikufa  baada ya treni kuwaka moto.

 Rais wa nchi hiyo Mohamed Morsi amemtaka waziri mkuu Hesham Gandil kutoa msaada wowote wa lazima utakaohitajika na kuwatibu waliojeruhiwa na kuahidi kuwaadhibu wale wote waliosababisha ajali hiyo.

Wednesday, November 14, 2012

UFARANSA YAUNGA MKONO BARAZA LA UPINZANI SYRIA-Yataka lisaidiwe kijeshi.


PARIS -UFARANSA,
France's President Francois Hollande addresses a news conference at the Elysee Palace in Paris, November 13, 2012. REUTERS/Philippe WojazerNchi ya Ufaransa imekuwa nchi ya kwanza toka barani ulaya kulitambua rasmi baraza jipya la mapinduzi nchini Syria SNC ambalo lilitangaza viongozi wake wapya siku ya jumapili.

Akizungumza akiwa mjini Paris, rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema kuwa nchi yake inalitambua baraza hilo kama chombo halali kinachoongoza mapinduzi nchini Syria na sasa kinachotakiwa ni kuangalia namna ya kuwasaidia waasi wa silaha.

Nchi nyingine za magharibi bado hazijatangaza kulitambua baraza hilo japo zimepongeza hatua ambayo imefikiwa na wajumbe wake kwa kujumuisha makundi yote yanayopigana nchini Syria.

Katika hatua nyingine mashambulizi zaidi yameripotiwa nchini Syria ambapo majengo ya shirika la umoja wa mataifa la kushughulikia wakimbizi duniani UNHCR yameshambuliwa.

Melisa Fleming ni msemaji wa UNHCR na amesema kuwa licha ya hali ya usalama kutoridhisha nchini humo lakini wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa msaada wa chakula na madawa.

Wednesday, November 7, 2012

NI OBAMA TENA!


MAREKANI,
Rais wa Maerkani Barack Obama ameibuka tena kidedea katika uchaguzi mkali wa kugombea urais wa Marekani,safari hii akimshinda Mitty Romney kwa jumla ya ya kura 303 kwa 206 katika ushindani mkali ambapo Romney alimshinda Obama katika kura za wananchi akipata asilimia 50 dhidi ya 49 za Obama.kaiongea baada ya kutangazwa matokeo rasmi Obama amewashukuru wamarekani kwa kuonesha imani juu ya uongozi wake na kumpa ridhaa y kuongoza tena taifa hilo kwa muhula wa miaka minne ijayo.

Katika hotuba yake baada ya kutangazwa kushinda rais Obama amesema kuwa kwa sasa anarejea ikulu akiwa na malengo thabiti na mwenye ari zaidi ya awali kwa lengo la kuwatumikia raia wa taifa hilo.
Obama amesema kuwa haijalishi tofauti zozote zilizopo kwa wamarekani bado kwa pamoja inawezekana kulifikisha taifa hilo mbele zaidi katika suala la maendeleo na usalama, ili kuhakikisha ndoto za wamarekani wote zinatimia.

Aidha rais Obama amemshukuru mpinzani wake Mitt Romney kwa kampeni zenye ushindani na kwamba ataendeleza ushirikiano na gavana huyo ili kuliwezesha taifa hilo kusonga mbele kwa manufaa ya wamarekani wote.


Tuesday, November 6, 2012

UCHAGUZI MAREKANI LEO-OBAMA ATOA MACHOZI KAMPENI YA MWISHO!





MAREKANI,

Baada ya kampeni za miezi kadhaa , vituo vya kupiga kura vimeshafunguliwa hivi karibuni katika uchaguzi wenye ushindani mkali na ambao ulikuwa na kampeni zenye kugharimu pesa nyingi zaidi kuwahi tumika katika historia za uchaguzi Marekani.

Katika kampeni za mwisho Rais Obama alitoa wito wake wa mwisho kwa wapiga kura katika mkutano wa kisiasa uliofanyika katika jimbo la Iowa hapo jana, ambapo kwa hisia alitokwa na machozi."Nimerudi tena nawaomba mtusaidie kumaliza tulichokianza, hapa ndipo mabadiliko yalipoanzia"Alisema Obama.

Ushindani katika uchaguzi huu ni mkali sana na mpinzani wa rais Obama wa chama cha Republican Mitt Romney amekuwa akiyazulu mara kwa mara majimbo mawili makuu Ohio na Pennsylvania.

Kura ya mwisho ya kutafuta maoni iliashiria kuwa rais Obama anaongoza katika majimbo mengi ambayo wagombea wote wana nafasi.

Lakini kura hiyo inaashiria pia huenda idadi ya watu watakao jitokeza kupiga kura ikawa kubwa miongoni mwa wafuasi wa Romney.

Kura za kwanza zilipigwa katika eneo la Dixville Notch katika jimbo la New Hampshire ambapo wagombea wote walitoka sare.

Monday, November 5, 2012

HAKUKALIKI, HAKULALIKI,HAKULALIKI WAGOMBEA WA URAIS WA MAREKANI


Obama na Romney wakipishana njia.
MAREKANI, Mbio za kuelekea ikulu ya White House nchini Marekani zimeingia katika saa za mwisho huku wagombea wakiizunguka nchi kutoa hoja za mwisho kuhusu uchumi, uokozi wa viwanda vya magari na msongamano jijini Washington.

 Obama mwenye umri wa miaka 51 na mpinzani wake Mitt Romney mwenye umri wa miaka 65 wanazidiana kidogo kwa mujibu wa maoni yanayochapichwa na vyombo vya habari, na kila moja anapambana kuwashawishi wapiga kura ambao bado hawajaamua nani wamchague.

Walipishana jimboni Ohio Jumapili, ambalo ndilo linalosemakana kuwa muhimu zaidi miongoni mwa majimbo saba yenye maamuzi katika uchaguzi wa Marekani. Juu ya hilo, Obama alizitembelea New Hampshire, Florida na Colorado siku hiyo ya Jumapili, wakati Romney alizitembelea Iowa, Virginia na Pennslyvania. Msisitizo wa Obama katika kipindi hiki ni kwa wapiga kura kuchagua kati ya dira mbili. "Huu siyo tu uchaguzi kati ya wagombea wawili au vyama viwili, ni uchaguzi kati ya dira mbili tofatu za Marekani," alisema Obama.
Rais Barack Obama akitambulishwa na rais wa zamani Bill Clinton katika mkutano wa kampeni mjini Concord, New Hampshire.Rais Barack Obama akitambulishwa na rais wa zamani Bill Clinton katika mkutano wa kampeni mjini Concord, New Hampshire.
Hoja za mwisho za Obama jimboni Ohio zilijikita katika uokozi wa kampuni za magari za Chrysler na General Motors mwaka 2009, ambao Romney aliupinga akiwa gavana wa jimbo la Massachusets wakati huo na kisema sekta ya magari ilipaswa kuachwa ifilisike. Matamshi hayo yamekuja kumuathiri, hasa katika jimbo lenye viwanda vingi la Ohio.
Katika mkutano siku ya Ijumaa mjini Springfield, Ohio, Obama aliwaambia wafuasi wake waliyozomea alipotaja jina la Romney, kwamba kupiga ndiyo kisasi bora zaidi. Romney alitumia mkutano wake mjini Cleveland kumshambulia Obama kuhusiana na kauli yake hiyo, na kusema badala yake, yeye anawaomba wapiga kura wachague kwa mapenzi ya nchi yao. Romney alisema mabadiliko aliyoahidi Obama yameshindikana
"Mabadiliko hayawezi kupimwa kupitia hotuba, mabadiliko yanapimwa kupitia mafanikio, na miaka minne iliyopita mgombea Obama aliahidi mambo mengi kwa watu wengi lakini ametimiza kidogo sana," alisema Romney.
Wapambe wapishana kushawishi wapiga kura
Makundi yanayojitolea kwa ajili ya wagombea yalikuwa yanapishana katika majimbo yenye maamuzi, wakiwasiliana na wafuasi wao kuhakikisha kuwa watapiga kura na kujitolea kuwasafirisha kwenda kwenye vituo vya kupigia kura. Wakati Romney akiwasihi wafuasi wake waende kwa wingi katika vituo vya kupigia kura siku ya jumanne, Obama anaelekeza juhudi zaidi katika majimbo yenye maamuzi.
Maoni yamekuwa yakiwaonyesha wawili hao wakikaribiana kwa sana lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema Obama bado ana nafasi ya kushinda. Edward Wycof William, mchambuzi wa masuala ya kisiasa anasema maoni yamekuwa yakibadilika kutoka wiki moja hadi nyingine, lakini kilichoonekana ni kwamba Romney hajaongoza kabisaa katika maoni yoyote katika majimbo muhimu.
Mitt Romney akiweka sahihi yake katika fulana ya mfuasi wake mjini Des Moines, Iowa Novemba 4Mitt Romney akiweka sahihi yake katika fulana ya mfuasi wake mjini Des Moines, Iowa Novemba 4.
Obama akumbushia hali ngumu aliyoikuta mwaka 2008
Obama anatafuta awamu ya pili huku kiwango cha ukosefu wa ajira kikiwa asilimia 7.2. Hakuna rais aliyefanikiwa kupata muhula wa pili tangu kumalizika kwa vita vikuu vya pili vya dunia kukiwa na kiwango cha ukosefun wa ajira kilicho juu ya asilimia 7.2. Uchumi bado unakua kwa chini ya asilimia 2, lakini Obama amewakumbusha wapiga kura juu ya mazingira ya mgogoro alimochaguliwa miaka minne iliyopita.
"Kumbukeni mwaka 2008 tulikuwa katikati ya mgogoro mbaya zaidi tangu mdororo mkubwa wa uchumi. Tulikuwa katikati ya vita viwili. Na sasa biashara zetu zimetengeneza ajira karibu milioni 5.5, viwanda vya magari vinafanya vizuri na sekta ya nyumba inaanza kurejesha thamani yake, tunategemea mafuta kutoka nje kwa kiasi kidogo kuliko wakati wowote katika kipindi cha miaka 20," alime Obama na kuongeza kuwa vita vya Iraq vimekwisha, vile vya Afghanistan vinakaribia mwisho na Osamba bin Laden aliuawa.
Wanajeshi wa Marekani wakiushusha shehena ya msaada kwa ajili ya waathirika wa kimbunga Sandy. Marekani inakwenda kwenye uchaguzi wakati eneo la kaskazini mashariki likikabiliana na madhara ya moja ya tufani kubwa zaidi katika historia ya nchi hiyo.Wanajeshi wa Marekani wakiushusha shehena ya msaada kwa ajili ya waathirika wa kimbunga Sandy. Marekani inakwenda kwenye uchaguzi wakati eneo la kaskazini mashariki likikabiliana na madhara ya moja ya tufani kubwa zaidi katika historia ya nchi hiyo.
Takriban watu milion 27 wamekwisha piga kura katika uchaguzi wa mapema. Zaidi ya milioni 130 walipiga kura mwaka 2008. Wapiga wanatarajiwa kuamua hatma ya viti vyote 435 vya Bunge la wawakilishi ambalo linatarajiwa kuendelea kudhibitiwa na chama cha Republicans, na theluthi moja ya viti vya bunge la Seneti lenye viti 100, ambako chama cha Democrats kinatarajiwa kuedeleza udhibiti mdogo. Uchaguzi wa mwaka huu unafanyika wakati sehemu ya kaskazini mashariki inakabiliana na madhara ya kimbunga cha Sandy kilichoharibu maelfu ya makaazi na kuua watu zaidi ya 100.
Waendesha kura za maoni wamtabiria ushindi Obama
Obama anaendelea kuwa na faida dhidi ya Romney katika majimbo yenye maamuzi, ambayo ndiyo yanaamua mshindi wa urais. Ili kushinda kiti hicho, mgombea laazima kura 270 za majimbo. Obama anahitaji kujihakikishia kura 243 za majimbo yanayoegemea chama cha Democrats, wakati Romney anaweza kujihakikishia kura 206, na hii inamuongezea shinikizo la kutafuta zaidi kura za majimbo yenye maamuzi.
Tayari mawakili wa kambi zote wanajianda kwa mpanbano mrefu wa mahakani katika majimbo yenye ushindani mkubwa. Baadi ya wataalamu wanatarajia vuta nikuvute kama zile za mwaka 2000, zilizochukua wiki tano kumpa ushindi George W. Bush. Tayari mvutano umeripotiwa jimboni Florida, baada ya wapiga kura wanaodhaniwa kuwa wa Democrats kuzuiwa na gavana wa jimo hilo ambaye ni wa chama cha Republican.
Obama na timu yake wakifuatilia mauaji ya Osama bin Laden. mauaji hayo yamekuwa moja ya hoja zake za kutaka muhula wa pili.Obama na timu yake wakifuatilia mauaji ya Osama bin Laden. mauaji hayo yamekuwa moja ya hoja zake za kutaka muhula wa pili.
Maoni yaliyochapishwa na gazeti la Wall Street Journal siku ya Jumapili yalimpa Obama asilimia moja zaidi ya Romney kitaifa akiwa na asilimia 48 dhidi ya 47 za Romney. Tovuti ya Real Clear Politics ilimpa Obama uongozi wa asilimia 0.2. Karibu waendesha kura za maoni wote wamemtabiria ushindi Obama katika kura za majimbo. Talking Point Memo imempa Obama kura 303 dhidi ya 191 za Romney, Fivethirtyeight.com imempa Obama kura 307 dhidi ya 231 za Romney na Pricneton Election Consortium ilimpa Obama kura 277 dhidi ya 206 za Romney(Chanzo DW)

Lipumba kutafuta suluhu ya Waislamu na Wakristo





DAR ES SALAAM-TANZANIA,
Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF) nchini Tanzania, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ameanza kutafuta suluhu kati ya viongozi wa dini za Kislamu na Kikristo ili kuweka misingi ya waumini wote kuheshimania na kudumisha amani nchini.

Prof. Lipumba amesema atafanya jitihada za kukutana na viongozi wa Kiislamu na Kikristo pamoja na wanasiasa akiwemo Rais Jakaya Kikwete ili kufikia lengo lake. Kiongozi huyo ameongeza kwamba, serikali ikitumia busara na kuwasiliana na Maimamu wa misikiti pamoja na viongozi wa Kikristo panaweza kupatikana tija. Lipumba amewaomba Waislamu wasishiriki kwenye maandamano baada ya Swala ya Ijumaa kwa kuwa hali hiyo ya mtafaruku ndiyo inayochochea ghasia na dhana kwamba Tanzania imetumbukia katika machafuko ya kidini.

Wiki iliyopita viongozi wa makundi mbalimbali ya waumini wa Kiislamu pamoja na polisi, walikuwa wakihimiza waumini kutojihusisha na maandamano hayo waliyoyaita haramu kwani kufanya hivyo ni uvunjifu wa amani. Waislamu wamekuwa wakiandamana wakitaka kuachiliwa huu Katibu wa Jumuiya na Taasisi ya Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda ambaye anaendelea kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za uchochezi.(chanzo:Tehran)
      

Sunday, November 4, 2012

IDADI YA VIFO KUTOKANA NA KIMBUNGA MAREKANI YAFIKIA 90


Madhara ambayo yamechangiwa na Kimbunga Sandy kilichopiga Jiji la New York nchini Marekani
MAREKANI, Idadi ya vifo vilivyosababishwa na kimbunga kikali cha Sandy ambacho kimepiga nchi ya Marekani hasa majiji ya New York na New Jersey imeongezeka na sasa watu wanaokadiriwa kufikia tisini wanatajwa kupoteza maisha. Kimbunga Sandy ambacho kinatajwa kuwa kikali zaidi kupiga nchi ya Marekani katika kipindi cha miaka mitatu kimeendelea kucha madhara makubwa ikiwemo ukosefu wa huduma ya umeme kwa wananchi.

Mamlaka nchini Marekani zimethibitisha watu milioni nne na laki tano kutoka majimbo kumi na mawili nchini humo wameendelea kukosa huduma ya umeme huku tatizo la upatikanaji wa mafuta nalo likijitokeza.
Kimbunga Sandy ambacho kimepiga zaidi eneo la Mashariki mwa Marekani kimesababisha hasara ya dola bilioni hamsini na kwa sasa serikali inaendelea na juhudi za kusafisha maeneo ambayo yamekubwa na madhara hayo.
Idadi ya vifo inatajwa huenda ikaongezeka kutokana na kila waokoaji wanapofika wanakutana na miili ya watu ambao wamepoteza maisha kutokana na kimbunga Sandys ambacho kilianzia Caribbean.

Kikosi Maalum ambacho kinafanya msako wa kutafuta watu waliopoteza maisha wameendelea kuahidi zoezi hilo litakuwa limekamilika haraka iwezekanavyo ili kujua idadi kamili ya watu waliopoteza maisha.

Takwimu zinaonesha watu wengi wamepoteza maisha katika Jiji la New York ambapo Mamlaka za Jiji hilo zinaeleza watu thelathini na wanane wamepoteza maisha huku wengine kadhaa wakiwa hawajulikani walipo.
Harakati hizi zinaendelea huku baadhi ya huduma zikiwa zimeanza kurejea kama ilivyokuwa awali huku njia za reli za chini ya ardhi nazo zikifunguliwa kwa mara ya kwanza pamoja na safari za ndege kuendelea kama kawaida.
Serikali nayo imeahidi kufika siku ya jumamosi huduma ya umeme itakuwa imerejeshwa katika maeneo yote ambayo huduma hiyo ilitoweka kipind ambacho Kimbunga Sandy kilisababisha madhara(chanzo RFI)

Thursday, November 1, 2012

AFRIKA KUSINI KUCHAPISHA NOTI ZENYE PICHA YA MANDELA


JOHANESBURG-AFRIKA KUSINI,
Afrika Kusini inatarajia kuchapisha noti mpya zenye picha ya rais Mandela mapema mwezi huu, kuonyesha heshima yao kwa rais huyu wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini.

Gavana wa Benki Kuu ya Afrika Kusini Gill Marcus amesema,noti hizo mpya zitatumika rasmi kuanzia tarehe 6 ya mwezi huu. Upande mmoja wa noti hizo utakuwa na picha ya rais wa zamani Mandela, na upande mwingine utakuwa na picha za wanyamapori maarufu watano wenye sifa barani Afrika. Gavana huyo amesema noti hizo mpya ni za Rand 10, 20, 50, 100 na 200, na zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia mpya itakayosaidia kugundua noti bandia.

Ili kuwafahamisha wananchi noti hizo, serikali ya Afrika Kusini imefanya shughuli husika za matangazo nchini humo pamoja na nchi za kanda hiyo ambako fedha ya Afrika Kusini inatumika zikiwemo Namibia, Swaziland, na Lesotho.(Chanzo:Idhaa ya China)

MLIPUKO WAUA 6 SYRIA

http://www.aljazeera.com/mritems/Images/2012/10/31/201210315413296734_20.jpgDAMASCUS-SYRIA,
Kumetokea milipuko miwili huko Damascus nchini Syria ambapo mlipuko mmoja umeua watu 6 kwa mujibu wa wanaharakati wameripoti.Pa,oja na milipuko hiyo kumeripotiwa mapigano makali kati ya vikundi vya waasi na serikali mjini humo.

Milipuko hiyo imetokea katika  kitongoji cha   washia kinachoitwa  Shia shrine na haijaeleweka kama walengwa walikuwa ni washia au Majengo ya usalama ya serikali yaliyopo maeneo hayo.kwa mujibu wa waasi wamesema watu 7 ndiyo waliouawa.
Licha ya mapigano ya kuipinga serikali kumekuwepo na mgawanyiko wa waislamu wa Kisuni na Washia ambapo imehofiwa kuwa wasuni wana lengo la kuwashambulia washia.

POLISI WAWAUA TENA WACHIMBA MIGODI KWA RISASI AFRIKA KUSINI


Jimbo la  Zulu Natal

 KWA ZULU NATAL-AFRIKA KUSINI,
Wachimba migodi wawili wameuawa na polisi nchini Afrika Kusini, wakati wa maandamano katika mgodi mmoja nchini humo , ikiwa ni tukio la hivi karibuni na vurugu mbaya.
Polisi wametuhumiwa kwa kuwafukuza wachimba migodi hao na kuwapiga risasi baada ya kujaribu kuvamia ghala la silaha karibu na eneo la Dannhauser mkoani Kwa Zulu Natal.
Maafisa wanasema kuwa sasa wanachunguza mauaji ya watu wawili.
Migomo kadhaa imekumba sekta ya madini nchini humo na kuvuruga uzalishaji wa madini hali ambayo imeathiri uchumi wa nchi hiyo.
Wachimbaji ambao wamekuwa wakigoma wamekuwa wakikabiliana na poliisi katika vurugu mbaya sana.
Katika tukio mbaya zaidi kuripotiwa , zaidi ya watu 40 waliuawa mwezi Agosti, katika ghasia kati ya polisi na wachimba migodi wa mgodi wa Platinum waliokuwa wanagoma karibu na mgodi wa Rustenburg, ulio umbali wa kilomita 120 Magharibi mwa Johannesburg.
Katika tukio la hivi karibuni, takriban wachimba migodi 100 walikusanyika nje ya mgodi wa Ladybank karibu na Dannhauser.
Polisi walidaia kuwa baadhi ya wachimba migodi hao walijaribu kuvamia ghala la silaha kwa lengo la kuiba silaha hizo.
Walinzi wa serikali walituhumiwa kwa kuwafukuza wafanyakazi hao hadi katika mtaa mmoja wa mabanda na kuwafyatulia risasi pamoja na kuwajeruhi wengine
"Wanaume hao wawili walipelekwa hospitalii lakini walifariki muda mfupi baada ya kuwasili hospitalini’’ taarifa ya polisi ilielezea.
‘‘Polisi wanashika doria katika eneo hilo na wamenasa silaha kutoka kwa walinzi waliokuwa kazini kubaini nani waliofyatua risasi hizo’’
Afrika Kusini ni moja ya nchi inayozalisha madini mengi na ina kiwanda kikubwa cha mkaa.(Chanzo:BBC)

YANGA YAIFUATA SIMBA KILELENI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh1-Xz2FF3S74puVk0p_AN0lYvK0cKtRTvYbJge0CDeIHHNLavDinu0JjY0Kfwwt42d4rvrsVP6WJjDQbfBy8aPuc8jsPK_oeKGKrAFW-rQZOcfZ_LS-NN6QTOZbaOmHlnkkosAxi-0hk/s640/DSC_5634.JPGDAR ES SALAAM-TANZANIA,
TIMU ya Yanga leo imeichapa Mgambo JKT ya Handeni, Tanga mabao 3-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huu, unaifanya Yanga iwe na pointi sawa na mabingwa watetezi, Simba SC waliotoka sare ya 1-1 na Polisi Morogoro uwanja wa Jamhuri

Mpaka timu zinakwenda mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yaliyofungwa  na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na mshambuliaji Didier Kavumbangu.

Cannavaro alifunga kwa kichwa krosi ya Oscar Joshua dakika ya pili, wakati Kavumbangu alimalizia pasi ya Hamisi Kiiza dakika ya 39.

Kipindi cha pili, Yanga walirudi na moto wao tena na kuendelea kuliandama lango la Mgambo JKT na Yanga dakika 34 kupata bao la tatu, mfungaji akiwa ni Jerry Tegete aliyeingia dakika ya 68 kuchukua nafasi ya Kavumbangu.

Mgambo JKT ilipata pigo dakika ya 85, baada ya beki wake wa kulia, Salum Mlima kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumchezea rafu mbaya Mbuyu Twite.

Kikosi cha Yanga; Ally Mustafa ‘Barthez’, Nsajigwa Shadrack, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbangu, Hamisi Kiiza na Haruna Niyonzima.

Mgambo JKT; Godson Mmasa, Salum Mlima, Yassin Awadh, Salum Kipanga, Bakari Mtama, Ramadhani Malima, Chande Magoja, Mussa Ngunda, Issa Kandulu, Fully Maganga na Juma Mwinyimvua

Katika mchezo wa Simba uliochezwa mjini Moro kwenye uwanja wa Jamhuri ilitoka sare ya 1-1 na Polisi na wenyeji wakitangulia kupata bao dakika ya 35 kupitia kwa Mokili Rambo na Amri Kiemba alisawazisha dakika ya 57.