Sunday, September 16, 2012

POLISI WAWASHAMBULIA TENA WACHIMBA MIGODI AFRIKA KUSINI



http://www.aljazeera.com/mritems/Images/2012/9/16/2012916113248805734_20.jpg
MARIKANA,AFRIKA KUSINI.
Polisi Afrika kusini wamewashambulia kwa risasi za mipira na mabomu ya machozi wanamigodi waliokuwa wakiandamana kudai ongezeko la mishahara na kupinga mashambulizi ya polisi dhidi yao hapo Jumamosi ya jana.

Maandamano hayo yalikuwa ya amani ambapo waandamanaji walibeba fimbo badala ya mapanga kama mwezi uliopita yalipotokea mauaji ya wanamgodi 45.Polisi wamesema wamevuruga maandamano hayo kwa sababu yalikosa kibali na leo wamewaomba wanamgodi hao kuachana na maandamano hayo pamoja na mikusanyiko yoyote isiyo halali.

Katika tukio hilo la jana polisi licha ya kusambaratisha maandamano hayo pia walipekua vyumba vya wanamgodi wa mgodi wa Marikana ambapo wanadai kukamata visu, mapanga,madawa ya kulevya na silaha nyingine za kijadi na kuwakamata watu 12 kwa kosa la kukutwa na silaha pamoja na madawa hayo.

Migomo katika mgodi huo imeendelea baada ya kushindwa kufikiwa kwa makubaliano kati ya wamiliki wa mgodi huo na wafanyakazi wanaodai kuongezwa kwa mishahara, hali iliyoyumbisha bei ya Platinum katika dunia na kuchochea migomo katika migodi mingine 6 nchini humo.

No comments:

Post a Comment