Thursday, September 6, 2012

BILL CLINTON AMBEBA OBAMA.



NORTH CAROLINA-MAREKANI,
Rais mstaafu wa Marekani Bw.Bill Clinton amewaambia wamarekani na dunia nzima kuwa anamwamini rais Obama kwa 'moyo wake wote' katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii hasa baada ya alichokifanya katika miaka yake minne ya uongozi na anastahili kuchaguliwa tena.

Rais huyo mstaafu alikuwa akizungumza katika mkutano wa chama cha Democratic katika uwanja wa Time Warner Cable Arena. huko North Carolina.
Clinton amesema hakuna rais ambaye angeweza kuhimili kuurekebisha uchumi mbovu alioukuta rais Obama kama alivyouokoa rais huyo,
"hakuna rais ambaye angeweza kuurekebisha uchumi na madhara yake siyo mimi au walionitangulia" alisema Clinton.

 Clinton amesema Obama amejenga misingi ya uchumi imara na wa kisasa kwa ustawi wa Marekani akiongeza kuwa hata watu wasipomwamini anachokisema yeye wajue kuwa anamwamini rais huyo kwa moyo wake wote.

Chama hicho cha Democrat kipo katika mkutano wake kuelekea uchaguzi ambapo hotuba hiyo ya Clinton inaonekana kumuinua rais Obama hasa kutokana na kukubalika kwa Rais huyo mstaafu ambaye alikuwa na rekodi nzuri ya uchumi enzi za utawala wake na ambaye ni moja ya watu maarufu na wanopendwa zaidi nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment