Wednesday, September 19, 2012

URUSI YAIAMURU MAREKANI KUSIMAMISHA MISAADA INAYOIPA.

 

Moscow-Urusi,
Serikali ya Urusi imelipiga marufuku shirika la kutoa misaada la Marekani USAID nchini humo kwa kile ilichodai mbinu za shririka hilo kuvisaidia vikundi vinavyotaka kubadilisha tamaduni za kisiasa za ndani na kuathiri uchaguzi wa nchi hiyo.

waziri wa mabo ya nje wa Urusi amesema katika taarifa yake kuwa shirika hilo linajaribu kubadili siasa za Urusi, zikiwemo uchaguzi na vyama mbali mbali vya umma kwa kutoa misaada.

Uamuzi huo utakuwa ni pigo kubwa kwa Rais Obama ambaye anakabiliwa na uchaguzi mwezi Novemba mwaka huu na anafanya kila juhudi kurudisha uhusiano mzuri na moja ya maasimu wake hao wa zamani.

Kwa upande wake serikali ya Marekani kupitia kwa msemaji wa Ikulu bi.Victoria Nuland imesema uamuzi huo wa Urusi hautakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa nchi hizo ikisisitiza kuwa Marekani  itaendeleza juhudi zake za kuimarisha demokrasia, haki za binadamu na maendeleo nchini Urusi.


No comments:

Post a Comment