Friday, February 28, 2014

BENKI YA DUNIA YAISIMAMISHIA UGANDA MSAADA-Ni matokeo ya kura ya kupinga ushoga.

Benki ya dunia imesitisha mkopo wa dola milioni 90 kwa Uganda wa kuimarisha sekta ya afya kufuatia kupitishwa kwa sheria inayoharamisha ushoga na kutoa adhabu kali kwa watakaopatikana na hatia
Hatua hiyo ya benki ya dunia haikutarajiwa na wengi kwani taasisi hiyo mara nyingi hujiepusha kuingilia masuala ya ndani ya kisiasa ya nchi wanachama au kuhusiana na masuala kama haki za mashoga, kuepuka kuzishurutisha nchi wanachame wake 188.
Hata hivyo msemaji wa benki hiyo David Theis amesema katika barua pepe kuwa wamesitisha mradi huo wa kuboresha sekta ya afya ya Uganda hadi watakapoufanyia tathmini na kuhakikisha malengo yake ya maendeleo hayataathiriwa na sheria hiyo mpya ya kuharamisha ushoga.
Rais wa benki hiyo Jim Yong Kim amewatumia wafanyakazi wake barua akisema benki ya dunia inapinga ubaguzi na itawalinda wafanyakazi wake wote na kuongeza kupitishwa kwa sheria hiyo ya Uganda sio nchi ya kwanza kufanya hivyo kwani ushoga umeharamishwa katika nchi 83 na zaidi ya nyingine 100 zinawabagua wanawake.
Mkopo ulikuwa uimarishe sekta ya afya
Licha ya kusimamishwa kwa mkopo huo wa dola milioni 90,benki ya dunia bado ina miradi mingine nchini Uganda ya kiasi cha dola bilioni 1.56. Mkopo huo ulitarajiwa kuidhinishwa hapo jana na ulipaswa kuangazia miradi ya kuboresha afya ya uzazi,afya ya watoto wachanga na uzazi wa mpango
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Serikali ya Uganda haina wasiwasi
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo amesema Uganda inaweza kujiendeleza bila ya misaada kutoka nchi za magharibi na kuongeza Uganda haina wasiwasi na hatua hizo kwani ni wakati kwa Afrika kupinga ukoloni, utumwa na ubabe kutoka magharibi.
Mwanaharakati ambaye amekuwa katika mstari wa mbele kuwatetea mashoga nchini Uganda Frank Mugisha alikutana na maafisa wa ngazi ya juu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani mjini Washington hapo jana kuomba usaidizi utakaowalinda mashoga.
Ofisi ya kutetea haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa umelaani kuchapishwa kwa majina ya watu wanaodaiwa kuwa mashoga nchini Uganda katika gazeti moja la udaku nchini humo na kuonya hatua hiyo inakiuka haki ya kuwa na faragha na kuonyesha wazi kuwa maisha ya mashoga yamo hatarini.
Kiongozi wa upinzani Uganda Kizza Besigye ameishutumu serikali kwa kutumia suala hilo kuwahadaa raia wa nchi hiyo ili wasiangalie masuala muhimu kama ufisadi au kuwepo kwa jeshi la Uganda Sudan Kusini.(E.L)

Thursday, February 27, 2014

Homa ya nguruwe yalipuka tena Mbeya

 
Ugonjwa wa homa ya nguruwe umelipuka tena mkoani Mbeya na kuua zaidi ya nguruwe 900 katika wilaya za Mbeya na Rungwe.

Mganga Mkuu wa Mifugo Mkoani Mbeya, Solomon Nong'ona akizungumza na NIPASHE jana alisema, ugonjwa huo umerudi tena baada ya kuzuka kwa mara ya kwanza Januari mwaka huu na kutokomezwa.

Alisema kufuatia kuzuka tena kwa ugonjwa huo, serikali kupitia sekta ya mifugo imepeleka dawa mkoani humo ambazo zinasaidia kupunguza kasi ya kuenea.

Nong'ona  alisema kufuatia kuzuka kwa ugonjwa huo wananchi nao wanajitahidi kununua dawa hizo ili kuudhibiti na kuwakinga nguruwe wanaowafuga.

Alisema ugonjwa wa homa ya nguruwe  bado haijathibitika kuwa na madhara kwa binadamu, hivyo wananchi wanaruhusiwa kula nyama ya nguruwe lakini aliyechinjwa katika machinjio rasmi na kuthibitishwa na daktari wa mifugo.

"Nguruwe hawa wanaweza kuliwa lakini wananchi wawe waangalifu kula nyama hizo kwani kula myama ambaye amekufa mwenyewe ni hatari kwani huenda amekufa kwa ugonjwa mwingine," alisema Nong'ona.

Alisema ugonjwa huo ulianza katika wilaya ya Mbeya na baadaye katika wilaya ya Rungwe.
CHANZO: NIPASHE

Monday, February 24, 2014

Milipuko ya mabomu yarindima Z’bar


Zanzibar. Watu wanne wamejeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar.
Katika moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Majeruhi wawili wamelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja.
Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Mkoa wa Kusini Unguja, Hamad Said Masoud alisema mlipuko wa kwanza ulitokea juzi katika eneo la Fuaoni Maili Nne wakati watu wasiojulikana waliporusha kitu kinachoaminika kuwa ni bomu wakati waumini wa Kanisa la Evangelist wakiendelea na ibada ya Jumapili.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema tukio la juzi, kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kilirushwa wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada na kutoa mlipuko na kishindo kikubwa. Alisema wakati wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo, milipuko mingine mitatu ilitokea jana.
Katika mlipuko wa kwanza kwa jana uliotokea saa 6.30 mchana katika kituo kimoja cha fundi vyuma aliyetambulika kwa jina la Juma Abdallah huko Unguja Ukuu ndiko kulikokuwa na watu waliojeruhiwa.
Waliojeruhiwa katika tukio hilo ni Pandu Haji Pandu aliyekatika mguu na Shaaban Khamis Ibrahim ambaye aliumia sehemu za kiuno.
Hamad alisema mtu mmoja aliokota chuma kizito na kukipeleka kwa fundi akitaka atengenezewe nanga kwa ajili ya uvuvi.
Alisema mhunzi huyo alipokea kazi hiyo na alipokuwa akijiandaa kwa matengenezo ndipo mlipuko huo ulipotokea. Mlipuko huo ulitokea sambamba na mwingine katika Mgahawa wa Mercury’s uliopo Malindi, Mkoa wa Mjini Magharibi na kusababisha huduma za chakula kusitishwa kwa muda.
Tukio la mwisho lilikuwa saa 7:15 mchana katika Kanisa la Anglikana, Mkunazini. Katibu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Zanzibar, Nuhu Saranya alisema: “Nilisikia kishindo cha mlipuko, wakati nikitafakari ni kitu gani hicho, nikasikia mlipuko wa pili nje ya kanisa letu,” alisema.
Mmoja wa majeruhi, Mohamed Ibrahim alisema hakujua kilichotokea huku akilalamika kuwa masikio yake hayasikii vizuri kutokana na kishindo hicho.

Friday, February 21, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE-WASICHANA WATESA-LINK HII HAPA.

Watahiniwa wa kike wamefanya vizuri kwa kuchukua nafasi saba kati ya 10 za juu, huku Shule ya Marian Girls ya Pwani ikiongoza kwa kuwa na wanafunzi wanne.
Mwanafunzi aliyeongoza ni Robina Nicholaus wa Shule ya Marian Girls, akifuatiwa na Magrath Kakoko wa St Francis (Mbeya) wakati wa tatu ni Joyceline Marealle kutoka Shule ya Canossa (Dar es Salaam).
Wengine ni Safarina Mariki na Abby Sembuche wa Marian Girls, wakati wavulana pekee kwenye wanafunzi 10 bora ni Sunday Mrutu kutoka Anne Marie (Dar es Salaam) na Nelson Rugola Anthony na Emmanuel Mihuba Gregory wa Kaizirege (Kagera).
Wanaofuata ni Janeth Urassa kutoka Marian Girls (Pwani) na Angle Ngulumbi wa St Francis (Mbeya).
Wasichana 10 bora
Wasichana waliofanya vizur kwenye mtihani huo wameongozwa na Robina Nicholaus (Marian Girls), Magrath Kakoko (St Francis), Joyceline Leonard Marealle (Canossa), Safarina W Mariki, Abby T Sembuche na Janeth Urassa (Marian Girls).
Wengine ni Angle Ngulumbi (St Francis), Getrude James Mande wa Precious Blood (Arusha), Violet Mwasenga wa St Francis na Catherine Swai kutoka Marian Girls.
Wavulana 10 Bora
Wavulana waliofanya Vizuri ni Sunday Mrutu wa Anne Marie, Nelson Rugola Anthony na Emanuel Mihuba Gregory wote kutoka Kaizirege, Razack Hassan wa St Matthew’s (Pwani) na Hamis Msangi kutoka Eangles (Pwani).
Wengine ni Joshua Zumba wa Uwata (Mbeya), Brian Laurent na Mohamed Ally wa Marian Boys (Pwani), Shahzill Msuya wa St Amedeus (Kilimanjaro) na Shabani Hamisi Maatu wa Mivumon Islamic Seminary (Dar es Salaam).

KAMPENI BUNGE LA KATIBA ZAANZA CHINICHINI-Sitta na Membe wahusishwa.


Dodoma,
Wakati ratiba ya shughuli za Bunge Maalumu la Katiba, ikitarajiwa kutangazwa rasmi siku ya uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa bunge hilo, jana baadhi ya wajumbe walikuwa wakifanya kampeni za wazi ndani ya Ukumbi wa Bunge. Ratiba ya uchaguzi ilitarajiwa kutangazwa jana jioni na ingeonyesha ni lini Rais Jakaya Kikwete, atalizindua bunge hilo na kuelezea siku kamili ya uchaguzi wa viongozi wake.


Ndani ya ukumbi jana, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), alionekana akizungumza na wajumbe, jambo ambalo baadhi ya watu wamelitafsiri kuwa ni kufanya kampeni. Chenge ni mmoja wa makada wanaotajwa kuwania nafasi hiyo.


Mwingine anayetajwa ni Mbunge wa Urambo Mashariki ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.


Wakati Chenge akiendelea na kampeni zake, Sitta alitumia muda mwingi kuzungumza na wajumbe ambao wengi walikuwa wakimfuata mahali alipoketi na baadaye, alionekana akiwazungukia wajumbe.


Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde, alisema hana jambo lolote la kufanya juu ya mapenzi yake kwa Sitta kwani ndiye anayeweza kuendesha shughuli hizo.


“Mimi Lusinde, kwa mapenzi yangu kabisa nasema kuwa kama jina la Sitta litachomoza basi lazima nimsaidie kuhakikisha anakalia kiti hicho kwa kuwa naona anaweza kuliko wengine,” alisema Lusinde.


Alisema kuwa bunge hilo limesheheni wataalamu wa sheria waliobobea na ambao kila mmoja anaweza kuifanya kazi hiyo kwa uaminifu, lakini akasisitiza kwamba kwa kuwa anayetakiwa ni mmoja basi angetamani nafasi hiyo imwendee Sitta.


Mjumbe mwingine kutoka katika Bunge la Muungano ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe, alisema kuwa kumchagua Sitta ni sawa na kumsaliti Chenge ambaye ni jirani yake na wanakaa viti karibu bungeni.

Chanzo:Mwananchi.

Wednesday, February 19, 2014

LOWASSA NA WENZAKE WATIWA KITANZINI-WAFUNGIWA KUGOMBEA UONGOZI CCM.

Dar es Salaam. Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imetangaza uamuzi mzito dhidi ya wanachama wake sita ambao hivi karibuni waliitwa na Kamati Ndogo ya Maadili na kuwahoji kutokana na tuhuma za kuanza kabla ya wakati kampeni za Uchaguzi Mkuu wa urais wa mwaka 2015.
CCM imewatia hatiani vigogo wote sita kwa makosa ya kujihusisha na kampeni za uchaguzi kabla ya wakati, hivyo kuwafungia kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho kwa miezi 12, pia wakiwa chini ya uangalizi.
Waliokumbwa na adhabu hiyo ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe.
Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari jana alisema wanachama hao wote sita walitiwa hatiani kwa makosa ya kuanza kampeni za kuusaka urais wa 2015 kabla ya wakati jambo ambalo ni kinyume na taratibu za chama hicho, hivyo kutoa onyo kali. Adhabu ya onyo kali kwa mujibu wa taratibu za chama hicho inamaanisha kuwaweka chini ya uangalizi kwa miezi 12 ili kuhakikisha hawajihusishi na vitendo vyovyote vinavyokwenda kinyume na misingi ya chama hicho, vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
“Mwanachama aliyepewa onyo kali atakuwa katika hali ya kuchunguzwa kwa muda usiopungua miezi 12 ili kumsaidia katika jitihada zake za kujirekebisha,” alisema Nnauye.
Hatua hiyo ya CCM imezitia doa harakati za vigogo hao, kwani watatumikia adhabu yao hadi Februari 2015 na wakati wote watakuwa wakichunguzwa mienendo yao.
Nnauye alisema makada hao kwa kuanza kwao kampeni za kutafuta kuteuliwa kuwania urais kabla ya wakati ni kinyume na kanuni za uongozi na maadili za CCM, toleo la Februari 2010, Ibara 6 (7)(i).
“Wamethibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii. “Vitendo vya namna hii ni kosa kwa mujibu wa kanuni za uongozi na maadili za CCM toleo la Februari 2010, Ibara kadhaa za kanuni hizo,” alisema Nnauye.
Alisema: “Kamati Kuu baada ya kuthibitisha makosa hayo, imewapa watu wote sita waliohojiwa adhabu ya onyo kali na kuwataka wajiepushe na vitendo vinavyokiuka maadili na iwapo wataendelea na vitendo hivyo chama kitawachukulia hatua kali.”
Alisema Kamati Kuu imeiagiza kamati ya maadili kuwachunguza mawakala na watendaji wa wanachama hao waliokuwa wakiratibu shughuli mbalimbali ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu hatua inayolenga kuhakikisha chama hakigawanyiki.
Nnauye alisema Ibara 6 (2) (1-5) ya maadili ya viongozi wa chama hicho inawazuia kutoa michango, misaada, zawadi za aina yoyote, kukusanya michango na kufanya kampeni bila ya kupata kibali kutoka kamati ya siasa ya halmashauri ya eneo husika.
CHANZO:MWANANCHI.

BUNGE LA KATIBA VITUKO TUPU.

Mh.Pandu Amir Kificho

MWENYEKITI wa CHADEMA, Freeman Mbowe ambaye pia ni mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, jana alinusuru mchakato wa uchaguzi wa mwenyekiti wa muda baada ya kuibuka vituko.
Mbowe katika ushauri wake alitaka mchakato huo uanze upya kwa karatasi za kura kugawiwa kwa utaratibu makini ili kila mmoja apige kura huku milango ikiwa imefungwa.
Ushauri wake ulikubaliwa na mwenyekiti wa kikao hicho ambapo mchakato ulifanyika upya kwa usimamizi mkali wa polisi, huku Bunge likiahirishwa kwa robo saa kutoa fursa ya kura kuhesabiwa.
Awali vituko kejeli na malumbano vilitawala zaidi uchaguzi huo wa Bunge lililoanza vikao vyake jana mkoani hapa.
Dalili za kuvurugika kwa uchaguzi huo zilianza kuonekana mapema kutokana na idadi kubwa ya wajumbe kusimama na kuwasha vipaza sauti bila kufuata taratibu walizoambiwa mapema.
Katika uchaguzi huo Mheshimiwa Pandu Amir Kificho alishinda nafasi ya Mwenyekiti wa muda wa Bunge la Katiba baada ya kupata kura 393 sawa na 69.19% ya kura 558 zilizopigwa na kuwaacha kwa mbali Costa Mahalu na Magdalena Rwebangira ambao wamepata kura 84 kila mmoja ambazo ni sawa na 14.79%
Kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba, mwenyekiti huyo wa muda atakuwa na jukumu la kuandaa na kupitisha kanuni za Bunge hilo zitakazotumika katika mijadala mbalimbali.

Tuesday, February 18, 2014

Bunge lagawanyika!

Dodoma. Bunge Maalumu la Katiba, linaanza leo mjini hapa, huku kukiwa na mpasuko mkubwa miongoni mwa wajumbe, unaotokana na misimamo tofauti.
Kipengele kinachowagawa wajumbe hao ni Muundo wa Serikali uliopendekezwa katika Rasimu ya Katiba.
Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, iliyokutana kwa siku mbili Mjini Dodoma imeondoka na msimamo wa kutaka wajumbe wake wa bunge hilo kutetea hoja ya Serikali mbili huku Chadema na CUF vinataka Serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila hivi karibuni alikaririwa akitishia kwenda mahakamani kuzuia mchakato mzima wa Katiba hadi iundwe Serikali ya Tanganyika.
Msimamo wa CCM
Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya CCM Mjini Dodoma jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye alisema msimamo wa chama chake haujabadilika na kwamba wanafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa Tanzania inabaki na mfumo wa Serikali mbili.
“Hatuwezi kukataa mawazo ya watu wengine, lakini kikubwa ambacho tunakisimamia ni kuhakikisha kuwa tunabaki na Serikali mbili na ndiyo maana tumezungumza na wajumbe wa NEC na leo (jana), tunakutana na wabunge wetu wa Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar,” alisema Nape.
Kuhusu kero zinazolalamikiwa na pande zote, alisema CCM inafahamu kero nyingi na kwamba upande wa Bara kuna kero nane na Zanzibar idadi kama hiyo.
“CCM imetengeneza mfumo mzuri wa kuziondoa kero hizo ndani ya Serikali mbili siyo kama wenzetu ambao wamebuni Serikali tatu eti iwe dawa ya kumaliza kero hizo kitu ambacho hakiwezekani,” alisema huku akiwataka wajumbe na Watanzania kwa jumla, kulumbana kwa hoja badala ya kupiga kelele.
Malecela aipinga CCM
Hata hivyo, kada mkongwe aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, John Malecela alitofautiana na msimamo huo akisema si sahihi kwa viongozi kuwatungia wananchi Katiba kama inayoonekana kufanywa na baadhi yao.
Akizungumza kwa simu kutoka Nairobi, Kenya, Malecela alisema: “Kama tuliona inafaa kuwatungia wananchi Katiba, hakuna ulazima wa kuwataka maoni yao. Mimi ni kiongozi na Katiba hii ni ya wananchi, nisingependa kutoa maelekezo ya nini kifanyike, kama viongozi wengine wanavyofanya.

Monday, February 17, 2014

Boko Haram waua 105 Nigeria.


Maafisa katika eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria wanasema kuwa zaidi ya watu mia mmoja wameuwawa katika shambulizi linaloshukiwa kutekelezwa na wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
Shambulizi hilo katika kijiji cha Izghe katika jimbo la Borno linajiri siku nne pekee baada ya watu 39 kuuwawa katika shambulizi jingine.
Seneta wa jimbo la Borno Mohammed Ali Ndume ameiambia BBC kwamba watu mia moja na sita waliuwawa katika shambulizi hilo la hivi punde.











Amesema takriban wanamgambo mia moja walivamia mji wa Izghe jumamosi usiku. Wananchi waliokuwa wakikimbia mashambulizi hayo wamethibitisha kuwa takriban wanaume thelathini walikusanywa na kisha kupigwa risasi.
" Waasi hao walikuja karibu saa tatu usiku na kisha kuwakusanya wanakijiji katika makundi, hususan vijana. Kisha wakaenda nyumba hadi nyumba na kuwauwa wanaume, na kuchukuwa kila kitu walichokuwa nacho,'' amesema Ali Ndume.

"Wamewauwa watu 106. 105 mia moja na tano ni wanaume na mwanamke mmoja kikonge aliyekuwa akijaribu kumlinda mjukuu wake wa kiume. Nadhani alipigwa risasi na kisha akafa."
Kisha wanamgambo hao walienda nyumba hadi nyumba wakiwauwa watu-wengi wao wakiwa ni wanaume. Baadhi walipigwa risasi huku wengine wakichinjwa.
Msemaji wa jeshi hakutoa maelezo kuhusu kisa hicho cha hivi punde lakini ameiambia BBC kwamba jeshi haliwezi kuwa kila mahali na kusema kuwa wanamgambo hao ni watu wa kuhamahama.


Sunday, February 16, 2014

Wachimba migodi wakwama mgodini A.Kusini


Waokozi nchini Afrika Kusini wanafanya kila juhudi kuwaokoa wachimba migodi wengi wanaohofiwa kukwama ndani ya mgodi wa dhahabu.
Waokozi hao wanasema kuwa wameweza kuwasiliana na wachimba migodi hao wanaokisiwa kuwa 30.
Wamekwama kutokana na mawe makubwa yaliyo ndani ya mgodi huo karibu na mgodi mwingine mpya wa dhahabu viungani mwa mji wa Johannesburg.
Wameelezea kuwa wachimba migodi wengine miambili wako ndani ya machimbo ingawa haijulikani ikiwa wamejeruhiwa.

KIKWETE: UNYONGE CCM BASI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wa chama hicho kuacha unyonge na kusema uvumilivu una kikomo chake.
Aliyasema hayo jana wakati anafungua kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM, kilicholenga kuweka msimamo wa chama kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ambayo inaanza kujadiliwa Jumanne wiki ijayo.
"Tuna uchaguzi mdogo, Iringa, Kalenga, tumeshapata mgombea na tumefanya hiyo kazi kwa niaba yenu kwa sababu hatukupata muda wa kuitisha Kikao cha Halmashauri Kuu, lakini mmetupatia mamlaka ya kufanya hivyo na Katiba imetupa fursa ya kufanya uteuzi kwa niaba yenu,"alisema.
CCM imemteua Godfrey Mgimwa ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Dk William Mgimwa, kupeperusha bendera katika uchaguzi mdogo utakaofanyika baadaye mwaka huu. Dk Mgimwa hadi anafariki dunia alikuwa Waziri wa Fedha.
Uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kalenga lililopo mkoani Iringa unatarajiwa kufanyika Machi 16, mwaka huu, huku tayari vyama vya CCM na Chadema vikiwa vimetaja wagombea wake, Chadema kikiwa kimetangaza, Grace Tendega Mvanda.
Rais Kikwete alisema chama hicho kinashindana na vyama vingine katika uchaguzi huo mdogo.
"Tunashindana na wenzetu wagomvi, maana wao ugomvi ndiyo sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa,"alisema Kikwete bila kutaja chama chochote cha siasa kwa jina.
"Tulizungumza nalo hilo kwenye Kamati Kuu, tulikubaliana kuacha unyonge. Ndiyo, kwenye Kamati Kuu tumekubaliana, tumesema jamani watu wote waende wakaseme tumekubaliana kuacha unyonge," alisema huku akicheka na kupigiwa makofi na wajumbe wa Nec.
Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, alitolea mfano wa tukio lilitokea Kahama mkoani Shinyanga, ambapo kijana mmoja alitolewa macho kwa bisibisi, na tukio la Igunga ambapo kijana mmoja alimwagiwa tindikali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
"Acheni unyonge na hata katika taarifa ya habari leo (jana) mtoe hivyo hivyo. Na mwache habari zote mseme hii tu (waandishi wa habari). Uvumilivu una ukomo wake," alisema huku wajumbe wakiendelea kumpigia makofi.
"Nalisema kwa sababu yanayotokea yanasikitisha sana. Pale Igunga kijana yule wamemwagia tindikali, pale Kahama kijana ametolewa macho kwa bisibisi,"alisema.
Hata hivyo, Rais Kikwete aliwataka wanachama wa CCM kujipanga vizuri katika uchaguzi huo, ili kuhakikisha wanapata ushindi mnono.
"Mpaka sasa kwa dalili tulizonazo hatuna mgawanyiko wala hakuna misukosuko maana lile la Arumeru (uchaguzi mdogo katika Jimbo la Arumeru Mashariki) lilikuwa na misukosuko tangu tumeanza hadi tumemaliza," alisema.
Katika uchaguzi huo, uliofanyika Aprili mosi, 2012 mgombea wa Chadema, Joshua Nassari aliibuka mshindi baada ya kumshinda Sioi Sumari wa CCM ambaye ni mtoto wa marehemu Jeremiah Sumari, aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi mwaka 2008 hadi 2010.
Alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi na wanachama wa CCM katika kata 23, ambazo CCM iliibuka na ushindi na kuwataka kuweka nguvu zaidi katika kuzikomboa kata nne zilizoangukia mikononi mwa wapinzani.
Kata ambazo wapinzani walishinda ni Sombetini (Arusha Mjini), Kiboroloni (Moshi Mjini), (Njombe Mjini),zote zilichukuliwa na Chadema. Kilelema mkoani Kigoma (NCCR Mageuzi).
Aidha, Rais Kikwete alisema awali wakati wanaahirisha kikao cha Nec kilichopita, walikubaliana watakuwa wakihamia mikoani kufanya vikao hivyo ambapo Mbeya waliomba kuwa wenyeji na walikubaliwa.
Hata hivyo, alisema waliamua kufanya tena kikao hicho mjini hapa, kwa sababu ya agenda watakazozizungumza kwenye kikao hicho ambazo ni suala linalohusu mchakato wa Katiba Mpya.
"Ili tutakapoyamaliza, tujue tuweke misimamo gani itakayokwenda kwenye Bunge la Katiba. Haina maana kuwa ile agenda yetu ya Mbeya tumeifuta, ahadi iko palepale, kikao kitakachofuata cha kawaida kitafanyikia Mbeya,"alisema.
Awali Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akimkaribisha Rais Kikwete, alisema kuwa wajumbe wa Nec ni 372, lakini waliohudhuria walikuwa ni 368 (sawa na asilimia 98.3) hadi kikao kinafunguliwa.

Saturday, February 15, 2014

Search This Blog Saturday, February 15, 2014 CAF CHAMPIONS LEAGUE: KIKOSI CHA YANGA KINACHOANZA LEO DHIDI YA KOMOROZINE DE DOMONI



1. Deogratias Munish "Dida" - 30
2. Mbuyu Twite - 6
3. Oscar Joshua - 4
4. Nadir Haroub "Cannavaro" - 23
5. Kelvin Yondani - 5
6. Athuman Idd "Chuji" - 24
7. Saimon Msuva - 27
8. Haruna Niyonzima - 8
9. Didier Kavumbagu - 7
10. Mrisho Ngasa - 17
11. Hamis Kizza - 20

Subs:
Barthez, Juma Abdul,Luhende, Rajab, Domayo, Dilunga n Bahanuzi

chanzo:Shaffih Dauda.

Wednesday, February 12, 2014

Sheria ya ndoa sasa kupigiwa kura ya maoni

Bagamoyo. Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Kairuki amesema kuwa Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 iko kwenye mchakato wa kurekebishwa kutokana na utata unaokinzana na sheria nyingine za masuala ya kijinsia.
Akizungumza baada ya ufunguzi wa warsha ya siku moja ya waandishi wa habari na sheria na sera zinazohusu ukatili wa kijinsia iliyoandaliwa na Taasisi ya Champion na Engender Health wilayani Bagamoyo juzi, Kairuki alikiri kuwepo kwa utata wa sheria hiyo jambo linaloendelea ukatili hasa kwa wanawake.
“Utata wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ulijadiliwa katika Baraza la Mawaziri na walishafika mbali. Lakini ilionekana kwa kuwa masuala ya ndoa na mirathi yanagusa mila, desturi, dini na tamaduni za watu, ilionekana siyo rahisi kutunga sheria haraka,” alisema Kairuki na kuongeza:
“Wapo wanaosema mtoto hawezi kuolewa akiwa na miaka 14 na wapo wanaosema anaweza. Baraza la Mawaziri liliamua kuwa kuwe na kura ya maoni (white paper).”
Hata hivyo alisema kuwa wakati mchakato huo ukikaribia kuanza uliingiliana na mabadiliko ya Katiba. Hivyo alisema kura hiyo ya maoni itafanyika baada ya kupatikana kwa Katiba Mpya.
Awali akifungua warsha hiyo, Kairuki alisema kuwa Serikali imechukua hatua za kukabiliana na ukatili wa kijinsia ikiwa pamoja na kuanzisha dawati la jinsia na watoto kupitia Jeshi la Polisi na timu za ulinzi na usalama wa watoto kupitia Idara ya Ustawi wa Jamii.
Akitoa mada katika warsha hiyo, Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya Engender Health, Dk Monica Mhoja alisema Serikali ya Tanzania inasifika kwa kuridhia sheria na mikataba ya kimataifa kuhusu ukatili wa kijinsia, lakini hazitekelezwi ipasavyo.
“Tunapokuwa kwenye majukwaa ya kimataifa, Tanzania tunasifika kwa kuridhia sheria na sera nyingi, wanapotuhoji kuhusu utekelezaji inakuwa shida,” alisema Dk Mhoja.
Chanzo:Mwananchi.

Adhabu kwa vigogo CCM-Wapo Lowassa,Makamba,Wassira,Sumaye.

Dodoma. Vigogo sita ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaanza kuhojiwa leo, huku wakikabiliwa na adhabu kadhaa ikiwamo ya kufungiwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwa watapatikana na hatia ya makosa yanayowakabili.
Kamati ya Maadili na Usalama ya chama hicho, inaanza kikao chake mjini Dodoma, chini ya uongozi wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula kuwahoji makada hao ambao ni wale wanaotajwa kuonyesha nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa 2015.
Miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuteka kikao hicho ni vitendo vinavyotokana na vita ya urais wa 2015, ambapo kumekuwa na matukio ya makada wa CCM kurushiana maneno hadharani na wengine kutuhumiwa kwa matumizi ya fedha.
Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM zinaruhusu wanachama wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi kutangaza nia zao, lakini zinakataza kampeni kabla ya muda uliowekwa rasmi ambao ni baada ya wagombea wa nafasi husika kupitishwa na vikao vya chama hicho.
Vigogo hao ambao tayari walishapewa barua za kuitwa mbele ya kamati hiyo ni pamoja na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.
Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
Kwa mujibu wa kanuni husika viongozi hao wanaweza kuchukuliwa hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufungiwa kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho kwa miezi sita, 12 au 18, ikiwa watapatikana na hatia katika tuhuma zinazowakabili.
Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema jana kuwa, Kamati Ndogo ya Maadili haina uwezo wa kutoa adhabu za moja kwa moja kwa watuhumiwa hao na badala yake inaweza kutoa mapendekezo ya adhabu kwa Kamati Kuu ya Maadili ambayo inaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
“Kamati ya Mzee Mangula ina mamlaka ya kufuta mashtaka baada ya kumsikiliza mhusika na kupima ushahidi dhidi yake, pale ambapo itaona kwamba pengine mhusika anapaswa kuchukuliwa hatua basi inapeleka mapendekezo katika Kamati Kuu ya Maadili,”alisema Nnauye.

AJALI YA NDEGE YAUA 77 ALGERIA.


Algeria imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kufuatia kuuawa kwa watu sabini na saba kwenye ajali iliyohusiha ndege moja ya Kijeshi Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.

Abiria mmoja alinusurika ajali hiyo iliyohusisha ndege aina ya Hercules C-130 iliyoanguka katika eneo la milima ya Oum al-Bouaghi, ikiwa njiani kuelekea mji wa Constantine.

Ripoti zinasema hali mbaya ya anga ilisababisha ajali hiyo ya ndege.

Rais wa nchi hiyo Abdelaziz Bouteflika amewasifu wanajeshi waliopoteza maisha yao na kuwataja kama wafia dini wa taifa hilo.

Wengi wa abiria sabini na nane waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni maafisa wa kijeshi na familia zao.
Mabaki ya ndege ya jeshi la Algeria iliyoanguka.
Mwanajeshi aliyenusurika, anaripotiwa kuendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Constantine kufuatia majeraha ya kichwa.

Wizara ya Ulinzi imesema kuwa imeunda tume maalum kuchunguza ajali hiyo na kuwa Ahmed Gaid Salah, ambaye ni mkuu wa majeshi na naibu waziri wa Ulinzi atazuru eneo la ajali hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, wizara ya ulinzi imesema kuwa hali mbaya ya anga iliyohusisha kimbunga na mvua kubwa ya barafu ilisababisha ajali hiyo.Runinga ya taifa ilionyesha picha za ajali hiyo.

Awali maafisa wa Ulinzi na shirika hilo la habari liliripoti kuwa watu 103 walikuwa ndani ya ndege hiyo lakini idadi hiyo ilipunguzwa hadi watu sabini na nane.

WAKAZI 200 DAR WAITAKA TANESCO ISHUSHE BEI YA UMEME

tanesco31_e316c.jpg

UMOJA wa wakazi zaidi ya 200 wa Dar es Salaam wametoa siku kumi kwa Shirika la Umeme nchini(TANESCO), pamoja na vyombo vingine vya maamuzi, kubatilisha maamuzi yake juu ya bei mpya ya umeme na irejeshwe bei iliyokuwepo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijijini Dar es Salaam kwa niaba ya wenzake, Kiongozi wa Hoja hiyo, Sheikh Rashid Kayumbo alisema kuwa bei hiyo imekuwa ikiwaumiza watanzania wengi.
Alisema ongezeko la bei ya umeme limesababisha kupanda bei ya bidhaa mbalimbali nchini, hivyo kuchochea zaidi ukali na ugumu wa maisha.
"Tunawasihi watanzania wote wawe na subira na wawe na amani kabisa juu ya hoja hii, pia watuunge mkono kwa asilimia 100 kwa ujumla wao, juu ya pingamizi hili na wawe tayari kuelekezwa cha kufanya juu ya pingamizi letu," alisema.
Alisema baada ya siku kumi kumalizika, bila utekelezaji wowote kama walivyotaka, Februari 21 watafanya mkutano mkubwa wenye sura ya kitaifa, ukijumuisha viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa na wabunge kupitisha azimio lao.
"Azimio letu litakuwa ni kususia umeme hadi itakaporejeshwa bei ya zamani, hii ni kuliko maandamano ya aina yoyote," alisema.
Alisema walifikiri kwamba kupandishwa kwa bei hiyo, huduma zitaboreshwa, lakini hadi sasa huduma za TANESCO ni za ubabaishaji na shirika hilo halina uhalali wa kupandisha bei ya umeme.
“Sisi wakazi wa jiji la Dar es Salaam wa wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni kwa niaba ya Watanzania wote nchi nzima, tunatoa siku kumi kwa Tanesco pamoja na vyombo vingine vya maamuzi katika suala hili kubatilisha maamuzi yake juu ya bei mpya ya umeme, na irejeshwe bei yetu iliyokuwepo kabla ya sasa”, alisema.
CHANZO:MJENGWA BLOG.

Tuesday, February 11, 2014

Vigogo sita CCM waitwa Kamati ya Maadili


Dar es Salaam. Vigogo sita ambao wanatajwa kuwa wanajiwinda kwa ajili ya kuwania urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu ujao, wameitwa mbele ya Kamati ya Ndogo ya Maadili ya chama hicho, kwa ajili ya kuhojiwa kwa tuhuma za kukiuka maadili.
Habari ambazo zililifikia gazeti hili jana zinawataja vigogo hao kuwa ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.
Wengine ni Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
“Wote wamepelekewa barua za wito wa kufika mbele ya Kamati ya Maadili inayoongozwa na Mzee Mangula (Philip, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara), ambayo itakutana mjini Dodoma, Februari 14 (kesho kutwa) ,” kilisema chanzo chetu cha habari kutoka Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam na kuongeza:
“Barua hizo zimesainiwa na Mzee Kinana (Abdulrahman, Katibu Mkuu wa CCM) mwenyewe na tayari zimeanza kusambazwa leo (jana) mchana.”
Kamati hiyo ndogo ya maadili, inaundwa na Mangula, Kinana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, Shamsi Vuai Nahodha, Dk Maua Daftari na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Pindi Chana.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye jana alithibitisha kuwapo kwa Kikao cha Kamati ya Maadili Februari 14 pamoja na kuitwa kwa baadhi ya wanachama kwa ajili ya kuhojiwa.
Hata hivyo, hakuwa tayari kutaja majina yao wala idadi ya walioitwa... “Wewe fahamu tu kwamba kikao hicho kitafanyika tarehe hiyo uliyoitaja, lakini masuala ya majina na idadi ya walioitwa yatajulikana kwenye kikao, mimi sina kwa sasa,” alisema Nnauye.
Katika siku za karibuni kumekuwa na vita ya maneno baina ya makada wa chama hicho, wakituhumiana kutangaza mapema kugombea urais kabla ya ruhusa rasmi ya chama.
Kauli za walioitwa
Jana, gazeti hili lilizungumza na baadhi ya walioitwa na wengi wao walisema hawakuwa wamepokea barua za wito huo.
Sumaye kwa upande wake alisema: “Kwa sasa niko Mwanza na sijapata barua yoyote ya kuitwa katika kikao chochote cha chama.”

Sunday, February 9, 2014

Serena akacha Indian Wells

 
HESABU za waaandaaji wa michuano ya tenisi ya Indian Wells BNP Paribas Open kuona nyota namba moja kwa wanawake, Serena Williams, anashiriki kipute cha mwaka huu zimeyeyuka.
Serena ambaye mara ya mwisho kushiriki michuano hiyo ni miaka 13 iliyopita, alisema juzi kuwa hatashiriki baada ya kutafakari kwa kina ushiriki wake.
“Baada ya kutafakari kwa kina, sitaweza kushiriki michuano ya Indian Wells BNP Paribas Open kwa mwaka huu,” alisema nyota huyo huku akiwatakia kila la heri washiriki katika michuano hiyo inayotarajiwa kuwaleta pamoja nyota mahiri wake kwa waume.
Akizungumzia uamuzi wa Serena, Mkurugenzi wa michuano hiyo, Steve Simon, alisema wanamkaribisha katika michuano ya mwaka ujao.

Wanafunzi wawili CBE wafa ajalini.

https://encrypted-tbn2.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcQCG9syU_OnEMKEX2xqVOpJma6BVZQExaF-vgznle2KuMgkkaSOwaHFcA 

WANAFUNZI wawili wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wamefariki dunia jijini Dar es Salaam juzi katika ajali ya gari iliyotokea katika viwanja vya Shabaha.
Akizungumzia ajali hiyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema ilikuwa saa 12 jioni, barabara ya White Sands, Mbezi Beach, baada ya gari lenye namba za usajili T 958 AXK aina ya Carina kuacha njia na kugonga mti.
Kamanda Wambura aliwataja waliofariki dunia eneo la tukio kuwa ni Ibrahim Kaliki (21) mwanafunzi wa CBE Mwanza na Samwel (23) anayesoma CBE Dar es Salaam.
Aliwataja majeruhi wengine katika ajali hiyo kuwa ni Christina Ami (20) mfanyabiashara na Maxon Kimaro (21) mwanafunzi Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kamanda Wambura, gari hilo lilikuwa likiendeshwa na George Deo (21), ambaye ni mwanafunzi wa CBE Mwanza,  likiwa na abiria watano wakitokea Whitesand Hotel kuelekea Barabara ya Bagamoyo.
Alisema gari lilipofika eneo hilo lilimshinda dereva na kuacha njia kisha kugonga mti, kupinduka na kuingia mtaroni.
Kamanda huyo alisema majeruhi wamelazwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo na maiti zote zimehifadhiwa hospitalini hapo huku Jeshi la Polisi likimshikilia dereva kwa mahojiano na uchunguzi wa ajali hiyo.
Chanzo:Mtanzania.

Saturday, February 8, 2014

Raia waanza kuhamishwa Syria.

homs_02492.jpg
Raia wakiwa wamebeba mizigo yao wanaondoka kwenye mji wa Homs.
Awamu ya kwanza ya raia wa Syria waliokuwa wamenasa kwenye maeneo yanayoshikiliwa na waasi mjini Homs imehamishwa huku serikali na waasi wakikubaliana kusitisha mapigano kwa muda kupisha huduma za kibinaadamu.
Televisheni ya taifa imeonesha picha za wafanyakazi wa Shirika la Hilali Nyekundu wakiwasaidia wazee waliodhoofu wakiwa wamefunikwa mablanketi ndani ya basi, huku mwanamke mmoja akiwa kwenye kiti cha maringi akisubiri zamu yake.

Televisheni ya serikali ilisema raia hao walikuwa wakitumika kama "ngao" na "makundi ya kigaidi" - jina linalotumiwa na serikali kuwaita waasi wanaopigania kuing'oa madarakani serikali ya Assad.
Wafanyakazi wa Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa wakiwa na vizibao vya buluu ndio waliosimamia uhamishwaji wa raia hao na gari yenye alama ya Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa ilionekana kuegeshwa karibu na eneo hilo.
Serikali ilikubaliana na kile kilichoitwa "mapumziko ya kibinaadamu" na wanaharakati wa upinzani mjini Homs walisema waasi nao walikubali kusitisha mapigano kwa siku nne.
Jeshi lilianzisha mkururo wa mashambulizi kuyachukua tena maeneo ya Mji Mkongwe mwanzoni mwaka 2012, huku mabomu ya takribani kila siku yakiuwa maelfu ya watu.
Mji huo wa tatu kwa ukubwa nchini Syria na uliopewa jina la "makao makuu ya mapinduzi" na waasi, umekuwa kituo kikuu cha mapambano tangu mwanzoni mwa takribani ya miaka mitatu ya upinzani dhidi ya Rais Bashar al-Assad.
Vyombo vya habari vya serikali vimesema kufikia jioni ya Alhamisi (tarehe 7 Februari), mabasi yalikuwa yameondoka Homs na jumla ya raia 60, wengi wao wanawake, watoto na wazee.
Mwandishi wa shirika la habari la AFP alisema kiasi cha raia 12 walishuka kwenye basi la kwanza kutoka mji huo ulio kwenye mikono ya waasi na ambao umekuwa ukizingirwa na jeshi kwa zaidi ya siku 600.
Hali mbaya ya kibinaadamu
Gavana wa Homs, Talal Barazi, aliiambia AFP kuwa kiasi cha raia 200 walikuwa "tayari kuokolewa jana" (Ijumaa) kwa mujibu wa taarifa zilizopokelewa na Umoja wa Mataifa.
Kuhamishwa kwa watu hao ni sehemu ya makubaliano ya kushangaza kati ya pande hizo mbili yaliyosimamiwa na Umoja wa Mataifa baada ya miezi kadhaa za mazungumzo.
Makubaliano hayo pia yanajumuisha kufikishwa kwa misaada wakati wa kusitishwa kwa mapigano kwa sababu za kibinaadamu.
Hata hivyo, Barazi alisema shehena ya kwanza ya chakula na madawa haitaweza kufikishwa kwa raia hadi Jumamosi (8 Februari).
Wanaharakati wamekuwa wakiripoti mara kwa mara juu ya upungufu mkubwa wa chakula ambapo kiasi cha watu 3,000 - wakiwemo wanawake, watoto na wazee 1,200 - walionasa huko, wanaishi kwa kula mazaituni na majani tu.
Mwanaharakati mmoja, Yazan, ameiambia AFP kupitia mtandao wa Intaneti kwamba wale wanaoondoka wana hisia mchanganyiko. "Kwa upande mmoja, wanafurahia kunusurika lakini pia wanahofia kitakachotokea baadaye, kwani wanaogopa kuwa watakamatwa na kuwekwa ndani na serikali."
Barazi alisema walioruhusiwa kuondoka ni watoto walio chini ya miaka 15, watu wazima wanaume walio na umri wa zaidi ya miaka 55 na wanawake, akiita operesheni hiyo iliyosimamiwa na Umoja wa Mataifa kuwa na mafanikio.
"Kulikuwa na ugumu awali kwa raia kutoka kwenye maeneo yaliyoshikiliwa na waasi kwenye Mji Mkongwe, lakini alhamdulillah kwamba hatimaye waliweza kuondoka," alisema.
Chanzo, dw.de.com/swahili

MALINZI: TUNA MZIGO WA MADENI KUTOKA KWA TENGA

 

 SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limesema changamoto kubwa linaloikabili sasa ni madeni ya mamilioni ya fedha waliyoyarithi kutoka uongozi uliopita wa Rais, Leodegar Tenga.


Akizungumza  katika tathimini yake ya siku 100 tangu alipochaguliwa kuwa rais mpya wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi, alisema madeni hayo ni makubwa ukilinganisha na kipato cha TFF kinachotegemea zaidi mapato ya milangoni ya mechi mbalimbali.



"Madeni tuliyoyakuta ni makubwa, lakini mengine tumegundua ni hewa, hivyo yanafanyiwa uhakiki ili tujue madeni halisi ili tuweze kuyalipa," alisema Malinzi aliyeingia madarakani Oktoba 27, mwaka jana.

"Pia tunafanya mazungumzo na watu wanaoidai TFF ili watupe masharti nafuu ya kulipa madeni hayo."

Kauli ya Malinzi imekuja ikiwa imepita miezi sita tangu TFF ipate aibu ya mabasi yake kukamatwa na Kampuni ya Udalali ya Flamingo ili kufidia deni la zaidi ya Sh50 milioni.


Chanzo:Mwananchi mtandaoni