Monday, February 11, 2013

PAPA BENEDICT XVI ATANGAZA KUJIUZULU


http://l1.yimg.com/bt/api/res/1.2/OghHOUVGAdw5jkaiqHQlag--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9aW5zZXQ7aD0zMzM7cT04NTt3PTUxMg--/http://media.zenfs.com/en_us/News/Reuters/2013-02-11T122658Z_1146797572_GM1E92B1JT301_RTRMADP_3_POPE-RESIGNS.JPG

http://l.yimg.com/bt/api/res/1.2/fBMzX47bwjrUut5Sd2DYZQ--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9aW5zZXQ7aD05MDA7cT03OTt3PTczNg--/http://media.zenfs.com/en_us/News/ap_webfeeds/cef0a2fc2096a524240f6a70670052e7.jpg
 http://l3.yimg.com/bt/api/res/1.2/1bfogd5OFbiezWIzY32kIQ--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9aW5zZXQ7aD01MDY7cT04NTt3PTYzMA--/http://media.zenfs.com/en_us/News/ap_webfeeds/7bca85b520d8a624240f6a70670087f4.jpg
VATICAN-ITALIA,
Kadinali Joseph Ratzinger ama Papa Benedict XVI  ametangaza uamuzi wa kujiuzulu mwishoni mwa mwezi huu baada ya takriban miaka minane akiongoza Kanisa Katoliki kwa hoja kuwa umri wake wa miaka 85 ni mkubwa kiasi kwamba hawezi kuendelea kuhudumu zaidikutokana na kudhoofu kimwili na kiakili.

Makao makuu ya Kanisa Katoliki huko Vatican yanasema yanatarajia Papa mpya atachaguliwa kabla ya mwisho wa mwezi wa tatu, na sherehe za Pasaka.

 Tukio jipya katika karne za hivi karibuni., ambapo papa wa mwisho kujizulu alikuwa ni Papa
Msemaji wa Vatikani Father Federico Lombardi, amesema kuwa hata wasaidizi wa Papa wa karibu mno hawakuwa na fununu juu ya tukio hili.

Kakake Papa huyu mzaliwa wa Ujerumani alipewa ushauri na Daktari wake asifanye ziara nyingine yoyote ya Marekani na kwamba kwa miezi kadhaa Mtakatifu Papa amekuwa akitafakari kujiuzulu.
Akizungumza kutoka nyumbani kwake huko Regensburg, Ujerumani, Georg Ratzinger amesema kuwa Kaka yake alikuwa ameanza kupata shida ya kutembea na kwamba kujiuzulu kwake ni hatua ya kimaumbile.


VIDEO YA PAPA AKITANGAZA KUJIUZULU:

Wakati wa kutawazwa kama Papa, Kadinali Joseph Ratzinger alikuwa mmojawapo wa mapapa wapya kuchaliwa akiwa mwenye umri mkubwa wa miaka 78.
Alitangazwa Papa mnamo mwezi Aprili 2005 kufuatia kifo cha marehemu John Paul wa pili.
Uongozi wake ulitokea wakati wa wimbi kali la ubakaji kulikumba kanisa katoliki katika kipindi cha miongo mingi, ubakaji uliofanywa na watawa dhidi ya watoto wavulana.

Katika taarifa yake, Mtakatifu Papa amesema: "baada ya kujichunguza binafsi na nafsi yangu mbele ya Mola wangu, nimefikia uwamuzi kua uwezo wangu na afya, ukiambatana na umri mkubwa, ni mambo yatakayokwaza jitihada zangu za kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki.

Kuna kipengele katika sheria ya Kanisa kinachosema kuwa kujiuzulu kwa Papa kunakubalika iwapo kitendo hicho kimefanywa kwa hiari na kwa utaratibu unaostahiki.

Hata hivyo kujiuzulu huko kumepokewa kwa hisia tofauti ambapo wapo waliokubaliana na wengine wakionekana kusita akiwemo katibu mkuu wa Papa John Paul II aliyeshikilia wadhifa wake mpaka mwisho wa uhai wake licha ya kuugua,Kadinali Stanislaw Dziwisz ambaye amewaambia waandishi wa habari nchini Polland kuwa "Haikutakiwa  kushuka kutoka katika msalaba".kwa upande wao viongozi wa duni wameupokea kwa hudhuni uamuzi huo ingawa wameuunga mkono.Waziri mkuu wa Ujerumani  Angela Merkel amesema uamuzi wa papa unapaswa kuheshimiwa ikiwa amejiuzulu kwa kujiona ni dhaifu kutekeleza majukumu yake, huku David Cameron waziri mkuu wa Uingereza akisema Papa benedict XVI atakumbukwa kiroho na mamilioni ya wafuasi wa dini".

No comments:

Post a Comment