Sunday, April 6, 2014

Matokeo ya Jumla Uchaguzi mdogo jimboni Chalinze- CCM WATISHA!

CCM 20812 = %86.5 CDM 2628 = %10.9 CUF 473 = % 1.9 AFP 78 = % 0.3 NRA 59 = % 0.2

 
Matokeo ya Uchaguzi Mdogo jimbo la Chalinze yametangazwa Chama cha Mapinduzi CCM kimepata jumla ya kura 20812,na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),kimepata idadi ya jumla kura 2828 na chama cha Wananchi CUF kimepata kura 474.
Hivyo chama cha Mapinduzi CCM kimeshinda Kiti cha Ubunge Jimbo la Chalinze


•••MATOKEO YA JUMLA•••

Talawanda: CCM 1192, CHADEMA 104, CUF 4.

Msoga: CCM 1248, CHADEMA 68, CUF 9

Lugoba: CCM 1594, CHADEMA 174, CUF 4

Kiwangwa: CCM 1180, CHADEMA 80, CUF 14

Kibindu: CCM 1131, CHADEMA 300, CUF 3

Fukayosi: CCM 1105, CHADEMA, CUF 69 17

Mandela: CCM 1394, CHADEMA 112, CUF 8

Mbwewe: CCM 1319, CHADEMA 166, CUF 23
Pera: CCM 1139, CHADEMA 49, CUF 19
  

Matokeo ya awali kwa baadhi ya vituo yanaonesha kuwa mgombea wa CCM Ridhiwani Kikwete ameshinda
Uchaguzi wa mdogo wa Jimbo la Chalinze umefanyika huku ukigubikwa na kasoro kadhaa, ikiwa ni pamoja na watu wachache kujitokeza vituoni kupiga kura, wapiga kura kulalamika ‘kupokwa’ vitambulisho vyao, vituo kuwa majumbani kwa watu, huku pia kukiwa na hofu ya vurugu.
Kasoro hizo zilijidhihirisha jana wakati wapiga kura shughuli ya upigaji kura ilipokuwa ikiendelea katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ambapo wananchi wa Chalinze walikuwa wakipiga kura mbunge wao, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Said Bwanamdogo aliyefariki mapema mwaka huu.



No comments:

Post a Comment