Saturday, May 24, 2014

Mganga amkata mtoto sehemu za siri na kuzibanika

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2325050/highRes/751577/-/maxw/600/-/d2148o/-/kanda.jpg 

Polisi wanamshikilia mganga wa jadi kutoka Kijiji cha Matera, Kata ya Nyanguge, Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza kwa tuhuma za kumnyonga mwanafunzi wa darasa la kwanza, Fausta Geofrey (8) na kukata viungo vyake na kuvibanika ili kupata dawa ya uganga.
Anadaiwa kufanya mauaji hayo Mei 21 katika Kijiji cha Bisole, Kata ya Muhutwe, wilayani Muleba.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumkata mikono yote, masikio, ngozi ya mgongoni na sehemu za siri na kuvibanika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, George Mayunga alisema mwanafunzi huyo akiwa na wenzake wawili saa 1:30 asubuhi alipita karibu na nyumba ya mganga wakielekea shuleni. Mayunga alisema mganga huyo alimwita na kumkaba shingo na mdomo ili asipige kelele kabla ya kumpeleka ndani ya nyumba alikomnyonga.
Baada ya kukata viungo vyake, mtuhumiwa anadaiwa kuchimba shimo chini ya kitanda chake na kuuzika mwili.
“Baada ya kumnyonga alikata mikono yote, masikio, sehemu za siri na sehemu nyingine kwenye mwili na kuanza kuvibanika ili vikauke aweze kutengeneza dawa ya uganga kwa wateja wake,” alisema Mayunga.
Aidha, Mayunga alisema kuwa mganga huyo amekuwapo kijijini hapo kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Alisema wazazi wa mwanafunzi huyo waliingiwa na hofu baada ya kufika saa 10:00 jioni bila kurejea nyumbani.
“Baada ya kumsaka bila mafanikio, waliamua kutoa taarifa kituo cha polisi ili kuomba msaada zaidi,” alisema Kamanda Mayunga.
Katika msako uliofanyika Jumapili Mei 22, polisi na wananchi walimtilia shaka mganga huyo baada ya kumhoji alikiri kufahamu alipo mtoto huyo na kuwaeleza kuwa alikuwa tayari amekufa.
Kamanda Mayunga alisema mganga huyo aliwapeleka hadi nyumbani na kuwaonyesha vifaa alivyotumia kwenye mauaji.
“Alituonyesha vifaa na alipomfukia mtoto huyo pamoja na viungo vilivyokuwa katika hatua ya ukaushwaji.”

Mganga amkata mtoto sehemu za siri na kuzibanika

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2325050/highRes/751577/-/maxw/600/-/d2148o/-/kanda.jpg 

Polisi wanamshikilia mganga wa jadi kutoka Kijiji cha Matera, Kata ya Nyanguge, Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza kwa tuhuma za kumnyonga mwanafunzi wa darasa la kwanza, Fausta Geofrey (8) na kukata viungo vyake na kuvibanika ili kupata dawa ya uganga.
Anadaiwa kufanya mauaji hayo Mei 21 katika Kijiji cha Bisole, Kata ya Muhutwe, wilayani Muleba.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumkata mikono yote, masikio, ngozi ya mgongoni na sehemu za siri na kuvibanika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, George Mayunga alisema mwanafunzi huyo akiwa na wenzake wawili saa 1:30 asubuhi alipita karibu na nyumba ya mganga wakielekea shuleni. Mayunga alisema mganga huyo alimwita na kumkaba shingo na mdomo ili asipige kelele kabla ya kumpeleka ndani ya nyumba alikomnyonga.
Baada ya kukata viungo vyake, mtuhumiwa anadaiwa kuchimba shimo chini ya kitanda chake na kuuzika mwili.
“Baada ya kumnyonga alikata mikono yote, masikio, sehemu za siri na sehemu nyingine kwenye mwili na kuanza kuvibanika ili vikauke aweze kutengeneza dawa ya uganga kwa wateja wake,” alisema Mayunga.
Aidha, Mayunga alisema kuwa mganga huyo amekuwapo kijijini hapo kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Alisema wazazi wa mwanafunzi huyo waliingiwa na hofu baada ya kufika saa 10:00 jioni bila kurejea nyumbani.
“Baada ya kumsaka bila mafanikio, waliamua kutoa taarifa kituo cha polisi ili kuomba msaada zaidi,” alisema Kamanda Mayunga.
Katika msako uliofanyika Jumapili Mei 22, polisi na wananchi walimtilia shaka mganga huyo baada ya kumhoji alikiri kufahamu alipo mtoto huyo na kuwaeleza kuwa alikuwa tayari amekufa.
Kamanda Mayunga alisema mganga huyo aliwapeleka hadi nyumbani na kuwaonyesha vifaa alivyotumia kwenye mauaji.
“Alituonyesha vifaa na alipomfukia mtoto huyo pamoja na viungo vilivyokuwa katika hatua ya ukaushwaji.”

Wednesday, April 9, 2014

JK asitisha Bunge la Katiba

Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta
WAKATI Bunge Maalumu la Katiba likikutana kesho kwa ajili ya kupokea taarifa za kamati na kuanza mjadala wa jumla kwa wajumbe wote, Rais Jakaya Kikwete ameridhia ombi la kulisitisha kuanzia Aprili 28 hadi Agosti mwaka huu, ili kupisha Bunge la Bajeti liendelee na vikao vyake.
Tangu kuanza kwa Bunge hilo Februari 18, mwaka huu, wajumbe wameweza kujadili sura mbili pekee za rasimu ya katiba ambazo hata hivyo uamuzi wake utategemea majadiliano yatayofanyika baada ya kamati zote kuwasilisha taarifa zao kuanzia kesho.
Bunge hili limetumia takribani wiki tatu kujadili kanuni zake, na hivyo kupunguza muda wake wa siku 70 uliowekwa kisheria bila kuanza kujadili sura na ibara za rasimu hiyo.
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta alizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kukutana na viongozi wawili wakuu wa dini, Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama
Sitta alisema kuwa juzi alipokutana na Rais Kikwete alimueleza umuhimu wa kuongeza muda kwa Bunge hilo ambapo alionyesha nia ya kulisogeza hadi Agosti mwaka huu.
Alisema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho za kumalizia kuipitia sura ya kwanza na ya sita ya rasimu inayozungumzia muundo wa serikali ambapo kesho wenyeviti wa kamati 12 za Bunge hilo watawasilisha taarifa zao kwa mtiririko bila majadiliano.
“Wakishawasilisha tunatarajia wiki ijayo wajumbe wote kupata fursa ya kuchangia kwa uwiano, lakini niseme kuwa sina hakika kama kwa muda uliosalia tutakuwa tumemaliza maana sheria namba 83 ya mabadiliko ya katiba inasema ni siku 70 tu, hivyo itakuwa ni aibu rasimu ipitiwe sura mbili pekee kati ya sura 17 zilizopo,” alisema.
Alieleza kuwa baada ya Bunge la Katiba kuahirishwa, litaanza Bunge la Jamhuri kwa ajili ya bajeti hadi Juni, na Julai wataitumia kwa kuwapa wabunge nafasi ya kutembelea majimbo yao ili Agosti Bunge la Katiba liweze kurejea tena kuendelea kupitia sura nyingine.
Sitta alifafanua kuwa baada ya Bunge Maalumu kuhitimisha kazi yao, watakabidhi kwa Rais Kikwete na mwenzake wa Zanzibar rasimu ya katiba inayopendekezwa kwa ajili ya kuiwasilisha kwa wananchi waweze kuipigia kura ya ama kuikubali au kuikataa.
“Unajua licha ya kuwepo purukushani nyingi za hapa na pale nia ya wabunge wengi ni kupata katiba bora na nzuri hivyo mchakato utakamilika tu,” alisema.
Akizungumzia sababu ya kuwatembelea viongozi hao, Sitta alisema kuwa katiba inamgusa kila raia na ndiyo sababu kama mwenyekiti wa Bunge Maalumu aliamua kukutana nao ili kuwafahamisha wametoka wapi, wako wapi na nini kinaendelea.
Sitta aliongeza kuwa kwa kutambua nafasi ya viongozi hao katika jamii hasa kwa kuongoza kundi kubwa la Watanzania, amekutana nao ili kuwasihi na kuelimisha wananchi wengi wanaowaongoza ikiwemo kuliombea Bunge hilo litoke salama.
Sitta atia shaka
Katika hatua nyingine, ziara ya Sitta kwa viongozi wakuu wawili wa dini imeacha maswali mengi ambapo baadhi ya watu wameitafsiri kama kampeni ya Chama Cha Mapinduzi kutafuta uungwaji mkono katika kutetea mfumo wake wa muundo wa serikali mbili.
Hatua hiyo inatokana na msimamo wa viongozi hao wawili kuwa sambamba na ule wa CCM katika suala la muundo wa Muungano ambapo wote wanataka serikali mbili.
Vyanzo vyetu vya ndani vimedokeza kuwa kwa muda mrefu CCM ilikuwa ikitafuta namna ya kupenyeza karata yake ili kupata uungwaji mkono wa Kanisa Katoliki ambalo lina wafuasi wengi nchini.
Hivi karibuni, Kardinali Pengo alilazimika kukutana na vyombo vya habari ili kuweka sawa taarifa iliyokuwa imetolewa na Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu wa kanisa hilo kupitia kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Tabora, Paul Ruzoka akitaka mapendekezo ya wananchi kwenye rasimu kuhusu serikali tatu yaheshimiwe.
Alisema maoni hayo ni yake binafsi wala si msimamo wa kanisa hilo huku akiweka bayana kuwa yeye ni muumini wa serikali mbili, lakini pia akasisitiza kwamba hayo ni maoni yake.

Sunday, April 6, 2014

Matokeo ya Jumla Uchaguzi mdogo jimboni Chalinze- CCM WATISHA!

CCM 20812 = %86.5 CDM 2628 = %10.9 CUF 473 = % 1.9 AFP 78 = % 0.3 NRA 59 = % 0.2

 
Matokeo ya Uchaguzi Mdogo jimbo la Chalinze yametangazwa Chama cha Mapinduzi CCM kimepata jumla ya kura 20812,na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),kimepata idadi ya jumla kura 2828 na chama cha Wananchi CUF kimepata kura 474.
Hivyo chama cha Mapinduzi CCM kimeshinda Kiti cha Ubunge Jimbo la Chalinze


•••MATOKEO YA JUMLA•••

Talawanda: CCM 1192, CHADEMA 104, CUF 4.

Msoga: CCM 1248, CHADEMA 68, CUF 9

Lugoba: CCM 1594, CHADEMA 174, CUF 4

Kiwangwa: CCM 1180, CHADEMA 80, CUF 14

Kibindu: CCM 1131, CHADEMA 300, CUF 3

Fukayosi: CCM 1105, CHADEMA, CUF 69 17

Mandela: CCM 1394, CHADEMA 112, CUF 8

Mbwewe: CCM 1319, CHADEMA 166, CUF 23
Pera: CCM 1139, CHADEMA 49, CUF 19
  

Matokeo ya awali kwa baadhi ya vituo yanaonesha kuwa mgombea wa CCM Ridhiwani Kikwete ameshinda
Uchaguzi wa mdogo wa Jimbo la Chalinze umefanyika huku ukigubikwa na kasoro kadhaa, ikiwa ni pamoja na watu wachache kujitokeza vituoni kupiga kura, wapiga kura kulalamika ‘kupokwa’ vitambulisho vyao, vituo kuwa majumbani kwa watu, huku pia kukiwa na hofu ya vurugu.
Kasoro hizo zilijidhihirisha jana wakati wapiga kura shughuli ya upigaji kura ilipokuwa ikiendelea katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ambapo wananchi wa Chalinze walikuwa wakipiga kura mbunge wao, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Said Bwanamdogo aliyefariki mapema mwaka huu.



Hali ya Michael Shumacher yaimarika

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/04/04/140404122707_michael_schumacher_304x171_getty_nocredit.jpg 
Bingwa wa zamani wa mbio za magari ya langalanga ya F1, Michael Schumacher ameanza kuonyesha hali ya kupata fahamu baada ya miezi kadha ya kuwa katika hali ya kutojitambua.
Wakala wake Sabine Kehm amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari amesema Schumacher "anaendelea vizuri", akisema kwamba wana "uhakika"wa kupona kwake.
Madaktari nchini Ufaransa wanafanya jitihada za kumwondoa katika hali ya kutojitambua, bingwa huyo mara saba wa F1.
Mjerumani huyo mwenye umri wa miaka 45-alipata majeraha makubwa ya kichwa baada ya ajali wakati akiteleza kwenye barafu katika milima ya Alps nchini Ufaransa Desemba 29,2013.
"Tuko pamoja naye katika kipindi hiki kigumu kwake, sisi na timu nzima ya madaktari na wauguzi wa hospitali ya Grenoble," amesema Bi Kehm.

UCHAGUZI CHALINZE KUMEKUCHA

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/04/vituo_1-300x169.jpg 

UCHAGUZI mdogo wa ubunge Chalinze, Bagamoyo, mkoani Pwani unaofanyika leo ambapo jumla ya vituo 288 vya kupigia kura vilivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 vitatumika tena.
Akizungumzia maandalizi ya uchaguzi huo jana, msimamizi wa uchaguzi huo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Samuel Salianga, alisema maandalizi yamekamilika kwa asilimia 95 na vifaa muhimu vimesambazwa kwenye vituo hivyo.
Alivitaja vyama vitano vinavyoshiriki uchaguzi huo kuwa ni CCM, CHADEMA, CUF, NRA na AFP huku akibainisha idadi ya wapiga kura kuwa ni 92,939.
Kwa upande mwingine Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Chalinze kuhakikisha vinawatumia mawakala wanaotoka eneo la vituo ili wawatambue wapiga kura wa eneo hilo.
Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema sheria haikatazi vyama hivyo kuteua mawakala kutoka majimbo mengine ya uchaguzi lakini ni vema kuwateua wale wanaotoka eneo lenye wapiga kura wanaowafahamu.
Licha ya kuwepo kwa idadi hiyo ya waliojiandikisha katika daftari la kupiga kura lakini kuna wasiwasi wa wapiga kura kutofikia idadi hiyo kutokana na miundombinu ya baadhi ya maeneo kuharibiwa na mvua zinazonyesha mkoani hapa.
Kufanyika kwa uchaguzi huo kunatokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wake, Said Bwanamdogo, ambaye alifariki dunia Januari 22, mwaka huu.

UCHAGUZI CHALINZE KUMEKUCHA

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/04/vituo_1-300x169.jpg 

UCHAGUZI mdogo wa ubunge Chalinze, Bagamoyo, mkoani Pwani unaofanyika leo ambapo jumla ya vituo 288 vya kupigia kura vilivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 vitatumika tena.
Akizungumzia maandalizi ya uchaguzi huo jana, msimamizi wa uchaguzi huo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Samuel Salianga, alisema maandalizi yamekamilika kwa asilimia 95 na vifaa muhimu vimesambazwa kwenye vituo hivyo.
Alivitaja vyama vitano vinavyoshiriki uchaguzi huo kuwa ni CCM, CHADEMA, CUF, NRA na AFP huku akibainisha idadi ya wapiga kura kuwa ni 92,939.
Kwa upande mwingine Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Chalinze kuhakikisha vinawatumia mawakala wanaotoka eneo la vituo ili wawatambue wapiga kura wa eneo hilo.
Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema sheria haikatazi vyama hivyo kuteua mawakala kutoka majimbo mengine ya uchaguzi lakini ni vema kuwateua wale wanaotoka eneo lenye wapiga kura wanaowafahamu.
Licha ya kuwepo kwa idadi hiyo ya waliojiandikisha katika daftari la kupiga kura lakini kuna wasiwasi wa wapiga kura kutofikia idadi hiyo kutokana na miundombinu ya baadhi ya maeneo kuharibiwa na mvua zinazonyesha mkoani hapa.
Kufanyika kwa uchaguzi huo kunatokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wake, Said Bwanamdogo, ambaye alifariki dunia Januari 22, mwaka huu.

Saturday, April 5, 2014

PICHA YA RAIS OBAMA YAWATOKEA PUANI SAMSUNG.

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/04/04/140404090825_obama_picha_512x288_bbc_nocredit.jpg 

Ikulu ya Whitehouse imeikashifu kampuni ya simu ya Samsung kwa kutumia picha ya Rais Barack Obama aliyojipiga na mchezaji maarufu nchini Marekani David Ortiz kama tangazo la kibiashara.
Picha hiyo ilipigwa na Ortiz mwenyewe akiwa na Rais Obama akitumia simu yake ya Samsung mapema wiki.
Hata hivyo kampuni ya Samsung iliisambaza kupitia kwa mtandao wa kijami wa Twitter kwa wateja wake na watu milioni 5.2 wanaoifuata kwa Twitter.
Msemaji wa Ikulu ya White House, Jay Carney, alisema kuwa picha ya Rais haipaswi kwa njia yoyote kutumiwa kwa sababu za kujinufaisha kibiashara.
Wakuu wa Samsung hawajasema lolote kuhusu malalamiko ya White House.
Bwana Carney amesema kuwa mawakili wa White House wanashauriwa kuhusu kitendo hicho cha Samsung.
"bila ya kusema mambo mengi, nataka niwaambie tu kwamba White House inapinga vikali jambo hili,'' alisema Carney
Ortiz alimpa Rais Obama Jezzi maalum kutoka kwa klabu anayochezea ya Red Sox ikiwa na jina la Rais siku ya Jumanne na jkisha kumshawishi kujipiga naye picha mwenyewe inayojulikana kama 'Selfie'.
"Nilimpa Jezzi na wapiga picha waka wanatupiga picha, basi nilijhisi na mimi kujipiga naye picha'' alisema mchezaji huyo.
Alikana kuwa kampuni ya Samsung ilimlipa pesa kwa picha hio.

Friday, April 4, 2014

Vikosi vya Marekani vyawasili Uganda kumsaka Kony

http://www.dw.de/image/0,,6478206_10,00.jpg

Kampala. Vikosi vya Marekani kwa ajili ya kumkabili kiongozi wa kundi la Lord Resistance Army (LRA) Joseph Kony vimewasili nchini Uganda huku vikiwa na vifaa vya kisasa zikiwamo ndege zenye uwezo wa kujaza mafuta angani.
Taarifa zimesema kuwa askari hao 150 waliwasili siku tatu zilizopita na kwamba sasa wanatazamiwa kuanzisha msako mkali katika maeneo ya mpakani mwa Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati ambako kiongozi huyo anaaminika kujifisha.
Hivi karibuni Rais Barack Obama aliidhinisha kutumwa kwa vikosi hivyo kama sehemu ya kuunga mkono juhudi zilizoanzishwa na Umoja wa Afrika za kumsaka Kony ambaye pia anatakiwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu(ICC) kutokana na makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Askari hao wamewasili wakiwa na vifaa vya kisasa ikiwamo ndege aina ya CV-200 yenye uwezo wa kujaza mafuta ikiwa angani na kwamba mkakati wao wa kwanza ni kuelekea kwenye misitu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Ofisa habari katika ubalozi wa Marekani nchini Uganda Daniel Travis alithibitisha kuwasili kwa askari hao lakini hata hivyo hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi.
“Hatuwezi kueleza zaidi kuhusiana mahali ambako vikosi hivyo vipo zaidi ya kusema kwamba vitakuwepo nchini kwa muda maalumu na hatutarajia kuona vinakuwepo zaidi ya muda ulioamuliwa,”alisema.
Vikosi hivyo vya Marekani vinatazamiwa kuongeza nguvu juhudi za kumsaka kiongozi huyo ambaye anatuhumiwa pia kwa kuwaandikisha askari watoto na kuhusika katika vitendo vya ubakaji.
Kwa muda mrefu vikosi vya Umoja wa Mataifa vimekuwa vikiendesha msako dhidi ya Kony bila mafanikio yoyote kutokana na kuhamisha mara kwa mara maficho yake. Vikosi hivyo vya Afrika vinaundwa na askari kutoka Uganda, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

CHANZO:MWANANCHI

UZEMBE HATI YA MUUNGANO: SAINI ZA NYERERE,MSEKWA ZACHEZEWA

 
Dodoma. Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amekiri “kuchezewa” kwa saini ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na sehemu ya saini ya aliyekuwa Katibu wa Bunge la Tanganyika, Pius Msekwa zilizopo kwenye hati ya sheria ya kuridhia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Akizungumza na gazeti hili jana, Sitta alisema ni kweli kuna maneno katika hati hiyo ya sheria namba 22 ya 1964, iliyosainiwa na Nyerere na Msekwa, Aprili 25, 1964, yameongezwa. Alisema katika saini ya Nyerere kumeongezwa herufi “us” kwa kompyuta na katika sehemu ya saini ya Msekwa kumeandikwa neno “Msekwa” kwa kompyuta, jambo ambalo ni makosa. Sitta alisema walioongeza maneno hayo ni wafanyakazi wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali baada ya kuona sehemu ya maandishi kwenye saini hizo hayasomeki, lakini walifanya makosa. “Wale vijana walipoona document (nyaraka) haisomeki waliongeza “us” mwisho kwa kompyuta kwenye saini ya Nyerere, ila walifanya makosa maana bora kitu kionekane kufifia hivyo hivyo lakini kibaki na maana yake,” alisema. Hata hivyo, Sitta alisema kwa waliofanya kazi na hayati Baba wa Taifa wanatambua saini iliyopo kwenye hati ya sheria hiyo ipo sawa ukiondoa makosa ya kuwekwa herufi hizo. Kuhusu saini ya Msekwa, alisema pia kulifanyika makosa katika sehemu ya saini hiyo, kuandikwa kwa kompyuta “Msekwa”. “Ni saini ya Msekwa, lakini vijana wa chamber kwa AG waliongeza neno “Msekwa” kwa kompyuta. Ni mtu asiyejua thamani na uhalisia wa saini ni kubaki ilivyo hata kama kwa miaka 100 hata mtu aje kuisoma kwa darubini,” alisema. Hata hivyo, alisema maudhui ya hati ya sheria hiyo, iliyosainiwa rasmi Aprili 25, 1964 ni sahihi kama ambavyo walikubaliana waasisi wa Muungano, Nyerere na Karume. Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema alisema kwamba hafahamu kama ofisi yake inahusika na kuchezewa kwa saini hizo, tofauti na madai ya Sitta. Sheria iliyopitishwa Z’bar Sitta alisema ili kuondoa utata, ameagiza kupatiwa hati ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Abeid Karume (Presidential Decree) aliyotoa kusaini makubaliano kwani wakati huo, hakukuwa na Bunge. “Karume alitumia Baraza la Mapinduzi akatumia amri ya Rais akasaini. Tunatarajia kuipata hiyo, sasa tutakuwa tumepata nyaraka za Bara na Zanzibar,” alisema Sitta.