Thursday, February 9, 2012

AFCON 2012- ZAMBIA YAIDUWAZA AFRIKA , YAITOA GHANA.


Zambia hapo jana wameiduwaza Afrika na Ulimwengu mzima baada ya kuwatoa mabingwa mara nne wa michuano ya mataifa ya Afrika Ghana 'The Black Star' kwa kuwafunga Goli 1-0 katika nusu fainali ya kwanza Uwanja Wa Bata Huko Gabon.

Kwa matokeo hayo Zambia wameingia fainali za michuano hiyo ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1994 walipofungwa na Nigeria Ambapo safari hii wanaenda kuktana na Ivory coast ambao jana wamewatoa mali kwa goli 1-0.

Ghana itabidi wajilaumu wenyewe kwa kupoteza nafasi nyingi ikiwemo ile ya Penati iliyokoswa na Asamoah Gyan, huku nyota huyo na mwenzake john Mensah ambao ndio tegemeo la timu hiyo wakicheza chini ya kiwango.
Mayunga ambaye aliingia kumbadili James Chamanga katika kipindi cha pili alionesha uwezo na uwepo wake uliwapa tabu walinzi wa Ghana.

Ghana walimaliza Mpira huo wakiwa watu 10 baada ya Mchezaji wake Derek b
oateng kupewa kadi nyekundu dakika sita kabla ya dakika 90 kumalizika bada ya kupokea kadi ya pili ya njano kutokana na faulo aliyoicheza.
Zambia wanaingia katika fainali hizo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya miaka 19 iliyopita huko gabon ambapo iliwapoteza wachezaji wake wote 25 baada ya ajali ya ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji hao.

No comments:

Post a Comment