Saturday, February 11, 2012

NI GHANA VS MALI KUTAFUTA MSHINDI WA TATU AFCON.

Malabo-GUINEA YA IKWETA, Kikosi cha Mali

Kikosi cha Ghana

Ghana inaivaa Mali leo hii katika mechi ya kumtafuta mshindi wa tatu wa michuano ya Mataifa ya Afrika bila wachezaji wake wanne tegemeo katika mji mkuu wa Guinea ya Ikweta Malabo.

Kiungo wa kati Derek Boateng ana kadi nyekundu aliyoipata kwenye mechi iliyopita dhidi ya Zambia, beki wake wa kati John Boye anakadi mbili za njano katika mechi mbili zilizopita, wakati Kapteni John Mensah na Kiungo mwingine Emmanuel Badu ni Majeruhi.

Ghana imeingia katika nafasi hiyo baada ya kupoteza mchezo wake dhidi ya Zambia na Mali walipoteza dhidi ya Ivory Coast katika nusu fainali.
Ghana ambao mafanikio yao yalikuwa juu katika miaka ya hivi karibuni kutokana na kutinga kuvunjika moyo baada ya kushindwa kufika Fainali katika michuano ya mwaka huu.


Mali kwa Upande wao wanajipongeza kwa kufikia hatua hiyo bila ya nyota wao wa kipindi kilichopita Fredrik Kanoute, Mamadou Diarra na Mamadou Sissoko, huku wakiegemea kupata faida ya kukosekana kwa wachezaji hao muhimu wa Ghana.
.
Hata hivyo mchezo huo unategemewa kuwa wa ushindani ambapo ghana wana kumbu kumbu ya Kuwafunga Mali magoli 2-0 katika hatua ya makundi.


No comments:

Post a Comment