Sunday, February 12, 2012

LA LIGA:BARCELONA WABANWA NA OSASUNA

Wachezaji wa Barcelona wakiwa na huzuni hapo jana mara baada ya Kupoeza dhidi ya Osasuna.


Hispania,
dejan lekic hapo jana aliisaidia timu yake ya Osasuna kuiangusha moja ya miamba ya soka Nchini Hispania Barcelona kwa jumla ya magoli 3-2.
Osasuna walipata goli lao la kwanza kupitia kwa mchezaji huyo Dejan katika dakika ya sita ya kipindi cha kwanza.Dakika 16 baadae katika dakika ya 22 Osasuna waliongeza goli lao la pili kupitia kwa mchezaji yule yule Dejan na kuwafanya waende mapumziko wakiongoza kwa magoli 2-0.
Baada ya mapumziko kocha wa Barcelona alifanya mabailiko na kumuingiza Kapteni Carles Puyol abaye aliongeza nguvu na kuwafanya Barcelona kupata goli katika dakika ya 6 ya kipindi cha pili kupitia kwa Alexis ssanchez ingawa furaha hiyo haikudumu kwani dakika ya 73 mchezaji Raul Garcia aliiandikia timu yake goli la tatu.
Zikiwa zimebaki dakika chini ya 20 mchezo kumalizika barcelona waliongeza bidii na kufanikiwa kupata goli la pili baada ya Cesc Fabregas kumtumbukizia Mpira Christian Tello ambaye hakufanya ajizi na kufunga goli hilo.

Baada ya goli hilo matokeo yalibaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo na kuwafanya Barcelona wakizidi kuachwa katika msimamo wa ligi hiyo na Mahasimu wa Real Madrid kwa Point saba huku Madrid bado wakiwa na mchezo mkononi.

No comments:

Post a Comment