Saturday, February 11, 2012

ROONEY AIPAISHA MAN UNITED KILELENI.




Wayne Rooney amefunga mara mbili katika ushindi wa magoli 2-1 wa Manchester United dhidi ya Liverpool kwenye Uwanja wa Old Traford na kuisaidia timu yake hiyo kukwea kileleni mwa ligi hiyo.

katika Mechi hiyo ambayo ilishuhudia Manchester United wakitawala sehemu kubwa ya kipindi cha pili Rooney alifunga goli la kwanza katika dakika ya 47 baada ya kona na kuongeza goli la pili katika dakika ya 50 huku goli la liverpool likifungwa na Luis Suarez katika dakika ya 80 .

Katika mechi hiyo pia kulishudiwa muendelezo wa uhasimu kati ya Mchezaji Luis Suarez wa Liverpool na Patrice Evra wa manchester united Baada ya mchezaji huyo wa Liverpool kukataa kupeana mikono.

Kwa matokeo hayo Manchester United Imeshika Usukani wa ligi hiyo ikiwa na pointi 58 mbele ya Manchester City wenye Pointi 57 wakiwa na mchezo mmoja mkononi wakati liverpool wao wanabaki na pointi zao 39 katika nafasi ya 7.

No comments:

Post a Comment