Tuesday, July 31, 2012

KAMPENI ZA URAIS MAREKANI-ROMNEY AWATIBUA WAPALESTINA

Mitt Romney Akiwa Jerusalem.


Marekani,
Mgombea wa urais kupitia chama cha Republican Mitt Romney ametibua tena anga za kimataifa baada ya kutoa matamshi yenye kuwakwaza Wapalestinakatika kampeni zake na ziara zake huko Israel. Mitt Romney ambaye hivi karibuni aliwatibua waingereza kwa kauli yake ya kuwa na wasiwasi kama Uingereza ipo tayari kwa michuano ya Olympic, ametamka kuwa Jerusalem ni mji mkuu wa Israel kitu ambacho hakitambuliwi na Wapalestina na washirika wake.
 Pia Romney amesema katika ushindani wa kiuchumi  kati ya Israel na Palestina ni Israel ndiyo iliyotajiri zaidi kutokana na utamaduni wake ambao ni bora zaidi ya Palestina.
Mpatanishi wa mgogoro wa Israel na Palestina kutoka Palestina Saeb Erekat amesema maneno hayo ya Romney yalikuwa ni ya kibaguzi sana akiyataja kama 'matamshi ya kibaguzi yanayoonesha ukosefu wa maarifa'.

"Kila mmoja anajua Palestina haiwezi kufikia ustawi wake kwa kiwango cha juu chini ya vizuizi vya Israel" Aliongeza Bw.Saeb.

Sunday, July 29, 2012

MGOMO WA WALIMU WATHIBITISHWA -Kuanza kesho .

 

TANZANIA,
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) kimethibitisha kuwepo kwa mgomo wa walimu Tanzania kuanzia

hapo kesho licha ya serikali kutangaza kuwa mgomo huo ni batili.

Rais wa CWT, Gratian Mukoba amesema kuwa Baraza la CWT lilitoa notisi ya saa 48 ambazo zimemalizika leo mchana na hivyo kesho mgomo utakuwepo na walimu watatakiwa kubaki majumbani kwao bila kwenda kazini. Mukoba pia alisisitiza kuwa mgomo huo ni halali kwani wananachama waliopiga kura kuhalalisha  mgomo walikuwa 153,000  ambapo kati ya 183,000   wakiwa sawa na asilimia 95.7 ya wanachama na hivyo kuhalalisha mgomo huo.


Rais huyo alimewataka walimu kutokuwa na hofu na ajira zao kwani mgomo huo umezingatia sheria.
Walimu wameingia katika mgomo huo wakiwa na  madai ya ongezeko la mishahara kwa asilimia 100, posho ya kufundishia kwa walimu wa Sayansi asilimia 55, asilimia 50 pamoja na posho kwa walimu wa masomo ya  sanaa na posho kwa  walimu wanaoishi katika mazingira magumu.

KAMATI YA NISHATI NA MADINI YAVUNJWA-Sababu ni ufisadi.

TANZANIA,
Kamati ya nishati na madini imevunjwa kwa tuhuma za ufisadi ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kitangaza uamuzi huo spika wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna Makinda alisema vitendo kama hivyo havikubaliki hivyo anaivunja kamati hiyo ya nishati na madini na kupeleka pia suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa hatua zaidi ikiwemo uwezekano wa kutajwa kwa wabunge wanaohusika katika sakata hilo.

Hatua hiyo ilifuatia hoja ya Mbunge Vita Kawawa wa jimbo la Namtumbo(CCM) aliyeomba Mwongozo wa Spika, akitaka jambo hili lijadiliwe na Bunge na Kamati za Bunge zinazotuhumiwa kwa rushwa zivunjwe, hoja ambayo iliungwa mkono na spika huyo na kuvunja kamati hiyo.
Habari za fununu kutoka  Dodoma zimeeleza kuwa katika mlolongo huo wapo pia wabunge  wanaotoka katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, na wengine kutoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
Wabunge waliochangia waliomba uchunguzi zaidi ufanyike na hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya watuhumiwa.

MAJESHI YA SYRIA YAWASHAMBULIA WAASI KWA NDEGE.

http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120729&t=2&i=635702901&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=300&r=CBRE86R0GDQ00
Mtoto akiangalia nyumba iliyobomolewa kwa mashambulizi.

http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120729&t=2&i=635702669&w=&fh=&fw=&ll=460&pl=300&r=CBRE86R1M9B00
Askari wa waasi akipita karibu na jengo lililobomolewa na ndege za jeshi la serikali.
SYRIA,
Vikosi vya serikali vimeripotiwa kuwashambulia waasi kwa helikopta za kijeshi na makombora asubuhi ya jumapili ya leo katika mapigano makali ya kugombea udhibiti wa mji wa pili wa Aleppo.Wanaharakati wameripoti mapigano katika baadhi ya Wilaya na vitongoji katika jiji hilo la kibiashara.

Msuluhishi wa mgogoro huo Bw.Koffi Annan na viongozi wengine wamesema hali katika mji wa Aleppo
 inaonesha umuhimu wa kumaliza mgogoro wa Syria.Kiongozi wa Baraza la kitaifa la Syria ambalo ni muunganiko wa vikundi vya upinzani dhidi ya serikali ya Syria Bw.Abdelbasset Sida amezitaka nchi marafiki na washirika wa Syria kuachana na baraza la Ulinzi la Umoja wa mataifa na badala yake waingie wenyewe Syria kuung'oa utawala wa rais Bashar al-Assad.
   
Mapigano nchini Syria yamedumu kwa takribani miezi 16 na kuua maelfu ya watu na hali hivi sasa ni ya vita nchini humo ambapo vikosi vya waasi vinapigana na majeshi ya serikali kuung'oa utawala wa rais  al-Assad.

Saturday, July 28, 2012

UFUNGUZI WA OLYMPIC WAFANA LONDON.


Vijana saba wakiwasha moto wa Olympic.
Add caption

mafataki yakipigwa hapo jana.

Moja ya michezo ya kuigiza
Moja ya washiriki wa Maonesho hayo.






Mr.Bean Naye alikuwepo!
Moja ya Michezo ya kuigiza hapo jana.      
http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120728&t=2&i=635285881&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=390&r=2012-07-28T021058Z_15_GM1E87S0AOR01_RTRRPP_0_OLY-PARK-DAY0
Mishale yenye rangi za bendera ya England ikirushwa juu kupita Uwanja wa Olympic.
http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120728&t=2&i=635285859&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=390&r=2012-07-28T021058Z_15_LM2E87R1HQ028_RTRRPP_0_OLY-OPEN-CEREMONY-DAY0-ACT1
Moja ya mandhari nzuri ya igizo hapo jana kuonesha Uingereza ya karne ya 17 kabla ya mapinduzi ya viwanda.

http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120728&t=2&i=635285911&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=390&r=2012-07-28T021058Z_15_LM2E87R1U5JKW_RTRRPP_0_OLY-OPEN-CEREMONY-DAY0-ACT1
Waigizaji hapo jana.





http://s2.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120728&t=2&i=635285882&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=390&r=2012-07-28T021058Z_15_GF2E87S00F501_RTRRPP_0_OLY-OPEN-CEREMONY-DAY0-ACT3
Mafataki yakipigwa ndani ya uwanja.


http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/photo_item/OLY-OPEN-CEREMONY-DAY0/ACT3/0/2012-07-28T002450Z_1560840710_LM2E87S0153WV_RTRMADP_3_OLY-OPEN-CEREMONY-DAY0-ACT3.JPG
Moto wa Olympic baada ya kuwashwa hapo jana.

Mandhari ya uwanja hapo jana.
http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Michelle+Obama+2012+Olympic+Games+Opening+2R45-1hPstbl.jpg
Michelle Obama akifuatilia sherehe hizo.

LONDON,
Malkia elizabeth akifungua mashindano ya Olympic hapo jana
Ni mafataki, ngoma, mandhari za kuvutia zenye kuonesha historia na tamaduni za Uingereza  na shamrashamra za kila namnaa wakati Michezo ya olympic kwa mwaka 2012 yenye ujumbe 'Hamasisha Kizazi' ilipofunguliwa rasmi hapo Jana.
Vijana saba wa umri wa miaka chini ya ishirini jana waliongoza tukio la kuwasha moto wa Olympic  na kufuatiwa na mafataki makubwa kusherehesha ufunguzi huo.

Tofauti na mashindano mengine uwashaji wa moto wa Olympic mwaka huu umeongozwa na vijana wadogo wasiofahamika badala ya wanamichezo maarufu kama ilivyozoeleka.Mgeni rasmi na mfunguaji wa michezo hiyo alikuwa ni Malkia Elizabeth (86)akiwa na mgeni wake mashuhuri mke wa rais wa Marekani Michelle Obama ."Natangaza ufunguzi rasmi wa michezo ya 30 ya Olympic" Alisikika na kufuatiwa na upigaji wa mafataki na kushangiliwa.

Sherehe hizo zimeashiria mwanzo wa siku 16 za michezo ya olympic ambayo itahusisha wanamichezo zaidi ya 16,000 kutoka nchi 204 duniani kote.




Friday, July 27, 2012

OLYMPIC KUFUNGULIWA LEO-Picha za Maandalizi ya Mwisho.

http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/photo_item/OLYMPICS-BRITAIN/0/2012-05-05T212906Z_922909035_GM1E8560FH101_RTRMADP_3_OLYMPICS-BRITAIN.JPG
Uwanja wa Olympic ukiwa tayari kwa sherehe za ufunguzi.

 Kengele zimelia usiku wa kuamkia leo nchini uingereza kuashiria Siku ya mwisho kabisa kuelekea ufunguzi wa mashindano ya Olympic utakaofanyika leo usiku ndani ya uwanja wa Olympic park katika jiji la London na kuhudhuriwa na watu maarufu wakiwemo Malkia Elizabeth na Michelle Obama mke wa Rais wa Marekani.
http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/photo_item/SPORTS-US-OLY-BLUNDERS-ADV1/2/2012-07-26T201622Z_1_CBRE86P1KBF00_RTROPTP_3_SPORTS-US-OLY-BLUNDERS-ADV1.JPG
Taa ndani ya uwanja zikiwa tayari kwa sherehe hizo.

Sherehe hizo zinatakazokuwa na shamra mbali mbali zikiwemo ulipuaji wa mafataki, muziki, na maonesho mbalimbali ya kimichezo na kitamaduni zinatarajiwa kufana na kuvutia wahudhuriaji zaidi ya 60,000 na watazamaji zaidi ya bilioni 1 dunia nzima.

http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/photo_item/OLYMPICS-OPENING/0/2012-06-12T113443Z_1830676218_LM1E86C0W2F01_RTRMADP_3_OLYMPICS-OPENING.JPG
Muundo wa uwanja wa lympic utakavyokuwa katika sherehe hizo.

http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/photo_item/OLY-AROUNDTOWN-ADV1/0/2012-07-26T205633Z_10312663_GM1E87R0DMU01_RTRMADP_3_OLY-AROUNDTOWN-ADV1.JPG
Jua likipenya kati ya bendera ya nchi zinazoshiriki mashindano hayo katika viwanja vya Bunge la Uingereza.



Mwenge wa olympic leo umemaliza ziara yake kwa kurudi london ambapo ulipitia mto Thames ndani ya majahazi ya kifalme ya Gloriana ambayo yalitumika pia katika sherehe za  Malkia Elizabeth mwezi juni.

http://london-games.reuters.com/london-olympics-2012/files/styles/article_large_landscape/public/user_upload/14541/2/RTR35DVV.jpg
Mkimbiza mwenge Amber Charles akiwa amebeba mwenge kutoka katika jahazi la kifalme chini ya daraja la 'Tower' Lonndon leo hii.

Viwanja vimeonekana kuwa tayari na watu wote wanahamasa jijini London juu ya kuanza kwa michezo hiyo ambayo imeigharimu nchi ya Uingereza zaidi ya trilioni 21 katika maandalizi yake.

            Kila la kheri kwa waingereza na wanamichezo wote wenye ushiriki katika michezo hiyo!

Wednesday, July 25, 2012

MDEE,NASARI WAKANUSHA KUMPIGIA DEBE ZITTO URAIS 2015.

 



Dar Es Salaam- TANZANIA,
Baada ya siku chache kudaiwa na vyombo vya habari kuwa wanamnadi mbunge wa Kigoma kaskazini Mh. Zitto Kabwe kuwania urasi mwaka 2015,Wabunge wawili wa Chadema Mh.Joshua Nasari na Halima Mdee, wamejitokeza na kukanusha taarifa hizo.

Kwa Upande wake Nassari hapo jana ametoa taarifa kwa vyombo mbali mbali vya habari akikanusha taarifa hizo na kudai kuwa ni uzushi na kwa upande wake hajawahi kusimama na kutamka maneno hayo.

Nasari alisema anaamini vitu muhimu ni mizizi au vyanzo vya matatizo yanayowakabili Watanzania kama umaskini, ujinga, maradhi, ufisadi na utawala mbovu wa Chama Cha Mapinduzi CCM na sio yo urais.

“Kama ambavyo chama changu, Watanzania wengine makini na mimi mwenyewe, naamini kuwa kwa sasa suala la muhimu kwetu kama Taifa ni kutafuta mizizi au vyanzo vya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii ya Watanzania,” alinukuliwa Nasari..


Kwa upande wake Mbunge wa Kawe Mh.Halima Mdee naye pia ametoa taarifa ya kukanusha habari hiyo akisema kimevunja misingi ya maadili ya vyombo vya habari kwa Uzushi huo.

“Habari hiyo imeniletea usumbufu mkubwa hasa kwa wananchama wa chama changu cha Chadema ambao wanajua kuwa chama chao makini ni mahiri katika kufuata katiba, kanuni na taratibu katika kuendesha mambo yake kwa manufaa ya watu wote,” alinukuliwa Mdee.
 
Gazeti hilo lilidaiwa kumnukuu Nasari wakati alipofika Kigoma ambapo liloidai alitamka kuwa Zitto anafaa kuwa ndiye rais ajaye wa Tanzania


RAIS ATTA MILLS WA GHANA AFARIKI DUNIA!

 

Hayati Atta Mills.
 



Accra-GHANA,
Rais Atta Miils wa Ghana amefariki dunia ghafla siku ya Jumanne imearifiwa, Rais Mills ambaye alijizolea sifa kubwa barani Afrika na Duniani kwa ujumla kwa kuboresha na kusimamia demokrasi ndani na nje ya mipaka ya nchi yake amearifiwa kufariki ghafla akiwa na umri wa miaka 68.

Rais huyo amefariki siku chache baada ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa hapo jumamosi iliyopita . Sababu za kifo chake  bado hazijawekwa wazi.ingawa mmoja wa ndugu wa karibu ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema rais huyo alikuwa akilalamika kuwa anajisikia maumivu tangu siku ya Jumatatu jioni na kufika siku ya jumanne mauti yalimfika.

Msemaji wa ofisi ya rais alitangaza kifo hicho, ambapokwa kufuata katiba ya nchi hiyo, makamu wa rais wa nchi hiyo bw. John Dramani Mahama (53) aliapishwa kuwa rais wa muda,saa chache baada ya kutangazwa kwa kifo hicho.

Rais huyo amefariki miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo ambapo alitarajiwa kutetea kiti chake hicho mnamo mwezi Desemba mwaka huu.Atakumbukwa kwa kusimamia demokrasi ya kweli katika taifa hilo kinara wa kuzalisha dhahabu Afrika na mzalishaji namba mbili wa Cocoa duniani.

Sunday, July 22, 2012

MAREKANI KUZIPATIA KENYA ,BURUNDI, UGANDA NA DJIBOUT SILAHA DHIDI YA ALSHABAB

Washington D.C -Marekani,

Marekani itaipatia Kenya, Uganda na Djibout vifaa vya kijeshi vya kisasa ili kuwasaidia kupambana na wanamgambo wa Al-shabab imearifiwa.

Kwa mujibu wa gazeti la Wall Street la Marekani katika habari yake hapo juzi tarehe 20,Kenya watapatiwa ndege zinazoruka bila rubani zipatazo nane na vifaa vingine vya kijeshi ikiwemo magari yenye silaha.

Nchi nyingine zilizobaki ambazo ni Uganda,Burundi na Djibout zitapatiwa vifaa vya kijeshi pia kuzisaidia kukabiliana na waasi hao.

RAIS MPYA WA INDIA ATANGAZWA-ni Pranab Mukherjee




INDIA,
 Aliyewahikuwa waziri wa fedha wa zamani wa India Bw.Pranab Mukherjee amechaguliwa kuwa rais mpya wa nchi hiyo kwa kushinda zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa na mabunge ya nchi hiyo. Kwa kawaida uchaguzi wa rais nchini India hufanywa na mabunge mawili na rais huwa hana madaraka makubwa kama ilivyo kwa nchi za kijamhuri kama Tanzania.

Mukherjee, 76, mfuasi wa chama cha Congress alikuwa akitumainiwa kushinda kiti hicho kutokana na kukubaliwa na watu wengi wakiwemo wale wa kutoka vyama pinzani tofauti na mpinzani wake Bw.Pumo A. Sangma (64) aliyewahi kuwa spika wa bunge la nchi hiyo anayetoka katika chama cha Bharatiya Janata Party.

 Licha ya kile kilichoonekana imani katika matamshi yake ya mwezi uliopita kuwa nafasi hiyo inatakiwa kutolewa tu na sio kufikiriwa au kuhangaikiwa Bw. Mukherjee amefanya juhudi za ziada kupata nafasi hiyo hasa alipokuwa akitaka uungwaji mkono na wa vyama vya upinzani vyenye mlengo wa kushoto.

Rais wa India huchaguliwa na wabunge 4'896 kutoka majimbo mbali mbali nchini humo na ushindi huo wa Mukherjee utaongeza nguvu ya serikali bungeni, wakati ambao inalaumiwa kwa ukuaji mdogo wa uchumi na tuhuma mbali mbali za utumiaji mbov wa ofisi za umma.

HERI YA MWEZI MTUKUFU!


MWEZI WA RAMADHAN NI MWEZI WENYE KULETA BARAKA KWA KILA MUAMINI, ANGA ZA KIMATAIFA TUNAWAOMBEA KILA LA KHERI WAISLAMU WOTE NA WOTE WENYE NIA NJEMA NA DINI YA KIISLAMU KILA LAKHERI NA BARAKA KATIKA MFUNGO HUU MTUKUFU WA RAMADHAN!!

Saturday, July 21, 2012

MWENGE WA OLYMPIC WAWASILI LONDON.

Ndege iliyobeba Mwenge wa Olympic ikiwasili mjini London Hapo Jana (REUTERS)

 LONDON-UINGEREZA,
Mwenge wa Olympic Umewasili mjini London jana  kuanza ziara yake ya mwisho  kabisa katika mji wa  ikiwa imebaki wiki moja kabla ya michezo ya Olympic kuanza.

 Mwenge huo uliwasili kwa kutumia Helkopta maalum ya kijeshi na kushushwa na Kamanda wa kikosi cha Maji ambaye alishuka kutoka juu ya Helkopta kwa kutumia kamba maalum na kutua katika mnara wa London ambao ni moja ya vivutio maarufu vya utalii Jijini humo.

http://l3.yimg.com/bt/api/res/1.2/KpMpumtXf1pwZXNwjsA0bg--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Zmk9aW5zZXQ7aD00MDY7cT04NTt3PTYzMA--/http://media.zenfs.com/en_us/News/ap_webfeeds/58637e46559eeb14150f6a706700222e.jpg
Kamanda wa kijeshi akishuka na Mwenge wa Olympic(REUTERS)
Baada ya hapo mwenge huo unatarajiwa kutembelea maeneo muhimu ya kidini,kisiasa na kifalme katika jiji hilo. Michezo ya Olympic inaanza rasmi tarehe 27 julai mpaka Agosti 12 2012, ambapo kwa sasa imebaki takribani chini ya wiki moja tu kuanza kwa michezo hiyo. Maafisa wa Uingereza wanaamini michezo hiyo itakuwa na mafanikio licha ya matishio kadhaa likiwemo la mvua na migomo kwa wafanyakazi hasa wa vyombo vya usafiri.

 

Friday, July 20, 2012

UAMSHO WAWASHA MOTO TENA ZANZIBAR.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMVUmcyjHgQG6W8IkkXGexb-9XI9atyPTKXR2V27F0mXq0hWVcXSrrgZMu31sl5OH36qFvKWR64ZrdAwi6ZeIrr-BKVlMTKz7zPwYUgp4Uv2d02KOzZph5L0F8hobLDPiwQCL86UZkDbg/s1600/znz.jpg
Unguja-Zanzibar,

Kumeripotiwa vurugu tena mjini unguja Zanzibar baada ya kundi la Uamsho kudaiwa kuandaa swala maalum kuwaombea marehemu wa ajali ya Meli ya kuingia mtaani wakiupinga muungano na kuituhumu Serikali ya Muungano kwa kutokushiriki kikamilifu katika zoezi la uokoaji.

Mashuhuda wamesema kundi hilo liliingia mtaani na baada ya hapo askari wameingilia maandamano hayo na kuyatawanya ambapo habari kutoka katika vyanzo visivyonauhakika imedaiwa mabomu na risasi za moto zinatumika mpaka sasa.
Habari za kina na uhakika zitaendelea kukujia hapa anga za kimataifa.

WATU 12 WAUAWA KWA RISASI KATIKA UKUMBI WA SINEMA MAREKANI

http://l.yimg.com/bt/api/res/1.2/znL0A21JQtRoQoGuGkbIXA--/YXBwaWQ9eW5ld3M7Y2g9NDA3O2NyPTE7Y3c9NjMwO2R4PTA7ZHk9MDtmaT11bGNyb3A7aD00MDc7cT04NTt3PTYzMA--/http://l.yimg.com/os/152/2012/07/20/colorad-jpg_141900.jpg
Baadhi ya ndugu na Jamaa wa Marehemu na Majeruhi katika eneo la tukio

 Denver,Colorado MAREKANI,
Kijana wa Umri mwenye umri wa miaka 24 aliyetambulika kwa jina la James holmes  akivalia kificha uso amewashambulia na kuwauwa kwa risasi watu 12 na kujeruhi wengine zaidi ya 50 katika ukumbi wa sinema wa Century Aurora 16 r katika kitongoji cha Denver-Colorado huko Marekani usiku wa kuamkia Ijumaa ya leo. 

Watu hao walikuwa katika ukumbi huo wa sinema wakiangalia filamu mpya ya Batman inayofahamika kama  "The Dark Knight Rises" .Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa muuaji aliingia ndani ya ukumbi na kutupa mabomu ya machozi na kisha kuanza kurusha risasi akiwalenga watazamaji.

Polisi mjini Colorado wamemkamata mtuhumiwa huyo ambaye ametambulika kwa jina la James Holmes ambaye aliwapigia polisi na kuwaambia kuwa alikuwa na vitu vyenye milipuko huko nyumbani kwao.

  
 Watu kumi na mbili wameripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya hamsini wamejeruhiwa katika tukio hilo.
Rais Obama ametoa salaam za rambi rambi kwa familia za ndugu na jamaa wa familia zilizokumbwa na janga hilo na kuwataka wawe pamoja kama familia moja ya Kimarekani.Rais obama pia amesema atafanya kila awezalo kuhakikisha muuaji anafikishwa katika vyombo vya dola.

Thursday, July 19, 2012

RUSSIA NA CHINA WAKWAMISHA ADHIMIO LA UN DHIDI YA SYRIA KWA VETO.

Russia na China wamepiga kura za Veto leo hii  katika baraza la usalama la Umoja wa mataifa kupinga hatua kali dhidi ya Syria na kukwamisha juhudi za kumaliza vurugu nchini humo.kura hizo zimekwamisha juhudi ya nchi za Mashariki za kutaka hatua kali dhidi ya Syria.
 Hiyo ni mara ya tatu kwa nchi hizo kupiga kura hizo ambapo nchi hizo mbili zimekuwa zikipinga hatua kali dhidi ya serikali ya Syria ambayo imekuwa chanzo cha vurugu na mauaji ya maelfu yaliyodumu kwa miezi 16.

Katika kura hizo ambazo azimio lake lingeongeza muda wa waangalizi wa umoja wa kimataifa nchini Syria nchi 11 zililiunga mkono, nchi mbili hazikupiga kura ambazo ni Afrika kusini na Pakistan, na nchi mbili zililipinga ambazo ni china na Russia.

Akiongea kwa masikitiko msimamizi wa umoja wa mataifa katika suluhu ya Umoja wa mataifa Bw. Koffi Annan amesema baraza limeshindwa kuchukua maazuzi imara na muhimu aliyoyategemea katika kumaliza vurugu na mauaji nchini Syria.

Waasi wazidi kusogea karibu na ngome ya serikali:
Wakati juhudi za kidiplomasia zikishindikana  wassi wamezidi kusogea katika ngome ya serikali baada ya hapo jana juzi kuwauwa viongozi muhimu katika serikali ya Syria.

Wednesday, July 18, 2012

HAPPY BIRTHDAY MANDELA!!

http://greencelebrity.info/wp-content/uploads/2012/04/who-is-nelson-mandela-photo-credit-todays-nigeria.jpg

Happy Birthday Mandela!! ndivyo waafrika na wapenda usawa duniani kote tunavyokutakia heri katika siku yako ya kuzaliwa baba wa bara la Afrika mpendwa Nelson Mandela leo unapotimiza miaka 94 tangu ulipozaliwa.

Mchango wako katika kuikomboa Afrika kusini na Afrika nzima kutoka katika mikono ya unyonyaji zitatambuliwa daima! Mungu aendelee kukujalia afya njema Mpendwa Wetu Mandela!

ANGA ZA KIMATAIFA!

MELI NYINGINE YAZAMA TANZANIA

Meli ya SKAGIT iliyokuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar ikiwa  imewabeba watu wapatao miambili imearifiwa kuzama katika bahari ya hindi eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar.

kwa mujibu wa taarifa za vikosi vya wanamaji , meli hilyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.Jeshi hilo la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu hao.
 
Polisi nchini Tanzania wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo,ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo.

WAZIRI WA ULINZI WA SYRIA AUAWA KATIKA MLIPUKO.

Waziri wa Syria aliyeuawa Bw.Daoud Rajha


DAMASCUS-SYRIA,
Waziri wa ulinzi wa Syria na Bw.Daoud Rajha na naibu wake Bw.Assef Shawkat, wameuawa katika mlipuko wa bomu baada ya mlinzi kujitoa mhanga huko Damascus. 

Kwa mujibu wa Televisheni ya Syria waziri huyo wa ulinzi na naibu wake ambaye pia ni shemeji wa Rais Assad wameuawa wakati wakihudhuria mkutano wa mawaziri na wanausalama.Vyanzo vya usalama vya Syria vimesema mlinzi huyo ni wa ngazi ya juu katika nafasi ya ulinzi.


Katika mlipuko huo waziri wa mambo ya ndani bw. Mohammad Ibrahim al-Shaar pamoja na maafisa kadhaa wamejeruhiwa pia, ingawa vyanzo vya habari vimesema rais Assad hakuwepo katika mkutano huo.




Mlipuko huo umekuja wakati mapigano katika mji mkuu wa Syria yakiingia siku ya nne kati ya majeshi ya serikali na waasi wanaowania kuuangusha utawala wa miongo minne(4) wa Rais Assad.
Vifo hicho vimeelezewa kuwa pigo kubwa kwa Rais Assad na serikali yake inayopigana kufa na kupona kubaki madarakani licha ya mashinikizo ya kimataifa kumtaka rais huyo kuachia ngazi