Monday, August 13, 2012

RAIS WA MISRI AWAONDOA MADARAKANI VIONGOZI WA KIJESHI.



CAIRO-MISRI,
Rais Mohammed Morsi amewaondoa madarakani mkuu wa jeshi na waziri wa ulinzi nchini humo bw.Hussein Tantawi na General Sami Anan pamoja na baadhi ya maafisa wa jeshi na kubatilisha agizo la katiba lililokuwa linalipa jeshi madaraka makubwa. Katika taarifa ya rais huyo iliyosomwa na msemaji wa Bw.Yasser Alli nafasi ya bw.Tantawi imechukuliwa na Abdul-Fatah al-Sessi huku ile ya ukuu wa jeshi ikichukuliwa na Sidki Sayed Ahmed. Waziri huyo na mkuu wa jeshi wote wamepewa madaraka mapya kama washauri wa rais.

Katika mabadiliko mengine jaji mkuu wa nchi hiyo bw. Mahmoud Mekki, ameteuliwa kuwa makamu mpya wa rais.Uteuzi huo umeanza mara moja.

Katika taarifa yake rais huyo ametetea uamuzi wake wa hatua hizo na kusema amelenga uzalendo zaidi na umelenga kukipa nafasi kizazi kipya.

Uamuzi huo umeungwa mkono na kufurahiwa na wananchi wa Misri ambao wamekusanyika kwa maelfu katika viunga vya Tahrir Square leo hii na kuimba wakimsifu rais Morsi.

Uamuzi huo umeelezewa kuwa ni wa muhimu hasa kwa wakati huu ambao shinikizo kubwa lilikuwa ni nkurejesha utawala wa kidemokrasia nchini humo na kuruhusu hali ya kawaida baada ya kuwepo udhibiti mkubwa wa jeshi katika madaraka.






No comments:

Post a Comment