Monday, August 6, 2012

WAZIRI MKUU WA SYRIA AJIUNGA NA UPINZANI

http://www.aljazeera.com/mritems/Images/2012/8/6//201286101153313734_20.jpg
Waziri mkuu aliyejiuzuru Bw.Hijab alipokuwa akiapishwa na Rais Al-Assad.

DAMASCUS-SYRIA
Waziri mkuu wa Syria Bw.Riad Farid Hijab, amejiunga na upinzani baada ya kutangazwa kufukuzwa wadhifa wake huo leo asubuhi.Waziri huyo mkuu ameripotiwa kuwasili Jordan leo na kutangaza kujiunga na upinzani,
"Natangaza kuanzia leo kuondoka katika mkondo wa kigaidi na mauaji na kuanzia leo mimi ni mwanajeshi niliyebarikiwa na ninajiunga na kundi la wanamapinduzi na wapigania uhuru" alinukuliwa Hijab katika taarifa yake iliyosomwa na msemaji wake Muhammad el-Etri.
 .
Etri alikanusha pia kuwa waziri mkuu huyo amefukuzwa akisema kuwa serikali imetoa tangazo la kumfukuza baada ya kutambua ameshaondoka nchini Syria.Etri amesema pia kuwa Hijab alikuwa na mpango huo na alikuwa akiwasiliana na jeshi la waasi la Free Syrian Army.

Katika taarifa yake hiyo waziri mkuu huyo mstaafu amewataka viongozi wengine wa Syria kuondoka na kuachana na serikali ya Bw.Al-Assad.
Bila shaka hilo litakuwa ni pigo kubwa kwa Rais Al-Assad ambaye mwezi uliopita aliwapoteza mawaziri wawili katika shambulio la bomu nchini humo.

No comments:

Post a Comment