Saturday, August 25, 2012

MLIPUKO WA KIWANDA WAUA 24 VENEZUELA.

Mlipuko katika kiwanda cha mafuta venezuela (Picha na Reuters)

FALCON-VENEZUELA
Watu wapatao 24 wamefariki akiwamo mtoto mdogo wa miaka 10 na wengine zaidi ya 54 kujeruhiwa baada ya kiwanda cha kusafisha mafuta cha Amuay kulipuka nchini Venezuela.Chanzo cha moto huo kimeripotiwa kuwa ni kuvuja kwa gesi ambayo baadae iliwaka na kulipua matangi mawili ya kuhifadhia mafuta katika kiwanda hicho.
Taarifa zinasema mlipuko ulifuatiwa na motomkubwa ambavyo kwa pamoja viliharibu vibaya nyumba zilizokuwa jirani na eneo hilo.

Kiwanda hicho ni moja ya viwanda vikubwa vya kusafisha mafuta duniani ambapo kinatoa hadi mapipa 645,000 kwa siku. Moto katika eneo hilo umedhibitiwa ingawa shughuli zote za uzalishaji zimesimama huku askari wakilinda eneo hilo.


No comments:

Post a Comment