Friday, August 24, 2012

WANAMGODI WALIOUAWA AFRIKA KUSINI WAOMBEWA.

http://gdb.voanews.eu/D6665CE2-085E-4BB6-B650-D6E5CE826744_mw800_s.jpgJOHANNESBURG- AFRIKA KUSINI
  Maelfu ya ndugu,jamaa na marafiki wa marehemu waliofariki wiki iliyopita katika mapambano kati ya wachimba mgodi wa Marikana na polisi walikusanyika hapo jana katika ibada ya pamoja kuwaombea marehemu hao. Ibada hiyo imefanyika katika eneo yalipotokea mauaji hayo huko Marikana ambalo limepewa jina la "Uwanja wa mauaji wa Afrika Kusini" na wanamgodi hao.

Viongozi wa kidini na kijadi ndiyo walioongoza ibada hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa serikali na vyama vya wafanyakazi.Moja wa viongozi wa kidini alikuwa ni Daniel Modisenyane  aliwaambia waliohudhuria kuwa jamii itajitahidi kupambana na hasara hiyo.
" Siyo rahisi kwa wafiwa kusahau kwa kuwa limekuwa tukio la kuumiza na hatujui hata tutawatuliza vipi" Alisema Modisenyane.

Viongozi wengine waliilaumus serikali kwa kuhusika na mauaji hayo na kuitaka kuchukua hatua kali kwa waliohusika.
Misa hizo zilifanyika pia katika sehemu mbalimbali nchi nzima.

No comments:

Post a Comment