Tuesday, August 21, 2012

WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA AFARIKI DUNIA

 



ADDIS ABABA-ETHIOPIA
 Waziri mkuu wa Ethiopia Bw.Meles Zenawi, 57 amefariki dunia huku Brussels Ubelgiji usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu. Taarifa za kifo cha waziri mkuu huyo zimetangazwa na msemaji wake Bw.
 Bereket Simon amesema waziri huyo alifariki katikati ya usiku baada ya kukimbizwa chumba cha wagonjwa mahututi.Kifo cha waziri mkuu huyo kilizushwa kwa muda mrefu na hali ikawa ya wasiwasi zaidi baada ya kushindwa kuhudhuria mkutano wa wakuu wa Africa mwezi uliopita.

Makamu waziri mkuu wa Ethiopia Bw. Hailemariam Desalegn ataapishwa punde kushika wadhifa huo mpaka chama tawala kitakapomchagua mrithi wa Bw,Zenawi kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo.

 Umoja wa Afrika umetuma salamu zake za rambi rambi kwa Ethiopia na kuelezea kifo hicho kama pigo kubwa kwa Afrika iliyompoteza mtoto Mahiri na hodari.

Uingereza pia kupitia kwa waziri Mkuu Bw.David Cameron imeelezwa kuguswa na msiba huo ikimtaja Waziri huyo kama mmoja ya Wazungumzaji wenye ushawishi barani Afrika.
Meles aliingia madarakani mwaka 1991 akimbadili Haile Mariam aliyekuwa kiongozi wa kijeshi na alisifiwa na wengi kwa juhudi zake zilizosaidia kukua haraka kwa uchumi wa nchi hiyo masikini.

Licha ya kulaumiwa na makundi ya haki za binadamu nchini humo kwa wakati fulani, waziri huyo atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwa jirani zake Somalia hasa katika mapambano dhidi ya
waasi pamoja na makundi yanayoshirikiana na Al Qaeda hali iliyomfanya rafiki mkubwa pia wa nchi za Magharibi. 
Hata hivyo haijawekwa wazi wapi na siku gani waziri huyo atazikwa.

No comments:

Post a Comment