Saturday, August 18, 2012

KUNDI LILILOMSHAMBULIA OBAMA LINA UHUSIANO NA REPUBLICAN.

http://a.abcnews.go.com/images/Politics/abc_obl_raid_120815_704x396.jpg
Ben Smith mmoja wa wanakikundi cha OPSEC Education Fund
WASHINGTON DC-MAREKANI,
Kundi la waliowahi kuwa majasusi na makomandoo  katika jeshi la Marekani pamoja na baadhi ya raia wa kawaida waliotoa tangazo lenye kumshambulia rais Obama kuhusu rekodi yake katika mambo ya usalama limebainika kuwa na uhusiano na chama cha Republican.

 Kwa mujibu wa kumbu kumbu zilizokusanywa na ofisi za umma pamoja na wavuti mbalimbali zimeonesha uhusiano kati ya wahusika wakuu katika kundi hilo lililojitambulisha kama OPSEC Education Fund na viongozi wa vitongoji na wa kitaifa kutoka katika chama cha Republican, ambapo katika orodha hiyo wapo wapo mhasibu,mwanasheria na kampuni ya video ya  kundi hilo.


Braden, mshauri wa mambo ya kisheria wa kundi hilo la OPSEC amekiri katika mahojiano kuwa alishawahi mshauri mkuu wa kamati ya taifa ya chama cha Republican mnamo miaka ya 1980 kamati ambayo ndiyo chombo kikuu cha chama ch Republican.Licha ya kuachana na nafasi hiyo Braden amekiri kuendelea kukishauri chama cha Republican katika shughuli mbalimbali za kisiasa, ingawa pia amesema huwa anajishughulisha na wateja wengine wa kawaida katika kazi yake kama mshauri wa kisheria.

Michael Smith,huyu ni mhasibu wa kundi hilo la OPSEC ambaye amethibitika kuwahi kuwa mshauri wa Republican pamoja na rais wa kundi lililokuwa linakiunga mkono chama cha Republican mwaka 2008 kilichotambulika kwa jina la Majority America.

Greener and Hook kampuni iliyotengeneza kipande cha video hiyo, hii ni kampuni ambayo inajitambulisha katika tovuti yake kama kampuni inayohusika na utengenezaji wa vipindi mbalimbali vya televisheni ambapo imeonesha kipande cha video iliyohusika na tuhuma hizo kwa rais Obama ikijitambulisha kama mtengenezaji mkuu.Kampuni hiyo imethibitika pia kuwa na uhusiano na Republican ambapo katika orodha ya wateja wake wakuu imewataja Kamati kuu ya kitaifa ya Republican, Umoja wa mameya wa Republican, Kamati ya mikataba ya Republican, na umoja wa wanawake wa republican.

Huo ni baadhi ya ushaidi uliotolewa katika tovuti mbalimbali na takwimu za ofisi za umma ukichapishwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Marekani kuonesha uhusiano wa wahusika wake na chama cha republican huku ushahidi mwingine ukiwa ni jengo la ofisi linalotumiwa na kudni hilo ambapo limekodiwa kutoka kutoka kwa kampuni ya The Trailblazer Group ambayo ni mshirika wa Republican ingawa kampuni hiyo imekanusha kuwa na uhusiano na kudni hilo zaidi ya upangishanaji wa jengo hilo. Pia mkanganyiko unaopatikana katika maelezo ya kundi hilo ambalo msemaji wake mkuu Bw.Chad Kolton alisema halipo kisiasa na wahusika wake hawajihusishi na siasa maelezo ambayo ni kinyume na ukweli kwani baadhi yao wameonekana kuwa walishiriki katika shughuli za kisiasa mnamo mwaka 2008 akiwemo Bw. Gabriel Gomez.

Kwa upande wa Democrats hawajajibu tuhuma hizo ingawa tayari walishatoa tuhuma kwa Republican kuhusika na kampeni hiyo ya kuwashambulia.Maafisa wa serikali ya Marekani wamesema suala hilo lilishughulikiwa kikamilifu na wahusika walichukuliwa hatua kali huku waandishi wa habari walioandika kuhusu habari za kijasusi kuhusu tukio la ukamatwaji wa Osama bin Laden wakikataa kupata habari hizo kutoka vyanzo vya Ikulu ya Marekani

No comments:

Post a Comment