Tuesday, August 7, 2012

WATU 16 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO DHIDI YA KANISA NIGERIA



Otite-NIGERIA, 
Watu wenye silaha wamewaua watu zaidi ya 16 kwa kuwapiga risasi katika kanisa katika mji wa Otite karibu na jiji la Okene nchini Nigeria imeripotiwa.Kamanda wa jeshi la Nigeria Bw.Gabriel Olorunyom ameviambia vyombo vya habari kuwa watu hao walivamia kanisa hilo wakati waumini hao walipokuwa katika ibada na kuwafyatulia risasi ambapo Mchungaji wa kanisa hilo ni moja ya waliouawa.






Kamanda huyo amesema watu wengine wengi wamejeruhiwa ingawa haiikuwa rahisi kutaja idadi yake kwa kuwa wamelazwa katika hospitali mbalimbali na wengine wanadhaniwa kukimbia na kujificha.

Tukio hilo limetokea saa 24 baada ya watu 17 kukamatwa na vifaa 34 vya milipuko na mpaka sasa hakuna kundi lililotangaza kuhusika na tukio hilo ingawa hisia kubwa ni kwa kundi la Boko Haram ambalo limekuwa likipinga elimu na dini za kimagharibi nchini humo.



No comments:

Post a Comment