Thursday, August 9, 2012

ALIYEWAHI KUWA BALOZI WA TANZANIA ITALIA AACHIWA HURU.

DAR ES SALAAM-TANZANIA,
Aliyewahikuwa balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, ameshinda kesi iliyokuwa inamkabili  baada ya upande wa mashitaka kuonekana hauna ushahidi wa kujitosheleza.
Prof.mahalu ambaye alikuwa akishitakiwa na serikali kwa kuisababishia hasara ya  Euro 2,065,827.60,  kwa manunuzi ya majengo ya Balozi nchini Italia kinyume cha sheria.
.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgyPE6dhkIt_DRo2Ai3FKHDA4b37cUMxsqzg4emAjpQ6TuJ9NUOZENsMCcJl744UpZf_gH6lsXoV1a35GiPE9Qjw2wcyCn_eCTvbA3q5DDWpZNXgOMcMW5JpdOulM6Kzn9aYTzn1VGXJmCL/s1600/DSC_0139.JPG
Akisoma hukumu hiyo leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Hakimu Ilvine Mugeta, amesema Profesa Mahalu  na  aliyekuwa Mkuu wa Fedha na Utawala katika ubalozi huo, Bi.Grace Martin, hawajapatikana na hatia kwa kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haujajitosheleza na kulingana na hivyo kuwa si wa kweli.
Kwa kigezo hicho hakimu huyo amewaachia huru washitakiwa hao kwa kuwa hawana kesi ya kujibu.

No comments:

Post a Comment