Monday, August 6, 2012

USAIN BOLT ASHINDA TENA MEDALI YA DHAHABU.

http://www.abc.net.au/news/image/4178898-3x2-700x467.jpgLONDON-UINGEREZA,
Usain Bolt mwanariadha mwenye kasi zaidi duniani ameonesha umahiri wake baada ya hapo jana kunyakua medali ya dhahabu akishika nafasi ya kwanza katika mbio za mita 100 wanaume, huku akiweka rekodi mpya ya kukimbia mita 100 kwa sekunde 9.63.
 Nafasi ya pili ilienda kwa mjamaika mwenzake Yohan Blake na ya tatu  ikachukuliwa na bingwa wa mbio hizo mwaka 2004 Justin Gatlinwa Marekani.
http://jahkno.com/wp-content/uploads/2012/08/Usain-Bolt-The-Legend-Wins-100m-London-2012-Olympic-111.jpg
 Ushindi huo wa Bolt umedhihirisha ubora wake na utawala katika riadha na kuwaondoa hofu mashabiki wake ambao walihofu angeshindwa kutokana na kuripotiwa kuwa na majeraha ya mkono.Wajamaika ambao hapo jana walikuwa pia wakisheherekea uhuru wa nchi yao wameupokea kwa shangwe ushindi huo.
Bolt sasa atalingana na mwanamichezo Carl Lewis wa Marekani ambaye naye amewahi kupata medali 2 za dhahabu katika mbio hizo za mita 100.


Wajamaica wakishangilia Ushindi huo katika jiji la kingstone -Jamaica.

"Baada ya nusu fainali nilipata ujasiri na kujiamini kwani miguu yangu ilikuwa vizuri na hicho kiliniongezea kujiamini" alisema Bolt baada ya ushindi huo.

No comments:

Post a Comment