Tuesday, August 21, 2012

MGODI ULIOUA AFRIKA KUSINI WAHAIRISHA TISHIO LA KUWAFUKUZA KAZI WAFANYAKAZI WALIOGOMA.

 http://www.globalpost.com/sites/default/files/imagecache/gp3_slideshow_large/south_africa_lonmin_marikana_miners_fired_20120820.jpg
 MARIKANA-AFRIKA KUSINI,
Uamuzi wa kuwafukuza wafanyakazi waliogoma  kushinikiza kuongezwa kwa mishahara na kupinga mauaji ya wenzao katika mgodi wa Marikana nchini Afrika kusini umegonga mwamba baada ya kampuni ya Lonmin inayomiliki mgodi  kuondoa tishio hilo.Akitangaza uamuzi huo makamu rais wa kampuni hiyo Bw.Mark Munroe amesema kuwafukuza maelfu ya wafanyakazi hakutasaidia kitu na hivyo kampuni yao imeamua kuondoa tishio hilo.

Ni asilimia 33 tu ya wafanyakazi 28,000 waliokuwa wameripoti kazini mpaka leo Jumanne ambayo ndiyo ilikuwa siku ya mwisho waliopewa na mgodi huo kurudi kazini, huku asilimia 67 ya wafanyakazi wakiwa bado wamegoma hali iliyoulazimu mgodi huo kusalimu amri.
Wafanyakazi hao wapo katika mgomo kushinikiza kuongezwa kwa mishahara yao na pia wakiwa katika maombolezo ya vifo vya wenzao 34 waliopigwa risasi katika mapambano na polisi wiki iliyopita.

Serikali ya Afrika kusini imeutaka mgodi huo kuachana na uamuzi huo na kusubiri kutafutwa kwa suluhu nyingine ambayo itakuwa na msaada kwa tatizo hilo.
  Wakati huo huo Bunge la Afrika kusini ambalo litakaa siku chache zijazo pamoja na mabo mengine litajadili suala hilo na kulitolea uamuzi, viongozi wa kisiasa wakiwemo wabunge na viongozi wa vyama vya siasa wameutembelea mgodi huo kujionea hali halisi ikiwa ni maandalizi ya mjadala unaotarajiwa kuwa mkali kuhusu tukio hilo.

No comments:

Post a Comment