Saturday, July 27, 2013

Polisi kwa kumwambukiza mtoto VVU


 
“Sasa nikawa najiona ninaanza kutokwa na vipele sehemu ya mbele na nyuma vinawasha sana na nimejikuna na sasa vimekuwa vidonda na vinatoa  harufu kali.’ Mtoto  wa miaka 15 

Dar es Salaam. Mkazi wa Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpa mimba na kumwambukiza,Ukimwi mtoto wa umri wa miaka 15.
Pamoja na kumwambukiza magonjwa, mtuhumiwa pia anadaiwa kuharibu sehemu za siri na nyuma ya maumbile ya mtoto huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Amana.
Mtuhumiwa wa tukio hilo ni  mlinzi wa minara ya simu, na inadaiwa kuwa alimshawishi mtoto huyo aliyekuwa anafanya kazi za ndani, aache kwa madai kuwa anamtafutia kazi yenye kipato kikubwa.
Akisimulia mkasa huo, katika Hospitali ya Amana alikolazwa, huku akitoa machozi, mtoto huyo alisema “mimi natokea Masasi mkoani Mtwara. Mama mmoja wa Mbagala alikuja kunichukua kwa ajili ya kumfanyia kazi za ndani lakini alinifukuza kazi akisema sijui kazi,”alisema na kuongeza:
“Nilihangaika na nikapata kazi za ndani kwa mama mmoja wa Gongo la Mboto ambako baba huyu mlinzi wa minara ya simu aliniambia niache kazi, niliyokuwa ninalipwa Sh20,000 na niende kufanya kazi yenye malipo ya Sh40,0000”.
 Alidai kuwa baada ya kutoroka kwa aliyekuwa akimfanyia kazi awali, alihamia kwa mlinzi huyo aliyekuwa amepanga eneo la  Vikongoro, Chanika iliyopo Manispaa ya Ilala na kukaa huko kwa madai atampeleka kwenye kazi hiyo.
Alidai uhusiano wao alipokuwa akienda sokoni na hata baada ya kuhamia kwake alilazimisha kumingilia kimwili na kinyume na maumbile. “Ikawa anafanya hivyo...kila siku akitoka kazini alikuwa ananilazimisha kufanya tendo la ndoa hivyo alikuwa ananiingilia mbele na nyuma na kunisababishia maumivu.  Nikimwambia naumia ananitishia sin’topata hata hiyo kazi yenyewe” na kuongeza:
“Sasa nikawa najiona niko tofauti,nikaanza kutokwa na vipele sehemu ya mbele na nyuma vinawasha sana na nimejikuna na sasa vimekuwa vidonda hivi hapa (anamwonyesha mwandishi) hata mwenyewe unaona na vinatoa  harufu kali”.
Akaongeza kuwa baada ya kuona  vidonda vimezidi, kabla na baada ya kufanya tendo la ndoa anachemsha maji ya moto huku yakichanganywa na dawa kwa ajili ya kujikanda sehemu zilizoathirika.
Amesema licha ya kuathirika hivyo, mwanaume huyo alikuwa akimzuia kutoka nje ya nyumba hiyo na alikuwa akioga na kujisaidia kwenye chumba hicho hadi anaporudi kazini mwanaume huyo na kumwaga huku chakula akiletewa na wakati mwingine analala bila kula.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala , Marietha Minangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema, upelelezi haujakamilika na mtuhumiwa yupo kituo kidogo cha Polisi Stakishari kwa mahojiano zaidi. Ili kupata taarifa zaidi juu ya mkasa huu usikose kusoma Mwananchi Jumamosi.

KATIBA : Dk Mvungi alazimika kuhubiri dini Misenyi


 

 
Na Editha Majura, Mwananchi 
Wajumbe 96 wa Mabaraza ya Katiba, Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, wamekutana kujadili Rasimu ya Katiba Mpya, kwa lengo la kuiboresha, kazi itakayodumu kwa siku tatu.
Akifungua mkutano huo jana, Afisa Utumishi wa wilaya hiyo, Donard Nssoko, alitaka wajumbe hao watoe maoni kwa niaba ya wananchi  ili Katiba ijayo iwe yenye maslahi kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Katika hali inayoashiria kuwa, tume imedhamiria kudhibiti wajumbe wa mabaraza hayo,wasiingize maoni yanayotokana na shinikizo la makundi ya kisiasa, kidini na kiuana harakati, mbinu mbalimbali za kubadili fikra za wajumbe hao zilitawala ufunguzi wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa Tume mkoani humo, Dk, Sengondo Mvungi aligeuka muhubiri alipokuwa akielekeza namna wajumbe wanavyotakiwa kutekeleza jukumu hilo, baada ya maelezo yake kulenga kujenga hofu ya Mungu ndani ya wajumbe.
“Mmetumwa na wananchi siyo mjigeuze tume, bali mboreshe maoni yao kwa kuandika kila kitakacholetwa na mjumbe, ili kikafanyiwe kazi na tume; kushiriki kwenu kuunda sheria kuu kwa Watanzania siyo suala la kibinadamu, bali Mungu amekushirikisha ufanye kazi hiyo kwa niaba yake,” alieleza Dk, Mvungi
Dk. Mvungi aliwataka watambue kuwa hawapo kutumiwa na makundi fulani, kuchakachua kwa kubadili maoni ya wananchi yaliyo katika rasimu, bali kuyaboresha na kwamba kama ilivyo kwa imani za Kikristo na Kiislamu, kwamba wanaoshiriki kujenga Kanisa au Msikiti wamebarikiwa.
Alisema kidunia, wanaoshiriki kuunda Katiba ambayo ni sheria kuu ya nchi, wamebarikiwa na kwamba kinyume na baraka za Mungu ni laana, hivyo akaasa wanapotekeleza jukumu hilo, wajitambue kuwa wanamtumikia Mungu kwa ajili ya watu wake wa Tanzania.
“Mimi siyo Padri, Askofu wala Sheikh nakuelekeza haya, ili ufahamu kuwa usipokuwa mwaminifu kwa Mungu na taifa lako katika hili, hutapata nafasi ya kujitetea mbele za Mungu, msije mkasema hatukujua kuwa kazi ya kutunga Katiba ni ya Mungu; ukikosea utahukumiwa,” Dk. Mvungi alieleza
Mjumbe wa Sekretalieti ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Marlin Komba kabla ya kufungua mkutano huo, alitoa karatasi kwa kila mjumbe ili iandike wadhifa na sifa yake katika jamii aliyotoka. Vikakusanywa na kuhifadhiwa kwenye bahasha moja.
“Vyeo na sifa zenu zimehifadhi kwenye bahasha hii, ukumbini mmebaki wajumbe wa mabaraza ya Katiba, mtakaoboresha rasimu ya Katiba ili ipatikane Katiba itakayokidhi mahitaji ya Watanzania siyo kwa maslahi ya dini, siasa au uanaharakati,” Komba alieleza
Kama hiyo haitoshi, mwisho wa maelekezo ya tume, Komba aliongoza mabaraza hayo kuimba ubeti mmoja wa wimbo wa taifa, akihimiza kuzingatia umuhimu wa kumshirikisha Mungu na kuzingatia utaifa katika kazi wanayotakiwa kufanya.
Baadhi ya wananchi walionekana kupendelea zaidi makundi fulani ya wananchi, mambo ambayo yanaonekana wazi kwamba yanaweza kuifanya katiba isizae matarajio ambayo wengi wanayo ya kuwepo kwa katiba iliyo safi kwa wote.

Mishahara mipya serikalini 2013


 
Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimuudumia mgonjwa hospitalini hapo. Wafanyakazi wa sekta ya afya ni miongoni wa walio ongezewa mishahara na serikari katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14. Picha na Maktaba 
Dar. Serikali imetangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma itakayoanza kutumika mwezi huu, huku kima cha chini kikiongezwa kwa asilimia 41.18 kutoka Sh 170,000 hadi Sh240,000.
Vilevile, mishahara ya watumishi wengine wa umma imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41. Waraka namba moja kwa watumishi wa umma uliotolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi Julai 2 mwaka huu, unaeleza kuwa marekebisho hayo ya mishahara yatahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa.
Wengine watakaonufaika na marekebisho hayo ni watumishi walioshikizwa kwenye taasisi za umma na watumishi ambao watakuwa kwenye likizo inayoambatana na kuacha kazi, kustaafu kazi au kumaliza mikataba baada ya Julai mosi mwaka huu.
Waraka huo umeonyesha kuwa watumishi wa serikali ambao wanapata mishahara binafsi isiyo ndani ya viwango vya mishahara ya serikali hawatahusika na marekebisho hayo.
Mei 29 mwaka huu, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, aliliambia Bunge, kwamba Serikali imekamilisha majadiliano ya kuongeza kima cha chini cha mshahara katika sekta 12 binafsi, kitakachoanza kutumika rasmi Julai mosi.
Waziri Kabaka alitaja sekta hizo kuwa ni ya Ujenzi, Shule Binafsi, Nishati, Viwanda na Biashara, Hoteli na Huduma za Majumbani, Ulinzi Binafsi, Madini, Afya, Uvuvi na Huduma za Majini, Usafirishaji, Mawasiliano na Kilimo. Kwa mujibu wa Kabaka, mishahara imepanda kwa kiwango cha asilimia kati ya 21 na 65 huku Afya ikiongoza kwa kuongezwa ikifuatiwa na sekta ya hoteli na huduma za nyumbani yenye asilimia 55.
Mei mosi mwaka huu akiwa mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete, aliahidi unafuu wa maisha kwa wafanyakazi kwa kuangalia uwezekano pia wa kupunguza kodi kwenye mishahara, Lipa Kadiri Unavyopata (PAYE).
Kuhusu kuongeza mishahara, Rais Kikwete aliahidi wafanyakazi wote kwamba Serikali itaendelea kuiongeza kulingana na hali ya uchumi wa nchi. Waraka huo unaonyesha kuwa mishahara mipya kwa watumishi wa serikali kada ya masharti (operational service), ngazi ya mshahara na mshahara mpya kwenye mabano ni;
TGOS A
TGOS A 1. (Sh240,000), TGOS A 2. (Sh245,600), TGOS A 3. (Sh251,200), TGOS A 4. (Sh256,800), TGOS A 5. (Sh262,400), TGOS A 6. (Sh268,000), TGOS A 7.(Sh272,000), TGOS A 8(Sh279,000), TGOS A 9.(Sh284,800), TGOS A 10(Sh290,400), TGOS A 11(Sh296,000), TGOS A 12(Sh301,600), TGOS A 13(Sh 307,200), TGOS A 14(Sh312,800), TGOS A 15(Sh 318,400), TGOS A 16(Sh324,000), TGOS A 17(Sh329,600) na TGOS A 18(Sh335,200).
TGOS B
TGOS B 1. (Sh347,000), TGOS B 2. (Sh356,500) TGOS B 3 . (Sh366,000), TGOS B 4 . (Sh375,500), TGOS B 5. (Sh385,000), TGOS B 6. (Sh394,500), TGOS B 7. (Sh404,000), TGOS B 8. (Sh413,500), TGOS B 9. (Sh423,000), TGOS B 10. (Sh432,500), TGOS B 11 . (Sh442,000) na TGOS B 12. (Sh451,500).

Sunday, July 14, 2013

ASKARI SABA WA TANZANIA WADAIWA KUUAWA DARFUR.


Dar es Salaam. Wanajeshi saba wa Tanzania, ambao ni miongoni mwa kikosi cha Umoja wa Mataifa, cha kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan, wanadaiwa kuwa wameuawa.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zilisema kwamba wanajeshi hao wa Tanzania, wamekufa kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, miili yao wanajeshi hao bado ipo nchini Sudan ikisubiri taratibu za kusafirishwa kuletwa nchini.
Hii ni mara ya kwanza kuripotiwa kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kufa kwa wakati mmoja.
Agosti mwaka jana wanajeshi watatu wa Tanzania huko Darfur waliripotiwa kuuawa kwenye tukio kama hilo.
Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) , Kanali Kapambala Mgawe alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu vifo vya wanajeshi wa Tanzania huko Darfur, alisema kuwa naye amesikia, lakini hana taarifa rasmi kwa mujibu wa taratibu za kiofisi.
Hii ni mara ya pili kwa wanajeshi wa Tanzania kuuawa katika Jimbo la Darfur, ambapo Agosti mwaka jana, Kanali Mgawe alinukuliwa na vyombo vya habari akithibitisha kutokea kwa vifo vya askari watatu ambao gari lao lilizolewa na maji walipokuwa wakivuka mto uliokuwa umefurika maji.
Kanali Mgawe aliwataja askari hao kuwa ni Sajini Julius Chacha, Sajini Anthony Daniel na Koplo Yusuph Said na kwamba askari wengine walinusurika baada ya kuogolea.
Tanzania ina askari 850 kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani jimbo la Darfur, ambao ni sehemu ya askari 1,081 wa kulinda amani katika jimbo la Darfur.
Wanajeshi hao wa Tanzania wametawanywa kwenye miji ya Khor Abeche na Muhajeria kusini mwa Darfur.
Aprili mwaka huu Tanzania ilipeleka wanajeshi wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kupambana na kikundi cha waasi wa nchi hiyo M23 kinachopigana kuiangusha serikali ya DRC.
Majeshi ya Tanzania yalipelekwa kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa. Tanzania inaungana na nchi za Afrika Kusini na Malawi kukamilisha kikosi cha wanajeshi 3,000. Tanzania imepeleka wanajeshi 850.(MWANANCHI)

ARUSHA SI SHWARI-SHEIKH AMWAGIWA TINDIKALI.

ARUSHA,hali ikiwa bado tete mkoani Arusha kutokana na tishio la uwepo vurugu za kisiasa pamoja na kundi la watu ambalo halijafahamika linalotekeleza vitendo vya kigaidi, tukio lingine lenye mwelekeo na sura ile ile limetokea tena jana.

Katika tukio la sasa, Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Arumeru, Said Makamba, amemwagiwa majimaji yanayodaiwa kuwa tindikali na kumsababishia maumivu makali usoni na kifuani.

Tukio hilo limetokea wakati wakazi wa Arusha mjini wakijiandaa kupiga kura leo, katika uchaguzi wa madiwani wa kata nne ambao tayari umeonyesha dalili mbaya, kutokana na kuibuka vitendo vyenye kuashiria kuuvuruga.
Tukio hilo, ambalo hata hivyo haijajulikana kama limetokana na masuala ya kisiasa au la, linafanana mazingira na lile la bomu lililorushwa kwenye mkutano wa kuhitimisha kampeni za Chadema Julai 15 mwaka huu, kwani yote yametokea siku moja kabla ya uchaguzi.

Taarifa  zinaeleza Sheikh huyo alikutwa na dhahama hiyo nyumbani kwake, huko eneo la Sombetini, wakati alipotoka nje ya nyumba yake kwenda kujisaidia, ndipo ghafla akatokea mtu akiwa na kikombe chenye majimaji hayo na kummwagia usoni.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Shaban Juma Abdalah, akizungumzia tukio hilo, alisema baada ya kumwagiwa tindikali, sheikh huyo alisaidiwa na majirani kukimbizwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, alikolazwa hadi hivi sasa.

Akizungumza kwa tabuSheikh Saidi Makamba, alisema tukio hilo lilimkuta akiwa anatoka katika Msikiti wa Jabal Hiraa Kwa Mrombo, ambapo mara baada ya kufika nyumbani aliingia ndani na kubadilisha nguo.

“Nilipomaliza kubadilisha nguo nilitoka nje kwa ajili ya kwenda msalani, baada ya kumaliza nikiwa natoka nje ghafla nilimuona kijana mmoja akinifuata kwa kasi huku akiwa ameshika kopo mkononi na alionekana mwenye shari.

“Nikiwa sijatafakari nini kinaendelea, ghafla niliona akinimwagia maji usoni, ambapo nilianza kusikia harufu kama ya spirit au petroli hivi, lakini hapo hapo macho yangu yalishindwa kabisa kufunguka na ndipo nilipoanza kupiga kelele.

“Nikiwa nje, mke wangu alikuja na kunichukua hadi ndani, baadaye ndio wakanileta hapa hospitalini kwa ajili ya matibabu,” alisema Sheikh Makamba.

Hata hivyo, Sheikh Makamba amesema kuwa hisia zake zinamtuma kuamini kuwa watu waliofanya hivyo huenda wakawa ni wale wanaotofautiana ndani ya dini ya Kiislamu.

Sheikh Makamba aliomba msaada wa matibabu zaidi kwa mtu yeyote ambaye ataguswa kumsaidia, kwani ameumia.

Tukio hilo lilimlazimisha Sheikh wa Mkoa kuitisha kikao cha dharura jana, kuzungumzia tukio hilo ambapo walivitaka vyombo vya dola kuwasaka wahalifu waliohusika katika tukio hilo la kinyama.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alipoulizwa juu ya tukio hilo alisema kuwa bado halijamfikia na kwamba kama tayari limeripotiwa atalifanyia kazi.

Matukio ya kigaidi kama kumwagiwa watu tindikali, milipuko ya mabomu na matumizi mengine ya silaha dhidi ya viongozi wa dini na wananchi katika mikusanyiko mbalimbali sasa yanaonekana kuanza kuzoeleka nchini.(MTANZANIA)

Saturday, July 13, 2013

TAIFA STARS YALALA 1-0 KWA UGANDA.

http://api.ning.com/files/IvqemBCauJFrdL5Kt9Q-SdQO*4G*DTWQ*DOV27oJq5B10EbCKNEiW6VpU1ac0pUuaSHOk7uoHA2m0CgzRnAsoY4LwNxwzAUo/IMG_4520.JPG?width=640 

http://api.ning.com/files/IvqemBCauJEqIkNwfL8F-IQuYWL5Z7snTXFc8-dnWisB1wfpXMrEyjITdj0PMPmHnDY79HGQNZ8Vn2BkChWcATggQHZjM7ZM/IMG_4536.JPG?width=640
Taifa Stars wakitoka vichwa chini.
DAR ES SALAAM,MATUMAINI ya timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushiriki fainali za CHAN nchini Afrika Kusini imefifia baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes'. Taifa Stars imelala katika mechi ya kwanza iliyopigwa leo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa matokeo hayo, Stars inasubiri mechi ya pili itakayopigwa jijini Kampala wiki mbili zijazo na kama itafanikiwa kuibuka kifua mbele zaidi ya matokeo ya leo itakuwa na uhakika wa kushiriki fainali hizo ila kama matokeo yatakuwa vinginevyo basi safari ya Stars itakuwa imeishia hapo.

HUYU NDIYE MZEE ANAYETAKA KUMFUFUA MWALIMU NYERERE.

 
 
Mzee (pichani) aliyeibuka hivi karibuni akidai kuwa ana uwezo wa kumfufua Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere amezua gumzo. Babu huyo aliibuka katika studio za Kyera FM huko mkoani Mbeya akihitaji msaada wa kumfikisha Butihama alipozikwa Mwalimu Nyerere mwaka 1999 ili amfufue. Mzee huyo alikuwa na ufunguo mkononi ambao anadai ndiyo utakaotumika kumfufua Nyerere. Anaeleza kuwa akishamfufua Mwalimu Nyerere ndiye atakayesimamia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. 

Friday, July 12, 2013

CCM VS CHADEMA -VITA KALI.

 
DAR ES SALAAM,Siku tatu baada ya Rais Jakaya Kikwete kuponda mpango wa Chadema kuanzisha kambi kwa ajili ya mafunzo ya ulinzi kuwalinda viongozi na wanachama wake,  chama hicho kikuu cha upinzani nchini kimeibuka na kusema kuwa kinaendelea na mpango huo na kambi hizo zitaanza rasmi wiki ijayo.
Kimesema hakitishwi na kauli ya Jeshi la Polisi kukionya juu ya  uanzishwaji wa mafunzo hayo,  kwamba jeshi hilo linatakiwa kuanza kukizuia Chama Cha Mapinduzi (CCM)  kwanza, kwa maelezo kuwa chama hicho tawala pia kina kikundi cha ulinzi ‘Green Guards’ ambacho kinafanya mafunzo ya kijeshi, huku kikitumia silaha za moto.
“CCM ndiyo wataipeleka nchi hii pabaya, wanawafundisha vijana huku wakiwabebesha  bunduki, wanajenga taifa la aina  gani, bunduki ni silaha ya kivita sasa wanaandaa watu kupigana na nani” alisema Mkurugenzi wa Organaizesheni na Mafunzo wa chama hicho, Benson Kigaira jana wakati akizungumza na wanahabari huku akionyesha picha za mafunzo ya CCM, zinazoonyesha vijana wakiwa wamebeba silaha (hata hivyo ni mbao zilizotengenezwa kwa mfano wa bunduki).
Wakati Chadema wakieleza hayo, CCM kimeshtushwa na taarifa hizo na kueleza kuwa hali hiyo sasa inahatarisha usalama wa nchi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Martin Shigela alisema ni vyema Chadema kikawaambia wananchi wawalinde, kuliko kuanzisha mafunzo huku akimtaka Msajili wa Vyama vya siasa nchini, John Tendwa kulitizama kwa kina suala hilo.
Akifunga Kongamano  la Amani lililoandaliwa  na Kituo cha Demokrasia  Tanzania (TCD), Dar es Salaam Julai 10, mwaka huu, Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa pia alikosoa kitendo cha Chadema kususia kongamano hilo alisema, “Sasa hawa kweli wanapenda amani yetu wakati hawapendi tuzungumze wanataka watu wauane, wapigane.”
Mbali na Rais Kikwete, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, SSP Advera Senso juzi alikionya chama hicho kuhusu mpango huo akisema kuwa kitendo cha chama chochote cha siasa kikiwemo Chadema, kuanzisha kikundi cha kujihami ni kinyume na sheria za nchi na endapo watafanya hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kauli ya jana ya Chadema ni mwendelezo wa ile iliyotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe Julai 9, mwaka huu, ambapo alisema  kimechukua hatua hiyo baada ya Serikali na vyombo vyake vya ulinzi na usalama kushindwa kufanyia kazi malalamiko yao kuhusu mauaji, vitisho na matukio ya kutisha wanayofanyiwa baadhi ya viongozi na wanachama wao.
Katika ufafanuzi wake Kigaila alisema Chadema hakianzishi vikundi vya kijeshi, bali mafunzo ya  kuwafundisha walinzi wa chama hicho  ‘Red Brigade’, jinsi ya kujilinda.
“Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni haki kwa raia yeyote kujilinda, Chadema ni taasisi ni haki yetu kuilinda taasisi yetu ndiyo maana tumesajili kikundi chetu cha ulinzi, sasa nani anatutisha, tunataka polisi waanze na CCM kwanza ambao katika mafunzo yao  wanafundisha hadi kupiga saluti na kutumia silaha,” alisema.
Alisema mafunzo hayo yataanza rasmi wiki ijayo, huku akisita kutaja siku yatakayoanza, wala mikoa yatakayofanyika na kusisitiza kuwa hayo yatatangazwa wiki ijayo wakati vijana wakienda katika mafunzo.(MWANANCHI)

TANZANIA YAIPIGA MKWARA RWANDA KUHUSU TISHIO LA KUISHAMBULIA

SERIKALI ya Tanzania imeipa onyo kali nchi ya Rwanda ikiitaka isijaribu kuota ndoto za kuishambulia kijeshi, vinginevyo itajibu mapigo kwa nguvu zote na kuhakikisha kuwa imeichakaza.
Kauli hiyo ya kwanza nzito imetolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa kufuatia taarifa ya matamshi makali yanayodaiwa kutolewa na Rais Paul Kagame wa Rwanda, dhidi ya Rais Jakaya Kikwete na kutishia kuishambulia Tanzania.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa wizara hiyo, Mkumbwa Ally, alisema ingawa Serikali ya Tanzania hadi sasa inajua haina ugomvi wowote na Rwanda, lakini amekiri kuwapo kwa kile alichokiita ‘kupishana lugha’ kwa Rais Jakaya Kikwete na Paul Kagame.
Mkumbwa alikiri Serikali ya Tanzania kunasa matamshi yanayodaiwa kutolewa na Rais Kagame katika moja ya hotuba zake aliyoitoa Juni 30, nchini kwake wakati akihutubia katika hafla moja ya vijana.
Kwa mujibu wa hotuba hiyo, ambayo kwa wiki sasa imesambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii, Kagame anadaiwa kusikika akitoa matamshi ya vitisho dhidi ya Rais Kikwete, kwamba anamsubiri katika wakati aujuao na kumchapa.
Baadhi ya maneno yanayodaiwa Rais Kagame aliwaambia vijana waliokutana katika mkutano wao uliojulikana kama ‘Youth Konnect’ na kufadhiliwa na mke wake, Janet Kagame, yanasema: “Huyu mtu mliyemsikia akiwa upande wa Interahamwe na FDLR na akashauri majadiliano….majadiliano?”
Aidha, Kagame anadaiwa kusema kuwa hatakuwa tayari kujadili jambo hilo, isipokuwa atamsubiri Rais Kikwete sehemu muafaka na ‘kumtandika’.
“Sitapoteza muda wangu kumjibu Kikwete, inajulikana maana kuna mahali hataweza kuvuka…haiwezekani,” alikaririwa akisema Rais Kagame, akilenga kumtisha Rais Kikwete.
Mbali na Kagame, baadhi ya viongozi kadhaa wa serikali ya Rwanda wamekuwa wakimshambulia Rais Kikwete wakimpachika majina ya kejeli ya; “Rais mhurumia magaidi, wauaji wa kimbari, mkorofi na mwenye dharau.”
Mkumbwa hata hivyo alisema Serikali ya Tanzania haina sababu ya kuingia katika vita na Rwanda, kwa sababu tu ya ushauri alioutoa Rais Kikwete wa kuitaka ikutane na wapinzani wake wanaoishi ndani ya nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kujadiliana kuhusu amani ya nchi za Maziwa Makuu.
Alisema msimamo wa Tanzania utabaki kuwa uleule wa kuitaka nchi hiyo ikubali kukaa meza moja na wapinzani wake, ili kumaliza migogoro inayoendelea katika nchi hizo za maziwa makuu, ambao unaungwa mkono na jumuiya ya kimataifa na SADC.
“Unajua mgogoro wa DRC na Rwanda hauwezi kumalizika bila ya nchi hizo kukaa meza moja na wapinzani wao ili kupata suluhu ya kudumu,” alisema Mkumbwa.
Aliwataka Watanzania kuwa watulivu na kuendelea na kazi zao kama kawaida, kwani serikali yao iko makini katika kulinda mipaka yake.
Chanzo cha mzozo
Msuguano baina ya nchi hizi mbili ulianza siku chache tu baada ya kumalizika kwa kikao cha viongozi wa nchi za Maziwa Makuu na ambacho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, chini ya uenyekiti wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Rais Kikwete wakati akimtaarifu Rais Museveni kile walichokuwa wamekijadili katika kikao hicho kwa vile aliketi kwa muda kwa kuwa alichelewa kuwasili, alisema ni vema serikali za Rwanda na Uganda zifungue mlango wa mazungumzo na waasi wao na akaanza kutaja majina ya vikundi vya uasi vya nchi hiyo vilivyopo nchini DRC.
Habari zinasema kauli ya Rais Kikwete iliungwa mkono na Rais Museveni akisema: “Bila mazungumzo hatutafika popote pale”.  Hata hivyo, matamshi hayo yalijibiwa kwa ukali na serikali ya Rwanda, kiasi cha kumlazimu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kutoa tamko bungeni.
Kwa kauli yake, Membe alisema serikali ilikuwa imeshangazwa na shutuma hizo za Rwanda kwani halikuwa jambo baya kutoa ushauri uliolenga kuleta mapatano na kuepusha umwagaji zaidi wa damu wa wananchi. Akaongeza kuwa, ilikuwa ni wajibu wa Serikali ya Rwanda kuupokea ama kuukataa, na wala si kutoa maneno ya kejeli na vitisho.
Kauli ya Zitto
Akizungumzia kauli hiyo ya vitisho, mwanasiasa machachari hapa nchini na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, alisema ushauri wa Rais Kikwete kwa Rwanda ulikuwa wa busara mno na akashangaa kuona nchi hiyo jirani ikitoa vitisho, kejeli, dharau na ukosefu wa adabu kwa Kikwete.
Katika moja ya tamshi lake alilolitoa jana katika mitandano ya kijamii, Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) alisema Marekani wanaongea na waasi wa kundi la Taliban, hivyo hakuna dhambi kwa Rwanda pia kufanya hivyo.
“Pia kama hutaki ushauri si unakataa tu, sasa kuanza kurushiana maneno ya nini tena? Hutaki ushauri basi. Maneno ya kila siku ya nini? Tangu Kikwete amesema kule Addis, hajasema tena. Membe (waziri) akajibu Dodoma Tanzania haijasema tena. Kigali inasema mambo haya kila siku kwa ajili ya nini?
“Taliban na Al Qaeda si wale wale? Wale watoto waliozaliwa mwaka 1994 na wakimbizi wa Kihutu waliopo Kongo nao ni wauaji? Tufikiri vizuri mambo haya. Kuna ‘genociders’ wasakwe, wakamatwe wahukumiwe. Kuna watu wana haki kabisa ya kutaka kushiriki kwenye siasa za Rwanda na wanazuiwa, wameshika silaha. Hawa lazima wakae meza moja wakubaliane,” alisema Zitto.
Mwanasiasa huyu alisema kwa sasa serikali za nchi hizo mbili zinatakiwa kuingia katika vita ya kupambana na kuondoa umasikini wa watu wake na si vita ya mtutu wa bunduki.
“Busara itumike kwa viongozi ‘neutral’ kama Uhuru Kenyatta kuwaweka pamoja Kagame na Kikwete wamalize tofauti zao. Haya maneno hayana maana yoyote,” alisema.
Alisema vita haitamuumiza Rais Kagame wala Rais Kikwete na familia zao, bali itaumiza wananchi wa kawaida wa mikoa ya Kagera na Kigoma na mikoa ya mpakani ya Rwanda.
“Vita itaturudisha nyuma sana kwenye juhudi za maendeleo. Vita itazima harakati za kujenga demokrasia nchini.  Busara itumike tu,” alisema Zitto.

Thursday, July 11, 2013

SHIRIKISHO LA SOKA LAVIFUNGIA VILABU VILIVYOFUNGANA 79-0.

Shirikisho la soka nchini Nigeria limevifungia vilabu vinne baada ya kuandikisha matokeo ya kushangaza katika michuano ya kupanda daraja.

Vilabu hivyo ni pamoja na Plateau United Feeders FC, Akurba FC, Police FC na Bubayuaro FC.
 
Plateua United Feeders iliichabanga Akurba FC mabao 79 kwa 0 huku Police Machine FC ikaikagaraza Bubayaro FC mabao 67 kwa 0.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi katika chama cha soka nchini humo NFF Muke Umeh,amesema kuwa matokeo hayakubaliki kamwe na lazima uchunguzi ufanyike ili kubaini vipi mabao hayo yalifungwa.
 
Plateau United na Police Machine FC walicheza mchuano huo wakiwa na alama sawa na mshindi alihitajika kupata mabao mengi li kujihakikishia kusonga mbele ili kupanda daraja na kucheza ligi ya Kitaifa.
 
Plateua United Feeders walipata mabao 72 katika kipindi cha pili cha mchuano wao huku, huku Police wakiandikisha mabao 61 katika kipindi cha kwanza cha mchuano wao.
 
Uongozi wa soka nchini Nigeria unasema kuwa hauwezi kueleza kilichitokea na wale wote watakaobainika kusababsiha matokeo hayo watachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za soka nchini humo.

ALIYEFARIKI SIKU YA HARUSI YAKE AZIKWA NA MWANAE.

ROMBO, Ilikuwa ni majonzi, vilio na huzuni katika kijiji cha Mahalu, wilayani Rombo, Kilimanjaro kufuatia mazishi ya aliyetarajiwa kufunga ndoa Jumamosi marehemu Levina Swai pamoja na mwanawe.
Marehemu Levina alizikwa na mwanaye kaburi moja baada ya kichanga hicho kufariki siku hiyo hiyo mara baada ya mama yake kupoteza maisha kwa kile kilichodaiwa ni kuugua Malaria, shinikizo la damu kuwa chini na upungufu wa damu.
Marehemu Levina alifariki wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Akizungumza katika kijiji cha Mahalu kata ya Makiidiwilayani Rombo, alikozikwa,wifi wa marehemu, Hortensia Mrima alisema wifi yake alifia hospitalini na alikuwa mwalimu wa Shule ya Msingi Nndawa mkoani Lindi akiwa katika mpango wa ajira ya walimu wapya.
“Mimi ndiye nilikuwa namuuguuza hospitalini tangu Alhamisi iliyopita na alikuwa anasumbuliwa na malaria na kupungukiwa na damu na pressure (shinikizo la damu) kuwa chini,”alisema Mrima.
Ibada ya mazishi ilianza saa 8:30 mchana ikiongozwa na Padri Emmanuel Mavengero na kuhudhuriwa na waombolezaji kutoka Tanga na Kilimanjaro.
Mazishi hayo yalitawaliwa na simanzi huku waombolezaji wengi akiwamo aliyetarajiwa kumuoa marehemu Levina,Gabriel Swai muda wote alikuwa akibubujikwa na machozi na kushindwa kuzungumza.
Wifi huyo alieleza kuwa wifi yake alipopimwa alikutwa na Malaria 13 na kupewa dawa za malaria za SP na dripu za Quinine ambazo zilimlewesha sana na kuendelea kudhoofu.
“Siku hiyo ya Alhamisi alikata kauli akawa haongei ikabidi daktari amwekee dripu za Glucose ili kumuongezea nguvu na shinikizo la damu ilirudi sawasawa lakini bado alikuwa amelegea na alikuwa haongei,”alisema.
Ilipofika Jumamosi ambayo ndiyo siku iliyokuwa imepangwa kufunga ndoa na Gabriel Swai, ikabidi madaktari wamuwekee maji ya uchungu ili kumuokoa mtoto baada ya mama kuwa mahututi.
“Yale maji ya uchungu yalimsaidia akaweza kujifungua mtoto wa kiume mwenye uzito wa kilo 1.7 na baada ya kujifungua alipoteza fahamu na saa 8:05 mchana akafariki dunia,”alisema.
Kwa mujibu wa Mrima, mtoto aliendelea kuishi huku akipewa maziwa lakini alikuwa akiyatapika, hadi ilipofika saa 5:00 usiku alifariki dunia.

Wednesday, July 10, 2013

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA TANO HAYA HAPA.



MAJINA YA WAVULANA-CLICK HAPA

MAJINA YA WASICHANA-CLICK HAPA

WATUHUMIWA WA BOKO HARAM WAFUNGWA MAISHA

Wanachama wanne wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Kiislamu la Boko Haram, wamehukumiwa kifungo cha maisha gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na mashambulio ya bomu yaliyosababisha vifo vya watu kumi na tisa.

Wanne hao walipatikana na hatia ya kupanga na kutekeleza mashambulio ya mabomu katika ofisi za tume ya uchaguzi na kanisa moja mwaka uliopita.

Hukumu hiyo ndiyo kali zaidi kuwahi kutolelwa kwa mwanachama au mshukiwa yeyote wa kundi hilo la Boko Haram.

Kundi hilo limehusika na mashambulio kadhaa ambayo yamesababisha maafa mengi katika maeneo ya Kaskkazini na Kati nchini Nigeria.

Katika miaka ya hivi karibuni kundi hilo limekuwa likiwalenga raia wa kawaida na zaidi ya watu elfu mbili wameuawa tangu kundi hilo la Boko Haram kuanzisha uasi mwaka wa 2009, katika juhudi zake za kutaka kuundwa kwa taifa jipya la Kiislamu katika eneo lililo na idadi kubwa ya Waislamu Kaskazini mwa Nigeria.

Hali ya ulinzi Kaskazini mwa Nigeria;

Hali ya hatari, ilitangazwa tarehe kumi na nne mwezi Mei mwaka huu, katika majimbo ya Kaskazini Mashariki ya Adamawa, Borno na Yobe, hatua iliyoishurutisha serikali ya nchi hiyo kutuma zaidi ya wanajeshi elfu mbili kushika doria katika eneo hilo na pia kuvunja kambi za wanamgambo hao.

BANTEKE AOMBA KUONDOKA ASTON VILLA.



Mchezaji wa klabu ya Aston Villa Christian Banteke amewasilisha ombi la kuondoka katika klabu yake na kuachia Chelsea na Aston Villa kuwania kumsajili kwa kitita cha Pauni Milioni 30.

Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka nchini Ubelgiji mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Aston Villa msimu uliopita akitokea klabu ya Genk ya Ubelgiji kwa kitita cha Pauni Milioni 7.

Benteke amekuwa akidaiwa kujiunga na klabu ya Arsenal, Chelsea na Tottenham Hotsupurs vilabu ambavyo vinatarajiwa kuendeleza mazungumzo na mchezaji huyo.

Uongozi wa Aston Villa unasema kuwa Banteke atasalia kuwa mchezaji wao ikiwa hatasajiliwa hivi karibuni kwa sababu alikuwa amesaini mkataba wa miaka mitatu na timu yake.

Kocha wa Villa Paul Lambert amesema kuwa ameshangazwa na kuhuzunishwa mno na Banteke kuhusu uamuzi wake kwa kile alichokisema mchezaji huyo hakuelewa kuwa mkufunzi huyo alikuwa anaijenga timu hiyo.

Katika hatua nyingine, mawakala wa mchezaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez anasema kuwa mchezaji huyo bado ana nia ya kuichezea klabu ya matufa bingwa barani Ulaya.

Klabu ya Liverpool imekataa Pauni Milioni 30 kutoka kwa klabu ya Arsenal ambayo imeonekana kutofutihwa na msimu wake nchini Uingereza.

Suarez alijiunga na Liverpool mwaka 2011 kwa kitita cha Puani Milioni 22 nukta 7 na ameichezea klabu hiyo mechi 96 na kuifungia mabao 51.

MATOKEO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KUTOLEWA LEO

DAR ES SALAAM, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imesema majina  ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu,  yatatangazwa leo.

Msemaji wa wizara hiyo, Bunyanzu Ntambi alisema jana kuwa, majina hayo yatatangazwa leo shughuli itakayofanyika katika ofisi za wizara hiyo.

 “Kesho (leo) saa nne, selected (waliochaguliwa) watatangazwa,” alisema Ntambi.

Awali Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema majina ya wanafunzi hao yatatangazwa siku yoyote ndani ya juma hili.

Mulugo jana alisema majina hayo hayajachelewa kutangazwa na kwamba wanafunzi wa kidato cha sita hufungua wiki ya tatu ya Julai na kwamba hata sasa bado hawajafungua.

“Matokeo tutayatoa wiki hii na  hatujachelewa kuyatangaza kwa sababu  kwa kawaida kidato cha tano na sita wanafungua shule wiki ya tatu Julai , kwa hiyo tukitoa wiki hii tutakuwa hatujachelewa,” alisema Mulugo.

Mmoja wa walimu wa Shule ya Sekondari ya Jangwani jijini Dar es Salaam, alisema kuwa kwa kawaida wanafunzi wa kidato cha tano huripoti shuleni wiki mbili kabla ya wale wa kidato cha sita kitu ambacho mwaka huu kimekuwa tofauti.

“Mpaka sasa hatujaambiwa kwa nini hii hali imekuwa hivi, kwa kawaida kidato cha tano huripoti shuleni wiki moja kabla ya kidato cha sita, lakini mpaka sasa waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano bado hawajatangazwa,” alisema Mwalimu huyo.

Wakati majina hayo yakitarajiwa kutangazwa leo, ni dhahiri kuwa shule za Serikali zenye kidato cha tano na sita zitaendelea kupata idadi ndogo ya wanafunzi tofauti na uwezo huku baadhi zisizo za Serikali zikitishia kuachana na biashara ya shule.

Hali hiyo inatokana na idadi kubwa ya wanafunzi kushindwa mtihani wa kidato cha nne, ambapo kwa mwaka 2012 waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu ni 35,349. Wwanafunzi walio katika nafasi kubwa ya kuchaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano ni wale waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu.(MWANANCHI)


BIBI HARUSI MTARAJIWA AFARIKI SAA MOJA KABLA YA HARUSI YAKE.

HANDENI,TANGA,Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Bibi Harusi ambaye ni mkazi wa Chanika mjini Handeni, Levina Mmasi (23) amefariki dunia saa moja kabla ya ndoa yake kufungwa katika Kanisa la Katoliki la Roma Wilaya Handeni Jumamosi na hivyo kuilazimu kamati ya maandalizi ya harusi kujigeuza na kuwa ya msiba.

Kifo hicho kilichotokea Jumamosi mwishoni mwa wiki iliyopita, kimekuwa gumzo mjini Handeni huku wananchi wakisema kuwa ni tukio ambalo halijawahi kutokea katika wilaya hiyo.

Msemaji wa familia ya marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Firmin Mrimasha, alisema kuwa chanzo cha kifo cha Levina ambaye alijifungua mwanzoni mwa wiki iliyopita,ilikuwa ni homa aliyoipata ghafla siku ya Alhamisi na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni na kukutwa na malaria na kisha kulazwa kwa matibu.

 “Huyu bibi harusi alikuwa ametoka kujifungua, alikuwa na mtoto wa kiume kutokana na ujauzito wa miezi saba, ndipo ghafla Alhamisi akapata homa tukampeleka hospitali alikolazwa na baada ya kupata nafuu, aliruhusiwa Ijumaa.

“Baada ya kuruhusiwa akaanza maandalizi ya harusi na Jumamosi ambayo ndiyo siku ya ndoa yake, alijiandaa lakini ilipofika saa 8.05 akafariki dunia akiwa nyumbani akisubiriwa kwenda kanisani kufunga ndoa ambayo ilikuwa ifungwe saa 9.00,” alisema Mrimasha.

Alisema, “Inasikitisha sana ila imeshatokea yaani marehemu amefariki saa moja kabla ya ndoa yake na baada ya kifo hicho, mtoto wake naye alifariki muda mfupi baada ya mama yake kufariki dunia,” alisema Mrimasha.

Akizungumzia mkasa huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Harusi hiyo iliyogharimu Sh7.7 milioni, Abdi Kipacha alisema kuwa kwake ni tukio la kwanza kutokea tangu kuzaliwa kwake na kamwe hawezi kulisahau.

“Nilishazipangia kazi kamati za maandalizi, lakini ghafla tukapewa taarifa kuwa bibi harusi amefariki...Hatukuamini, ikabidi niwatangazie wanakamati wenzangu kuwa hakuna tena shughuli, bibi harusi amefariki,” alisema mwenyekiti huyo wa kamati na kuongeza:

“Kitu tulichokuwa tukisubiri ni kuambiwa bibi harusi angefika saa ngapi, lakini ghafla tukapewa taarifa za kifo, ilikuwa ni vigumu kuamini lakini ni kweli imetokea na inasikitisha kwani si jambo la kawaida,” alisema Kipacha.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na wanandugu ni kuwa marehemu alikuwa Mwalimu wa Shule ya Msingi Nndawa mkoani Lindi na kwamba alikuwa katika kundi la walimu wa ajira mpya ambayo hadi mauti yanamkuta alikuwa hajapokea hata mshahara wake wa awali.

Akizungumzia hali hiyo, Padri aliyekuwa afungishe ndoa hiyo, Max Sabuni wa kanisa hilo Katoliki Handeni alisema:       “Nimesikitishwa na tukio hili kwa kuwa halikuwahi kunitokea...Kilichobaki ni wanandugu kuwa watulivu kwa kuwa Mungu amechukua kiumbe wake kwa muda alioupanga.”

Aliwataka ndugu, jamaa na marafiki kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi.


Monday, July 8, 2013

Murray bingwa mpya wa Wimbledon

Andy Murray

Andy Murray amekuwa Muingereza wa kwanza kushinda taji la Wimbledon tangu mwaka 1936, ikiwa ni zaidi ya miaka 77.

Murray amemfunga Novak Djokovic raia wa Serbia kwa seti tatu kwa kwa bila katika mchezo wa fainal za wanaume za michuano ya tenesi ya Wimbledon.

Murray amemshinda mchezaji anayeorodheshwa wa kwanza duniani Novak Djokovic kwa seti tatu kwa bila za 6-4, 7-5, 6-4.

Andy Murray amesema anashindwa kuamini kile alichokifanya kwani mechi hiyo ilikuwa ngumu, huku joto likiwa kubwa lakini anashukuru ameweza kumaliza mechi hiyo kwa ushindi muhimu kwake na kwa taifa.

Hili ni taji la pili la michuano mikubwa ya tenesi duniani maarufu kama Grand Slam baada ya kushinda lile la Michuano ya wazi ya Marekani.

Muingereza wa mwisho kushinda taji la Wimbeldon ambalo hufanyika mjini London kila mwaka alikuwa ni Fred Perry aliyeshinda taji hilo kwenye michuano ya mwaka 1936.

Mwaka jana Andy Murray alipoteza mchezo wa fainali ya michuano ya Wimbledon kwa kufungwa na Roger Federer.

Malkia wa Uingereza, Elizabeth wa pili amemtumia ujumbe wa Pongezi Andy Murray kwa ushindi wake katika mechi ambayo ilishudiwa pia na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameroon

Nyati mweupe azua tafrani Ngorongoro

WAHIFADHI watafiti na wataalamu kadhaa, wako katika harakati za kumsaka Nyati wa ajabu anayedaiwa kuwa na rangi ya maziwa, ambaye hivi karibuni ameonekana katika mwambao wa bonde kuu la Ngorongoro (Kreta) na kusababisha tafrani kubwa.

Kwa mujibu wa mtalaam wa ikolojia katika mamlaka hiyo, Patrice Mattay, uwepo wa nyati (mbogo) huyo wa aina yake hifadhini hapo, kumeibua suala jipya katika utafiti wa wanyama pori, kwani hakujawahi kuwepo Nyati mwenye rangi nyeupe popote duniani. Kwa kawaida Nyati huwa anangozi yenye rangi nyeusi.

Nyati huyo mweupe aligundulika kwa mara ya kwanza na maafisa wa polisi wanaofanya kazi katika kituo cha polisi kilichopo ndani ya hifadhi hiyo, ambao wanasema mnyama huyo hupita katika maeneo ya kituo hicho majira ya asubuhi akiwa miongoni mwa mbogo wengine takribani 20. Ngorongoro ina nyati wapatao 350.

“Ni kweli hata mimi binafsi nimemshuhudia Nyati huyo mweupe akikatiza katika sehemu mbalimbali za hifadhi ya Ngorongoro majira ya asubuhi akiwa katika kundi la mbogo wengine,” alisema mkuu wa kituo cha Ngorongoro Afisa wa Polisi, JJ Paul.

Hadi sasa ni maaskari wanaofanya doria katika maeneo ya hifadhi hiyo, hususan nyakati za asubuhi, ndio wanaothibitisha kwa kiwango kikubwa kumuona Nyati huyo wa ajabu ambaye sasa anatarajiwa kuwa atakuwa kivutio kipya cha utalii nchini.

Meneja Uhifadhi katika mamlaka ya Ngorongoro, Amiyo T. Amiyo amesema tayari shirika lake limekwisha tuma askari wake kadhaa kumsaka Nyati huyo wa ajabu, ili kubaini eneo ambalo anapatikana kwa ajili ya kuwezesha utafiti zaidi.

“Na kwa mtu yeyote mwenye kutuletea taarifa kuhusu Nyati huyo mweupe zitakazotuwezesha kumpata mnyama huyo, basi naye pia atazawadiwa ipasavyo,” alisema Amiyo.

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ndiyo inayoongoza kwa kupata watalii wengi nchini na kwa mujibu wa Ofisa Utalii wa Shirika hilo, Asantaeli Melita, zaidi ya wageni 585,000 hutembelea eneo hilo, na hasa Kreta, kila mwaka.

Idadi ya wanyamapori walioko Ngorongoro kwa sasa inafikia 300,000 wengi wao wakiwa ndani ya bonde lenyewe huku baadhi na hasa twiga wakiishi nje ya Kreta.

Mbali na Mbogo wa jabu aliyegunduliwa hivi karibuni, eneo la Ngorongoro pia lina maajabu mengine kadhaa, ukiwemo kilima cha mchanga unaotembea bila kusambaratika, idadi kubwa ya Kakakuona, mnyama anayedaiwa kuwa na uwezo wa kutabiri, pamoja na idadi kubwa ya wanyama adimu kama Mbwa-mwitu na Faru.

USAFIRI DAR KITENDAWILI

DAR ES SALAAM, Abiria  waliokuwa wasafiri kwenda mikoani na nchi jirani, wamekwama katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo kutokana na uchache wa mabasi.

Mwananchi jana ilishuhudia mamia ya abiria wakisubiri mabasi yalikuwa njiani  kurejea Dar es Salaam ili na wao waweze kusafiri kwa mabasi hayo.

Katika kituo hicho ambacho kwa kawaida huwa na mabasi mengi, kwa siku ya jana muda wa saa nne hadi tano ni mabasi matatu tu ya Shabiby Line, Hood na Simba One ndio yalikuwa yakipakia abiria kuelekea Morogoro na Dodoma,huku kukiwa hakuna basi lolote la kuelekea mikoa ya Kaskazini.

Abiria hao wengi wakiwa ni wanafunzi walikuwa wakirejea shuleni kwa ajili ya muhula mpya wa masomo unaotarajiwa kuanza leo.

Wakizungumza na Mwananchi walisema wanadhani uhaba wa mabasi umetokana na uwapo wa wanafunzi wengi ambao wanarudi shule baada ya kumaliza likizo za katikati ya mwaka.

“Sisi tumekata tiketi tangu jana ya kwenda Dodoma, tunakwenda Msalato Sekondari,lakini leo tumefika hapa asubuhi na tulitakiwa kuondoka na basi la saa nne lakini mpaka saa tano hii tunaambiwa tusubiri basi liko njiani linakuja”walisema wanafunzi ambao hawakutaka kutaja majina.(MWANANCHI)

Saturday, July 6, 2013

Papa John Paul II kutangazwa Mtakatifu.

http://media.tumblr.com/tumblr_lk598yBV7a1qaf7km.jpg 

VATICAN, Papa Francis amethibitisha uamuzi wa kumtangaza kuwa mtakatifu mwenyeheri Yohane Paul ll ambaye alifariki dunia mwaka 2005.

Katika uamuzi wake jana, Papa Francis ameeleza kuwa miujiza mbalimbali na ushahidi wa matendo ya mwenyeheri Yohane Paul II yanampa nafasi ya kumtangaza mtakatifu kulingana na kanuni za Kanisa Katoliki.

Uamuzi huo wa kumtangaza mtakatifu Yohane Paul ll utamfanya Papa Francis kumweka katika orodha ya watakatifu kiongozi huyo ambaye aliongoza kanisa hilo tangu mwaka 1978 pamoja na Papa mwingine, Yohane XXlll, ambaye alifariki dunia miaka 50 iliyopita na ambaye alikuwa kipenzi cha wengi.

Kwa mamlaka yake, Papa Francis atamtangaza pia Papa Yohane XXlll kuwa mtakatifu, ingawa makao ya kanisa hilo, Vatican hayathibitishi rasmi muujiza wake.

Vatican ilieleza jana kuwa Papa Francis anao uwezo na mamlaka ya kumtangaza mtu yeyote kuwa mtakatifu kufuatana na mchakato ambao umewekwa na kanisa hilo na kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa, bila kuangalia au kuegemea zaidi kigezo cha muujiza.

Hata hivyo, Vatican inaeleza kuwa sherehe za kumtangaza mwenyeheri Papa Yohane Paul ll kuwa mtakatifu zitafanyika kabla ya mwisho wa mwaka.

Tayari, Desemba 8 imeandaliwa rasmi kama siku maalumu ya kufanyika kwa shughuli hiyo, kutokana na kuwa sikukuu kubwa ya kanisa hilo kwa kumbukumbu ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili, siku ambayo pia watawa hasa wa kike huweka nadhiri zao.

Vyombo vya habari vya Poland alikozaliwa mwenyeheri Papa Yohane Paul ll vimeendelea kueleza kuwa Oktoba ndiyo unaoweza kutumika kwa shughuli hiyo, siku ambayo ni ukumbusho wa kuteuliwa kwake kuwa kiongozi wa kanisa hilo mwaka 1978.

Hata hivyo, maofisa wa Vatican wameeleza kuwa itakuwa mapema mnno kwa shughuli hiyo kubwa kwa kanisa hilo.

Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi alithibitisha kuwa muujiza wa kwanza wa mwenyeheri Papa Yohan Paul ll ulihusisha mwanamke raia wa Costa Rica.

Gazeti la Kikatoliki la Hispania, La Razon limemtaja mwanamke huyo kuwa Floribeth Mora na kueleza kuwa alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya ugonjwa wa kichwa, ambao ulipona kwa maajabu Mei Mosi, 2011 , siku ambayo tukio la kutangazwa kwa Yohane Paul ll kuwa mwenyeheri kulifanyika mbele ya waumini 1.5 milioni katika Viwanja vya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican kwa heshima yake.

Katika matoleo kadhaa ya gazeti hilo mwezi uliopita, La Razon limeeleza kuwa Mora aliamka akiumwa kichwa Aprili 8 na kwenda hospitali, hali yake ilikuwa mbaya kiasi cha kurudishwa nyumbani na kuambiwa kuwa ataishi kwa mwezi mmoja.(MWANANCHI)

Thursday, July 4, 2013

RYAN GIGGS ATEULIWA KOCHA/MCHEZAJI MANCHESTER UNITED

MANCHESTER CITY-UINGEREZA,Klabu ya Manchester United leo imemtangaza mchezaji mkongwe zaidi wa klabu hiyo kuwa kocha wakati akiwa bado anaendelea kuichezea klabu hiyo.

Taarifa hizo zimethibitishwa na mtandao rasmi wa Manchester United kwamba Giggs ambaye hivi karibuni alimaliza mafunzo yake ya ukocha atakuwa mmoja ya jopo la makocha watakaomsaidia David Moyes kuendesha jahazi liloachwa na Sir Alex Ferguson.

Pia wakati huo huo kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba David Moyes amemteua Phil Neville kuwa kocha wa timu ya kwanza.

JESHI NCHINI MISRI LAMPINDUA RAIS MOHAMED MORSI.

The Egyptian army has toppled President Mohammed Morsi. (Amr Nabil/Hassan Ammar/AP) 
 
us-egypt-morsi.jpeg2-1280x960 
Jeshi nchini Misri limemuondoa madarakani Rais aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia nchini humo Mohamed Morsi na imemteuwa kiongozi wa muda wa nchi baada ya maandamano makubwa yanayoipinga serikali.

Akihutubia kwa njia ya televisheni jumatano jioni, mkuu wa jeshi, Abdul Fatah Khalil Al-Sisi alisema katiba ya Misri imesitishwa kwa muda na mkuu wa mahakama ya katiba ameteuliwa kuwa kiongozi wa muda nchini humo. Sisi alitangaza kwamba jeshi linaangalia watu wa Misri kufuatana na maandamano makubwa ya upinzani yakidai kuwa Rais Mohamed Morsi ajiuzulu.

Kufuatia hotuba ya kwenye televisheni Bwana Morsi alitoa taarifa kupitia akaunti yake ya Twitter, akiita hatua ya jeshi ni “mapinduzi kamili”. Aliwasihi wa-misri wote kukataa hatua ya jeshi lakini pia aliwataka kuwa na amani.

Kiongozi mpya wa muda nchini Misri, Adli Mansour ana umri wa miaka 68 ni mkuu wa sheria katika mahakama ya juu ya katiba. Ataapishwa alhamisi.Kusoma zaidi bofya

Kama sehemu ya mwongozo mpya unaoungwa mkono na jeshi kwa nchi, sisi aliutaka uchaguzi wa urais na wabunge, jopo kutathmini katiba na kamati ya mashauriano kitaifa. Alisema mwongozo ulikubaliwa na makundi kadhaa ya kisiasa. 

Pia aliwasihi watu wa Misri kuepukana na ghasia. Jeshi lilimpa Bwana Morsi saa 48 kutatua matatizo ya kisiasa au kuwepo hatari ya jeshi kuingilia kati. Viongozi wa jeshi walisema wataweka “mwongozo” kama tofauti kati ya serikali ya ki-islam na wapinzani wake hawatamaliza matatizo yao ifikapo jumatano mchana ya tarehe tatu mwezi wa saba mwaka 2013. Tarehe hiyo ya mwisho ilipita muda wake bila ya hatua zozote kuonekana. 

Bwana Morsi hakika alikataa wito wa kujiuzulu na aliapa kuendelea kubaki madarakani hata kama itamsababishia kifo chake. Pia alilalamika jeshi kutoa kitisho chake cha kuingilia kati katika matatizo ya kisiasa. 

Baruti zilipaa angani kwenye umati wa watu wanaocheza na kupeperusha bendera katika uwanja wa tahriri Square mjini cairo, kiini cha ghasia za mwaka 2011 ambazo zilimuondoa Rais wa muda mrefu nchini Misri, Hosni Mubarak.

Katika wiki ilizopita maandamano yenye ghasia kati ya wafuasi na wapinzani wa bwana Morsi yameuwa takribani watu 40. Jeshi la Misri limetangaza kuchukua madaraka ya nchi hiyo huku likitangaza kuwa si mapinduzi lakini Mohamed Morsi si rais tena wa Misri. Tayari Saudia Arabia imetuma salamu za pongezi kwa mkuu wa jeshi la nchi hiyo kwa kluchukua madaraka.

Hali ya rais Morsi ilikuwa ngumu pale wananchi wake walipoamua kuingia mitaani kumpinga siku chche zilizopita kwa maandamano baada ya kujitwalia madaraka mengi kiutawala kama mtangulizi wake.(Chanzo: BBC)

Tuesday, July 2, 2013

Rais Obama awasili, aisifu Tanzania



Dar es Salaam. Rais Barack wa Marekani, Obama ametaja vipaumbele vinne vya Marekani kwa Tanzania, ambavyo vinajumuisha miradi mbalimbali ya umeme, miundombinu ya barabara, maji na programu za vijana kwa lengo la kuongeza ajira.
Kiongozi huyo aliwasili Dar es Salaam jana mchana ikiwa ni nchi ya mwisho katika ziara yake barani Afrika ikitanguliwa na Senegal na Afrika Kusini.
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais Jakaya Kikwete Ikulu, Rais Obama alisema aliainisha mambo hayo wakati alipozungumza na mwenyeji wake huyo.
Alisema katika mazungumzo hayo, waligusia mradi wa mkubwa wa umeme uitwao Power Afrika wenye lengo la kuongeza kiwango cha umeme kinachozalishwa nchini na barani Afrika ili kupata umeme nafuu na wa uhakika utakaochagiza kuongeza uzalishaji na kukuza ajira.
Nchi nyingine za Afrika ambazo zitanufaika na mpango huo ni Kenya, Ghana, Liberia, Nigeria na Ethiopia.
Rais Obama alisema pia wamezungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo, ukuzaji wa demokrasia na utawala bora. Alimzungumzia pia mchezaji nyota wa mpira wa kikapu wa Tanzania, Hashimu Thabeet anayecheza katika Ligi Kuu ya Marekani (NBA), akiwa na timu ya Oklahoma Thunder ya Marekani, akisema hawakuzungumzia suala lake na kuahidi kufanya hivyo siku nyingine.
Akijibu swali iwapo anaridhishwa na misaada ambayo nchi yake inatoa kwa Tanzania, Rais Obama alisema anafarijika kwa matunda yanayopatikana katika mapambano dhidi ya malaria, barabara mpya zinazojengwa na katika maeneo mbalimbali ya nchi.
“Hatutoi dawa, bali tunajenga miundombinu ya afya, hatutoi chakula, bali kuwezesha nchi kujitosheleza kwa chakula pia tunasisitiza kubadilishwa kwa sheria mbalimbali ili kutoa fursa kwa sekta binafsi kuleta mitaji yao kwa wingi zaidi, lakini jambo la muhimu ni kuijenga Afrika,” alisema.
Kuhusu sekta ya utalii, Rais Obama alisema watatangaza vivutio vya Tanzania, lakini kwa kuwa ameambiwa ujangili ni tatizo, Serikali yake itaisaidia Tanzania kukabiliana na changamoto hiyo.
“Tutatangaza utalii, nimeelezwa ujangili ni tatizo hivyo Marekani itasaidia kupambana na changamoto hiyo na tutaongeza fedha kuhakikisha hali hiyo inatokomea,” alisema.
Akichangia hoja ya misaada ya Marekani, Rais Kikwete alisema Mradi wa Maendeleo ya Changamoto za Milenia (MCC), umekuwa msaada mkubwa kwa Tanzania.
Alisema kupitia MCC, Tanzania imepata msaada wa kujengewa barabara katika maeneo ya vijijini na yale yanayozalisha chakula kwa wingi.(MWANANCHI)

Monday, July 1, 2013

OBAMA KUTUA LEO TANZANIA-ATAINGIA SAA NANE MCHANA

Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Dar es Salaam. Yametimia! Baada ya siku kadhaa za kusubiri kwa hamu, vitabu vya historia ya Tanzania vinaongezewa kumbukumbu wakati Rais wa Marekani, Barack Obama atakapowasili nchini leo mchana kwa ziara ya siku mbili. Ndege ya Air Force One itakayombeba  Obama na msafara wake itakanyaga ardhi ya Tanzania saa 8.40 mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako atapokelewa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete.
 Obama ambaye anafuatana na mkewe Michelle na binti zake, Malia na Sasha, anatua Tanzania ikiwa ni sehemu yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Anawasili Tanzania akitokea Afrika Kusini ambako alikwenda Ijumaa baada ya ziara yake ya Senegal.
Historia imetimia
Imepita miaka 50, tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alipotembelea Marekani, Julai 13, 1963 na kukutana rais wa nchi hiyo wakati huo, John F Kennedy na ziara hiyo inaaminika kuanzisha urafiki wa viongozi hao ambao umedumu hadi sasa. 
Ujio wa Rais Obama una maana na faida kubwa kwa Tanzania katika maeneo ukiangalia kihistoria, kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi pia.
Ziara ya  Obama ni heshima kubwa kwa Tanzania na itaingia katika vitabu vya kihistoria kwani ana rekodi ya kuwa mtu mweusi wa kwanza kuchaguliwa kuongoza taifa la Marekani. Kuchaguliwa kwake (Obama), ambaye baba yake mzazi alikuwa na asili ya Kenya kuliashiria nuru mpya kwa siasa za Marekani kwani watu weusi wa taifa hilo kwa miaka mingi walikuwa wakipigania haki za kufaidika na fursa za kiuchumi na kisiasa katika taifa la Marekani.
Tanzania, kwa miaka mingi ilikuwa inaunga mkono harakati za watu weusi na ndiyo maana iliikuwa karibu na viongozi wa harakati za kupigania haki za watu weusi.
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa karibu na Martin Luther King na mkewe Correta , ambao waliongoza harakati za mtu mweusi kujikomboa.Pia, viongozi wengine wa harakati hizo za mtu mweusi kutambuliwa kule Marekani, Jesse Jackson, Andrew Young na Malcolm X waliitembelea Tanzania mara nyingi.    Obama alipochaguliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2008 alifurahiwa na wapenda amani kote duniani na hasa Waafrika kwani walimhesabu kuwa ni sehemu yao.
Kuja kwake leo ni heshima kubwa kwani Tanzania inakuwa nchi ya nne  Afrika kutembelewa na Obama baada ya Ghana mwaka 2009 na ziara yake ya hivi karibuni ya nchi za Senegal na Afrika Kusini.
Ukizingatia kuwa  Obama  ana miaka mitatu na nusu kabla ya kumaliza kipindi chake cha pili cha uongozi wake huenda ziara hii ndiyo ikawa ya mwisho kwake barani Afrika akiwa na wadhifa wa rais.