Wednesday, July 10, 2013

BANTEKE AOMBA KUONDOKA ASTON VILLA.



Mchezaji wa klabu ya Aston Villa Christian Banteke amewasilisha ombi la kuondoka katika klabu yake na kuachia Chelsea na Aston Villa kuwania kumsajili kwa kitita cha Pauni Milioni 30.

Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka nchini Ubelgiji mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Aston Villa msimu uliopita akitokea klabu ya Genk ya Ubelgiji kwa kitita cha Pauni Milioni 7.

Benteke amekuwa akidaiwa kujiunga na klabu ya Arsenal, Chelsea na Tottenham Hotsupurs vilabu ambavyo vinatarajiwa kuendeleza mazungumzo na mchezaji huyo.

Uongozi wa Aston Villa unasema kuwa Banteke atasalia kuwa mchezaji wao ikiwa hatasajiliwa hivi karibuni kwa sababu alikuwa amesaini mkataba wa miaka mitatu na timu yake.

Kocha wa Villa Paul Lambert amesema kuwa ameshangazwa na kuhuzunishwa mno na Banteke kuhusu uamuzi wake kwa kile alichokisema mchezaji huyo hakuelewa kuwa mkufunzi huyo alikuwa anaijenga timu hiyo.

Katika hatua nyingine, mawakala wa mchezaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez anasema kuwa mchezaji huyo bado ana nia ya kuichezea klabu ya matufa bingwa barani Ulaya.

Klabu ya Liverpool imekataa Pauni Milioni 30 kutoka kwa klabu ya Arsenal ambayo imeonekana kutofutihwa na msimu wake nchini Uingereza.

Suarez alijiunga na Liverpool mwaka 2011 kwa kitita cha Puani Milioni 22 nukta 7 na ameichezea klabu hiyo mechi 96 na kuifungia mabao 51.

No comments:

Post a Comment