Thursday, July 11, 2013

SHIRIKISHO LA SOKA LAVIFUNGIA VILABU VILIVYOFUNGANA 79-0.

Shirikisho la soka nchini Nigeria limevifungia vilabu vinne baada ya kuandikisha matokeo ya kushangaza katika michuano ya kupanda daraja.

Vilabu hivyo ni pamoja na Plateau United Feeders FC, Akurba FC, Police FC na Bubayuaro FC.
 
Plateua United Feeders iliichabanga Akurba FC mabao 79 kwa 0 huku Police Machine FC ikaikagaraza Bubayaro FC mabao 67 kwa 0.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi katika chama cha soka nchini humo NFF Muke Umeh,amesema kuwa matokeo hayakubaliki kamwe na lazima uchunguzi ufanyike ili kubaini vipi mabao hayo yalifungwa.
 
Plateau United na Police Machine FC walicheza mchuano huo wakiwa na alama sawa na mshindi alihitajika kupata mabao mengi li kujihakikishia kusonga mbele ili kupanda daraja na kucheza ligi ya Kitaifa.
 
Plateua United Feeders walipata mabao 72 katika kipindi cha pili cha mchuano wao huku, huku Police wakiandikisha mabao 61 katika kipindi cha kwanza cha mchuano wao.
 
Uongozi wa soka nchini Nigeria unasema kuwa hauwezi kueleza kilichitokea na wale wote watakaobainika kusababsiha matokeo hayo watachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za soka nchini humo.

No comments:

Post a Comment