Sunday, July 29, 2012

MAJESHI YA SYRIA YAWASHAMBULIA WAASI KWA NDEGE.

http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120729&t=2&i=635702901&w=&fh=&fw=&ll=700&pl=300&r=CBRE86R0GDQ00
Mtoto akiangalia nyumba iliyobomolewa kwa mashambulizi.

http://s1.reutersmedia.net/resources/r/?m=02&d=20120729&t=2&i=635702669&w=&fh=&fw=&ll=460&pl=300&r=CBRE86R1M9B00
Askari wa waasi akipita karibu na jengo lililobomolewa na ndege za jeshi la serikali.
SYRIA,
Vikosi vya serikali vimeripotiwa kuwashambulia waasi kwa helikopta za kijeshi na makombora asubuhi ya jumapili ya leo katika mapigano makali ya kugombea udhibiti wa mji wa pili wa Aleppo.Wanaharakati wameripoti mapigano katika baadhi ya Wilaya na vitongoji katika jiji hilo la kibiashara.

Msuluhishi wa mgogoro huo Bw.Koffi Annan na viongozi wengine wamesema hali katika mji wa Aleppo
 inaonesha umuhimu wa kumaliza mgogoro wa Syria.Kiongozi wa Baraza la kitaifa la Syria ambalo ni muunganiko wa vikundi vya upinzani dhidi ya serikali ya Syria Bw.Abdelbasset Sida amezitaka nchi marafiki na washirika wa Syria kuachana na baraza la Ulinzi la Umoja wa mataifa na badala yake waingie wenyewe Syria kuung'oa utawala wa rais Bashar al-Assad.
   
Mapigano nchini Syria yamedumu kwa takribani miezi 16 na kuua maelfu ya watu na hali hivi sasa ni ya vita nchini humo ambapo vikosi vya waasi vinapigana na majeshi ya serikali kuung'oa utawala wa rais  al-Assad.

No comments:

Post a Comment