Sunday, July 22, 2012

MAREKANI KUZIPATIA KENYA ,BURUNDI, UGANDA NA DJIBOUT SILAHA DHIDI YA ALSHABAB

Washington D.C -Marekani,

Marekani itaipatia Kenya, Uganda na Djibout vifaa vya kijeshi vya kisasa ili kuwasaidia kupambana na wanamgambo wa Al-shabab imearifiwa.

Kwa mujibu wa gazeti la Wall Street la Marekani katika habari yake hapo juzi tarehe 20,Kenya watapatiwa ndege zinazoruka bila rubani zipatazo nane na vifaa vingine vya kijeshi ikiwemo magari yenye silaha.

Nchi nyingine zilizobaki ambazo ni Uganda,Burundi na Djibout zitapatiwa vifaa vya kijeshi pia kuzisaidia kukabiliana na waasi hao.

No comments:

Post a Comment