Wednesday, July 18, 2012

MELI NYINGINE YAZAMA TANZANIA

Meli ya SKAGIT iliyokuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar ikiwa  imewabeba watu wapatao miambili imearifiwa kuzama katika bahari ya hindi eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar.

kwa mujibu wa taarifa za vikosi vya wanamaji , meli hilyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.Jeshi hilo la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu hao.
 
Polisi nchini Tanzania wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo,ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo.

No comments:

Post a Comment