Sunday, February 5, 2012

MANCHESTER YAIBANA CHELSEA NYUMBANI.

Javier Hernandez wa Manchester United Akifunga Goli la tatu Dhidi Ya Chelsea.

STAMFORD BRIDGE,

Manchester United leo wamejitutumua na kutoka nyuma ya magoli 3 hadi droo ya magoli 3-3 dhidi ya mahasimu wao wakubwa Chelsea waliokuwa Uwanja wao wa nyumbani.

Chelsea walijikuta wakiongoza katika dak. 36 baada ya goli la kujifunga la Jonny Evans wa Manchester na baadae kufuatiwa na Magoli ya ya juan mata dak. 46 na David luiz dak. 51 na hivyo kuwa mbele kwa magoli 3-0.
hata hivyo wayne rooney alikuja kuvuruga furaha ya Chelsea baada ya kufunga penati zake mbili walizopata dakika ya 58 baada ya Sturidge kumchezea rafu Evra na dak. 69 baada ya Wellbeck kuguswa kidogo na Ivanovich na manmo dak. ya 84 javier harnandez aliifungia manchester United bao lake la tatu baada ya kupiga kichwa kilichomshinda Kipa Peter cech wa chelsea.

kwa matokeo hayo manchester City imeendelea kuwa kileleni mwa ligi hiyo kwa kuwa na pointi 57 ikifuatiwa na manchester united yenye point 55 na Totenham 49 huku chelsea Ikishika Nafasi ya Nne kwa kuwa na point 43.

No comments:

Post a Comment