Sunday, February 9, 2014

Serena akacha Indian Wells

 
HESABU za waaandaaji wa michuano ya tenisi ya Indian Wells BNP Paribas Open kuona nyota namba moja kwa wanawake, Serena Williams, anashiriki kipute cha mwaka huu zimeyeyuka.
Serena ambaye mara ya mwisho kushiriki michuano hiyo ni miaka 13 iliyopita, alisema juzi kuwa hatashiriki baada ya kutafakari kwa kina ushiriki wake.
“Baada ya kutafakari kwa kina, sitaweza kushiriki michuano ya Indian Wells BNP Paribas Open kwa mwaka huu,” alisema nyota huyo huku akiwatakia kila la heri washiriki katika michuano hiyo inayotarajiwa kuwaleta pamoja nyota mahiri wake kwa waume.
Akizungumzia uamuzi wa Serena, Mkurugenzi wa michuano hiyo, Steve Simon, alisema wanamkaribisha katika michuano ya mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment