Friday, September 14, 2012

MAANDAMANO YA WAISLAMU KUPINGA FILAMU YA KIMAREKANI YAZIDI KUPANUKA




 
Sudan,Yemen na Tunisia,
Waandamanaji wa kiislamu wenye itikadi kali na waliochukizwa na filamu yenye kudhihaki dini ya kiislamu wamezingira na kushambulia balozi za Ujerumani,na Marekani mjini Khatoum nchini Sudan leo.

Waandamanaji hao wamevavamia Balozi za Ujerumani nchini humo na kuwasha moto pamoja na kuchana bendera ya Ujerumani kisha kupandisha bendera yenye nembo ya Kiislamu.Waandamanaji wengine wamekusanyika katika ubalozi wa Marekani baada ya swala ya Ijumaa ya leo ingawa vurugu hazijaripotiwa katika balozi hiyo.

Huko Yemen yametokea mapambano makali kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga filamu hiyo ambapo mtu mmoja ameripotiwa kufariki na wengine 15 kujeruhiwa.

Tunisia, katika mji mkuu wa Tunis waandamanaji wameupiga mawe ubalozi wa Marekani na kuwalazimu askari wa kutuliza ghasia nchini humo kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya.


Filamu hiyo iliyotengenezwa nchini Marekani na kusambazwa katika mtandao imeamsha hasira na chuki za ulimwengu wa kiislamu dhidi ya Marekani huku serikali ya Marekani kupitia kwa waziri wake wa mambo ya nje Bi.Hilary Clinton ikikanusha kuhusika na filamu hiyo na kuilaani vikali kuwa ni yenye kuchukiza na kufedhehesha.

No comments:

Post a Comment