Friday, September 7, 2012

OBAMA AOMBA MUDA ZAIDI KWA WAMAREKANI-Ambeza Romney.


CHARLOTE,NORTH CAROLINA-MAREKANI ,
Hatimaye mgombea wa kiti cha urais nchini Marekani kupitia chama cha Democrats Rais Barack Obama amekubali uteuzi wake na kuwataka wamerakani kumpa muda zaidi wa kuboresha uchumi na maisha ya Wamarekani.
Akiongea katika mkutano mkuu wa chama cha Democrats Obama amesema amefanya mengi katika kipindi chake cha uongozi na Wamarekani wanatakiwa kuchagua kati ya nchi pamoja na uchumi au tuhuma kutoka kwa wapinzani wake.

Uchumi na Ajira:
Akiongelea uchumi rais huyo amesema siyo rais kumaliza matatizo ya uchumi yaliyoanza kwa miongo kadhaa kwa kipindi cha miaka michache,
"Siwezi kujifanya njia ninayoitoa ni ya haraka au rahisi"alisema Obama na kuongeza"Itachukua zaidi ya miaka michache kumaliza changamoto ambazo zimejengwa kwa miongo kadhaa"

 Rais huyo ameongelea umuhimu wa mpango wake wa kuitegemeza nchi katika nishati ya mafuta ili kufikia mwaka 2020 Marekani iweze kupunguza kiwango cha mafuta inayoyaingiza kutoka nje  kwa zaidi ya nusu,mpango ambao umepangwa kutengeneza ajira laki sita  katika viwanda vya gesi asilia akisema kuwa mpango huo utaongeza ajira.

Pia rais huyo ameongelea mpango wake wa kuongeza ajira katika viwanda vya uzalishaji zipatazo milioni 1, pamoja na ajira 100,000 za walimu wa hesabu na sayansi katika sekta ya Elimu.

Sera za kigeni:
Akiongelea sera za kigeni rais huyo amemshambulia mpinzani wake Romney kwa kupinga sera zake akisema yeye si mzoefu katika sera hizo na yeye(Obama) ameonesha uimara katika sera hizo akigusia pia kauli ya Romney kuwa Urusi ni adui namba moja wa Marekani, ambapo amesema huwezi kuwaita Urusi ni maadui namba moja wa Marekani badala ya Al Qaida isipokuwa ukiwa na mawazo mgando ya vita baridi, Pia rais huyo amehofia ukweli wa Romney kuboresha uhusiano na China ilhali kauli zake zimemwingiza katika mvutano na marafiki wao wakubwa Uingereza akirejea kauli za Romney wakati wa ufunguzi wa Olimpiki.

 Usalama wa nchi:
Obama alisema ametimiza sehemu kubwa ya ahadi zake za mwaka 2008 katika usalama wa nchi ambapo aliahidi kumaliza vita nchini Iraq na amefanya hivyo, pia kuongeza mapambano na kuidhohofisha Taleban huko Afghanistan,Pia amesema Alqaida imedhoofishwa na inaendelea kudhoofishwa na kiongozi wake Osama ameuawa.

 Obama amesema hatotumia fedha za nchi hiyo kununua na kutengeneza silaha bali kuboresha maisha ya Wamarekani kwa kujenga shule zaidi na kutoa huduma nyingine za kijamii.

Pia rais huyo amesema alitoa ahadi ya kuendelea kuwathamini zaidi askari wastaafu walioitumikia Marekani kwa vipindi mbalimbali.

Mazingira:
Rais Obama pia ameongelea suala la utunzaji wa Mazingira akisema mpango wake wa gesi asilia utasaidia kulinda mazingira na kuiepusha Marekani na majanga ya kimazingira.

Mgombea huyo alikuwa akifunga mkutano wa Chama cha Democrats kuelekea uchaguzi mkuu wa Marekani ambapo atapambana na Mitty Romney wa Chama cha Republican hapo Novemba 6 mwaka huu.
Mkutano huo umeelezewa na wengi kumpa nguvu mpya mgombea huyo ingawa bado ushindani ni mkubwa kuelekea uchaguzi huo kwa huku changamoto ya ukuaji wa ajira ambazo zinapanda na kushuka bado ni kikwazo na haijatoa mwelekeo kamili juu ya imani ya wapiga kura kwa rais huyo.

No comments:

Post a Comment