Saturday, September 8, 2012

USAFIRI WA RELI DAR KUANZA OKTOBA .

 
DAR ES SALAAM-TANZANIA,
Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) imesema usafiri wa reli yenye urefu wa kilomita 197 jijini l Dar es Salaam utazinduliwa rasmi mwaka huu mwezi Oktoba hata kama baadhi ya miundo mbinu ya reli hizo haitakamilika.Kwa mujibu wa mkurugenzi wa ufundi wa kampuni ya reli Tanzania Bw.Mohamed Mohamed amesema sehemu kubwa ya ujenzi huo imekamilika ingawa bado kuna changamoto nyingi.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kandarasi za ujenzi wa miundo mbinu hiyo ikiwemo sehemu za kukatisha tiketi, vuwekaji wa kokoto katika reli , vyoo na alama za tahadhari zimeshatolewa kwa makampuni mbalimbali.

 Mkurugenzi huyo alisema moja ya changamoto ni namna ya kuwaamisha watu waliopo ndani ya eneo linapotakiwa kupita mradi huo ambapo aliwataka watu wote waliopo ndani ya kilometa 15 kutoka eneo la Reli kuondoka.

Mradi huo wa relikwa sasa tayari  umeshaanza na ukarabati wa njia ya reli ya Stesheni ya Dar es Salaam hadi Ubungo Maziwa unaendenlea, njia ambayo treni itatumia takriban dakika 35 kutoka mwanzo hadi mwisho wa kituo hukuikisafirisha abiria 16,000 kwa siku.

Kwa reli ya Tazara  safari hiyo inatarajia kuhudumia abiria 20,000  kwa siku na kufanya jumla ya abiria kuwa 36,000.na hivyo kuwa msaada kwa Jiji hilo lenye wakazi zaidi ya milioni 4.

No comments:

Post a Comment