Monday, September 24, 2012

KOREA KASKAZINI KUFANYA MAPINDUZI KATIKA KILIMO

http://www.csmonitor.com/var/ezflow_site/storage/images/media/content/2012/0725-north-korea-kim-jong-un/13252612-1-eng-US/0725-north-korea-kim-jong-un_full_600.jpg
Pyongyang-Korea Kaskazini,
Habari kutoka Korea kaskazini zinasema kuwa mageuzi ya kiuchumi yatakayoruhusu wakulima kuweka mazao yao na kushinikiza masoko huru, yanaidhinishwa .

lengo la hatua hiyo linaonekana kulenga kuongeza mazao katika nchi hiyo iliyo na uchumi unaoendeshwa na serikali na unaokumbwa na ukosefu mkubwa wa chakula.

Hakuna tangazo rasmi lililotolewa na wizara ya kilimo nchini humo lakini wachambuzi wanaiona kuwa ishara ya uwezekano wa mabadiliko ya mwelekeo chini ya kiongozi mkuu mpya Kim Jong-un ambaye tangu amerithi uongozi kutoka kwa baba yake amefanya baadhi ya mabadiliko ikiwemo kuwa na hotuba katika vyombo vya habari mara kwa mara na badiliko alilolifanya la kumbadilisha mkuu wa jeshi wa nchi hiyo aliyekuwa mzee na kumteua mkuu mpya ambaye n kijana.

Masoko huru yamekuweko kwa miaka kadhaa Korea kaskazini tangu kiongozi mwazilishi wa Korea kaskazini Bw.Kim Il Sung kuanzisha mfumo wa mashamba ya ushirika ambayo yaliwataka wakulima kutunza hifadhi ya chakula kinachobaki badala ya kukiuza.

No comments:

Post a Comment