Saturday, October 13, 2012

UMOJA WA KIMATAIFA WAANDAA MPANGO WA KUISHAMBULIA MALI KIJESHI



BAMAKO-MALI,
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limethibitisha mpango wa kushambulia waasi walioivamia sehemu ya nchi ya Mali huku likitoa siku 45 kwa nchi za Afrika magharibi kutoa taarifa kuhusu mpango wa makubaliano uliopo.

 Ujumbe huo uliothibitishwa na baraza hilo Ijumaa ya jana umeutaka utawala wa Bamako na wawakilishi wa waasi wa Tuareg pamoja na waoiganaji wa kiislamu wanaotawala kaskazini kujihusishakatika mapatano.
Wanachama hao wameonya kuwa mpango huo uzingatie mtazamo wa kuleta umoja,uimara na uhuru wa kisiasa nchini Mali.

Mali imegawanyika tangu mwezi machi mwaka huu baada ya rais wa nchi hiyo kupinduliwa hali iliyowafanya waasi wa Tuareg kuteka sehemu kubwa ya nchi hiyo wakishirikiana na waasi wa kiislamu wenye uhusiano na Al-Qaeda.

No comments:

Post a Comment