Friday, October 26, 2012

OBAMA APIGA KURA ZA AWALI-AVUNJA REKODI.


CHICAGO-MAREKANI, Rais Barack Obama wa Marekani amepiga kura ya awali hapo jana na kuwa rais wa kwanza kupiga kura ya awali. Obama amepiga kura hiyo katika mji wa Chicago ambako ndiyo nyumbani kwao. Obama yupo katika kampeni ya siku mbili katika majimbo nane yanayotegemewa kutoa mshindi wa Urais kutokana na kutokuwa na ushabiki wa Chama likiwepo jimbo kubwa la Ohio.
Upigaji kura huo wa rais Obama umekuwa sehemu ya kampeni za Rais huyo ambaye amewahamasisha watu kupiga kura mapema, ambapo mpaka sasa inakasdiriwa watu zaidi ya milioni 7 wameshaoiga kura zao na hivyo kufanya vituo zaidi ya asilimia 35% kuwa tayari vimepigiwa kura siku ya uchaguzi.
Mfumo huo wa kupiga kura mapema ni muhimu kwa watu ambao huwa na udhuru au kuhofia kutokuwepo siku ya kupiga kura.
Wakati huo huo wanakampeni wa Rais Obama wameunga mkono ndoa za Kishoga katika majombo matatu ya Washington,Maryland na Maine ambako kura za maoni zinapigwa kuhusu kurudisha au kuondoa ndoa hizo.
Mpinzani wake Mitty Romney alikuwa Ohio hapo jana katika kampeni huku kura za maoni zikionesha Mitty Romney akiongoza kwa asilimia kadhaa zikiwemo asili mia 54 kwa 49 kwa 47 katika kituo cha habari cha BBC ya Uingereza na asilimia 52 ya watu wakipiga kura za umwamini Mitty Romney katika uchumi dhidi ya asilimia 47 wanaomwamini Obama katika katika kituo cha habari cha ABC.



No comments:

Post a Comment