Monday, October 22, 2012

Wapiganaji wa kigeni waingia Mali Kaskazini

Mamia ya wanajihadi kutoka nje ya nchi ya Mali wameripotiwa kuwasili kaskazini mwa nchi hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita kupigana na wanamgambo wa kiislamu wanaomiliki eneo la kaskazini mwa Mali wakati vikosi vya kimataifa vikitarajiwa kuingilia kati mzozo wa Mali. Wakazi wa Mji wa Timbuktu, Gao na Maafisa usalama wa nchini Mali na Makamanda wa makundi ya kiislam wamethibitisha kuwa kumekuwa na wimbi la wapiganaji wa kigeni wanaoingia kaskazini mwa Mali kwa zaidi ya siku mbili zilizopita. Kuwasili kwa wanajihadi hao kutoka Sudan na Sahara Magharibi, kunatokea siku mbili tu baada ya mkutano wa kimataifa wa nchi washirika wa Mali ambao umedhamiria kuongeza mshikamano na serikali ya Mali kurudisha eneo hilo. Wakati huohuo,Serikali ya Ufaransa inatangaza kurejelea ushirikiano wake wa kijeshi na nchi ya Mali, Ushirikiano ambao ulisimamishwa tangu jaribio la mapinduzi ya tarehe 22 ya mwezi Machi 22 mwaka Wimbi hilo la wapiganaji limeingia wakati huu ambapo jumuia ya kiuchumi ya nchi za magharibi mwa Afrika,ECOWAS ikiendelea na harakati za kuvamia kaskazini mwa nchi hiyo na kusambaratisha Makundi ya kiislamu katika eneo hilo.(Chanzo RFI)

No comments:

Post a Comment