Wednesday, October 31, 2012

CHELSEA YAMTUHUMU MWAMUZI DHIDI YA MATAMSHI YA KIBAGUZI KWA MIKEL OBBI




LONDON-UINGEREZA,
Klabu ya Chelsea ya nchini Uingereza imemtuhumu mwamuzi aliyechezesha wa mchezo wao na Manchester United Mark Clattenburg kumtolea maneno ya kibaguzi kuungo wake raia wa Nigeria John Mikel Obi. Msemaji wa Chelsea ameweka bayana wameshawasilisha malalamiko yao ili hatua zichukuliwe dhidi ya Clattenburg ambaye amekumbana na ukosoaji mkubwa kwa kile kinachoelezwa ni kushindwa kuumudu mchezo huo. Chama cha Waamuzi wa Kulipwa PGMO kimekiri kupokea malalamiko hayo na kusema watayafanyia kazi kwa kadri ambavyo itaonekana na uchunguzi utafanyika ili kubaini iwapo Clatternburg alitoa maneno ya kibaguzi kwa Mikel Obi. Katika mchezo huo Manchester United ilivunja mwiko wa kushindwa kupata ushindi kwenye michezo ya Ligi Kuu katika uwanja wa Stamford Bridge kwa kipindi cha miaka kumi baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-2. Chelsea ililazimika kumaliza ikiwa na wachezaji tisa baada ya kushuhudia Branislav Ivanovic na Fernando Torres wakilimwa kadi nyekundu kitu ambacho kilizusha lawama za kila mara kwa mwamuzi Clattenburg. Manchester United ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata goli kupitia kwa David Luiz ambaye wakati anaokoa akaukwamisha mpira wavuni kabla ya Robin Van Persie kufunga goli la pili na kushuhudia Juan Mata akifunga goli la Chelsea kabla ya mapumziko. Kipindi cha pili Chelsea waliongeza kasi na kufanikiwa kupata goli la kusawazisha kupitia Ramires kabla ya Javier Hernandez hajafunga goli la tatu na la ushindi dakika kumi na tano kabla ya mchezo kumalizika na kuiba ushindi Manchester. Goli la Hernandez lilizidisha hasira kwa wachezaji wa Chelsea na hata mashambiki wake kutokana na kudai mfungaji alikuwa kwenye eneo la kuotea na halikustahili kuwa goli na kushuhudia Mikel Obi akilimwa kadi ya njano kwenye malumbano hayo. Kwa matokeo hayo sasa Chelsea inaendelea kuongoza kwa tofauti ya pointi moja baina yake na Manchester United ambayo imepiteza michezo mieili tangu kuanza kwa Ligi msimu huu na huu ukiwa mchezo wa kwanza kwa The Blues kufungwa.(Chanzo RFI)

No comments:

Post a Comment