Monday, October 15, 2012

MKUTANO WA FRANCOPHONE WAFUNGWA.

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/4f48dfca7accc969fc3ad0912c4afc14_L.jpgMkutano wa wakuu wa umoja wa nchi zinazotumia lugha ya kifaransa Francophone ulifungwa jana huko Kinshasa, baada ya kupitisha maazimio kuhusu Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na Mali.
 Katika mkutano huo viongozi hao wwamekubaliana kuheshimu umoja na ukamilifu wa ardhi wa Mali na kutaka kuimarisha mchakato wa mazungumzo kati ya pande zote nchini Mali, ili kuleta utulivu wa hali ya kisiasa nchini humo.

Kuhusu mgogoro wa Demokrasia na Rwanda viongozi hao wamezitaka nchi hizo ziendelee na mazungumzo ya kuimarisha uaminifu baina yao ili kuondoa mgogoro unaozikabili kuhusu mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Viongozi hao pia waliitaka jumuiya ya kimataifa kuwa na mkutano wa kujadili kuimarisha mapambano dhidi ya uharamia katika Ghuba ya Guinea.

Mkutano huo uliwakutanisha wakuu 15 wa serikali za nchi zinazozungumza kifaransa, mkutano ujao umepangwa kufanyika Senegal mwaka kesho

No comments:

Post a Comment