Thursday, October 25, 2012

ISRAEL NA PALESTINA WASHAMBULIANA KIJESHI



ISRAEL/PALESTINA,  Majeshi ya Palestina yamerusha maroketi zaidi ya 40 kuelekea Israel hapo jana huku isarel na wenyewe wakifanya mashambulizi ya anga kuelekea Ukanda wa Gaza.



Kwa mujibu wa hospitali huko Gaza  zimesema kuwa Wanajeshi watatu waliokuwa wakijiandaa kufanya Shambulio la Roketi waliuawa  Wna wenginei wengine wanane kujeruhiwa, huku shambulio kuelekea Israel likijeruhi watu kadhaa.

Mashambulio hayo yamefuatia  mwanajeshi mmoja wa Israeli kujeruhiwa vibaya katika Shambulio la Bomu alipokuwa akifanya Doria mpakani  Kissufin eneo la Gaza hapo juzi.

Chama cha Hamas kimethibitishwa waliouawa kuwa wanajeshi wake huku waziri Mkuu wa Israeli Benjamini Netanyahu akiahidi kulipa kisasi kwa Gaza amabao amewatuhumu kuungwa mkono na Tehran.

No comments:

Post a Comment