Monday, October 22, 2012

FIDEL CASTRO AONEKANA TENA



HAVANNA-CUBA,
Kiongozi mwanamapinduzi wa Bw. Fidel Castro(86) ameonekana kuwa katika hali nzuri tofauti na uvumi baada ya kukutana na aliyewahi kuwa makamu wa rais wa Venezuela Bw. Elias Jaua hapo jumamosi iliyopita.Jaua ambaye ameonesha picha za kiongozi huyo na kuwaambia waandishi wa habari kuwa kiongozi huyo yupo katika hali nzuri.

Fidel Castro hajaonekana hadharani tangu mwezi Machi mwaka huu alipokutana na kiongozi wa kanisa Katoliki duniani papa Benedict XVI.Tangu wakati huo kiongozi huyo hajaonekana hadharani na kuzua utata juu ya afya yake huku wengi wakivumisha yupo mahututi na wengine wakidai amefariki.

Tangu kuonekana kwake mwezi Machi kiongozi huyo amekuwa akitoa hotuba zilizoandikwa kwenye vyombo vya habari bila ya yeye kutokea huku baadhi ya hotuba hizo kuonekana zina dosari kiasi na kuzua maswali kuhusu afya ya kiakili ya kiongozi huyo.

Bw.Jaua ambaye anagombea ugavana katika jimbo la Miranda huko venezuela amesema waliongea na Fidel Castro katika Hoteli ya Havana na waliongea kuhusu mambo mengi yakiwemo kilimo na siasa,"Ndiyo nimeonge na Fidel jana alikuwa vile vile kama yule Fidel wa zamani na mashavu yake ya pink," Martinez aliliambia shirika la Reuters.


No comments:

Post a Comment