Wednesday, October 31, 2012

KIMBUNGA CHA SANDY CHASABABISHA HASARA ZAIDI YA DOLA BILIONI ISHIRINI.




MAREKANI,
Rais wa Marekani Barack Obama atangaza majimbo ya kaskazini mashariki ya Marekani ya New York na New Jersy kuwa maeneo ya "maafa makubwa" baaada ya kimbunga kikubwa kilichopewa jina la Sandy.

Tangazo hilo limetolewa hapo jana siku ya jumanne na linaruhusu kutumika kwa fedha ya serikali katika maafa hayo.

Kimbunga Sandy kilifika nchi kavu siku ya Jumatatu jioni na kinaendelea kupunguka nguvu zake kinapita sehemu za kati na kaskazini ya marekani. Maafisa wanasema watu 16 walifariki katika katika maeneo ya mashariki ya Marekani kutokana na kimbunga hicho ambacho kilisababisha vifo vya watu 65 wiki iliyopita katika nchi za Caribbean.

Kwa siku ya pili mfululizo shughuli zote za serikali na biashara pamoja na shule katika miji mikubwa mashariki ya Marekani ziliendelea kufungwa siku ya Jumanne wakati mamilioni ya watu wakiwa hawana huduma ya umeme.

Takriban wasafiri elfu 10 walikwama katika miji hiyo ya mashariki ya nchi baada ya maelfu ya safari za ndege kuahirishwa kwa siku ya pili. Halikadhalika huduma za usafiri wa mijini iliendelea kufungwa na mjini New York kumekuwepo na mafuriko ya maji katika njia za reli za chini kwa chini.

Watalamu wa uchumi wanatabiri kwamba kimbunga Sandy huwenda kimesababisha hasara inayogharimu takriban dola bilioni 20.(VOA)

No comments:

Post a Comment