Thursday, March 8, 2012

KULIKONI YATAWALA AFYA YA LOWASSA!

DAR ES SALAAM, Kumekuwa na habari za utata kuhusu hali ya afya ya Waziri mkuu aliejiuzulu na mbunge wa Monduli Mh. Edward Lowassa, huku baadhi ya habari zikitaarifu kuwa mbunge huyo amelazwa katika hospitali huko ujerumani. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi hapo jana tarehe 7 Machi, limefanikiwa kuzungumza na Mbunge huyo ambaye alikiri kuwepo hospitalini ingawa alikataa kuelezea kwa undani kuhusu hali yake ya afya. Alipoulizwa kuhusu suala hilo katibu wa bunge Dk Thomas Kashillilah alisema ofisi yake haina taarifa juu ya suala hilo. Hali hiyo bado inazua maswali mengi lakini pengine tuendelee kuvuta subira juu ya taarifa rasmi ya kinachoendelea.

No comments:

Post a Comment