Wednesday, May 22, 2013

RIPOTI YA TUME YAPENDEKEZA KENYATTA NA RUTO KUSHITAKIWA

NAIROBI-KENYA,Viongozi wa ngazi za juu nchini Kenya, wakiwemo Rais Uhuru Kenyatta na Makamu wake William Ruto, ni miongoni mwa waliopendekezwa kushtakiwa katika ripoti ya kushtusha iliyotolewa na Tume ya TJRC. 


Tume ya maridhiano na haki ilikabidhiwa jukumu la kuchunguza visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyofanywa tangu mwaka 1963 nchi hiyo ilipojipatia uhuru wake.


Iliundwa baada ya ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/08 uliozua ghasia miaka mitano iliyopita kama njia ya kuleta maridhiano miongoni mwa wakenya.

Baada ya uchaguzi huo, watu 1,500 waliuawa na wengine zaidi ya 600,000 kulazimika kutoroka makwao.


Kenyatta na Ruto, waliokuwa mahasimu katika uchaguzi wa mwaka 2007, walishinda uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Machi baada ua kuungana chini ya muungano wa Jubilee.

Licha ya kuwa hakuna mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo dhidi ya Rais na naibu wake, inapendekeza uchunguzi zaidi dhidi ya maafisa wakuu waliotajwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007 na hata kufunguliwa mashtaka.(CHANZO:BBC&DW)

No comments:

Post a Comment