Tuesday, June 5, 2012

RAIS WA NIGERIA ATEMBELEA ENEO LA AJALI YA NDEGE.

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan

http://www.dw.de/image/0,,15996043_401,00.jpg

LAGOS, NIGERIA

©Jonathan Rebboah/Wostok Press/Maxppp France, Paris 25/11/2011 Le president du Nigeria Goodluck Jonathan arrive au palais de l Elysee The President of Nigeria Goodluck Jonathan at the Elysee PalaceRais wa Nigeria Goodluck Jonathan amehahidi kuwa serikali yake itaimarisha usafiri wa anga baada ya hapo jana watu  153 kufariki baada ya ndege ya shirika la Dana abiria kuanguka nchini humo.
Rais Jonathan ametoa ahadi hiyo  wakati alipolitembelea eneo la kitongoji cha mji wa Lagos, ambako ndege ya abiria ya shirika la Dana ilianguka jana na kuwaua abiria wote 153 waliokuwemo katika ndege hiyo.
"Tumekuwa tukijizatiti kuboresha sekta ya usafiri wa ndege hapa nchini. Ajali hii ni pigo kubwa kwetu na nitahakikisha ajali kama hii haitokei tena humu nchini,"alinukuliwa rais huyo baada ya kushuhudia ajali hiyo.


Uchunguzi wakwama;
Kwa mujibu wa taarifa ya mwandishi wa habari wa shirika la AFP, polisi walilazimika kutumia vitoa machozi wakati watu takriban 2,000 walipojaribu kuingia eneo lililofungwa na polisi wakitaka kushuhudia athari za ajali hiyo na hivyo kutatiza uchunguzi.
hadi leo  waokoaji wamefaulu kutoa maiti zisizopungua 62 kutoka kwa mabaki ya ndege hiyo. Kanisa, jengo la makazi ya watu la ghorofa mbili na duka la huduma za uchapishaji liliharibiwa vibaya katika eneo la ajali.  Moshi bado unafuka katika eneo la ajali na wafanyakazi wa zimamotowamekuwa wakiendelea na juhudi za kuuzima moto unaoendelea kuwaka kwenye mabaki ya ndege hiyo.
Solomon Omotayo ni miongoni mwa mashuhuda wa ajali hiyo ya  ndege  ikipoteza muelekeo muda mfupi kabla kuanguka katika kitongoji cha Iju jijini Lagos. "Tulipoiona, ilkuwa chini mno! Dakika kama mbili baadaye tukasikia mlio. Tuliufuata moshi hadi hapa. Maafisa waliondoa maiti lakini sijui ni ngapi. Ni hasara kubwa na maiti nyingi zingali zimefunikwa."alisema Solomon.

No comments:

Post a Comment