Wednesday, January 9, 2013

baadhi ya Wajumbe wa Umoja wa Mataifa waunga mkono kutumika kwa ndege za upelelelezi Congo.



Waasi wa M23 wanaohatarisha usalama wa Mashariki mwa Congo

DRC CONGO,
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa,UN wameunga mkono pendekezo la kuanza kutumika kwa Ndege maalum za upelelezi mashariki mwa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC ili kulinda usalama wa Raia.

 Mkuu wa Operesheni za Umoja wa Mataifa, Herve Ladsous amesema kuwa amewasilisha ombi maalumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha mpango wa kutumika kwa ndege maalumu zenye uwezo wa kuona hata wakati wa usiku kwenye maeneo ya Mashariki na Mpakani mwa DRC na Rwanda.
 
Pendekezo hilo limepingwa vikali na nchi ya Rwanda, huku baadhi ya Mataifa yakionesha wasiwasi wao iwapo ndege hizo zitaidhinishwa kutumika kuongezea nguvu vikosi vya MONUSCO katika kuimarisha usalama nchini humo.

Iwapo Baraza la Usalama litaidhinisha mpango huo itakuwa ni maraya kwanza kwa UN kupitisha mpango kama huo nchini DRC mpango utakaosaidia pia kukabiliana na Waasi.(CHANZO:RFI)

No comments:

Post a Comment