Friday, January 11, 2013

TANGA KUGAWANYWA NA KUWA MIKOA MIWILI.


 
TANGA-TANZANIA, Kamati ya ushauri mkoa wa Tanga RCC imepitisha pendekezo la kuugawa mkoa wa Tanga na kuwa mikoa miwili na kuiagiza sekretarieti ya mkoa kulifanyia kazi pendekekezo hilo.
Katika pendendekezo hilo lililotolewa na Afisa Mwandamizi wa serikali za mitaa Yohana Paul mkoa wa Tanga utabaki na wilaya za Tanga, Muheza, Mkinga na Pangani
Aidha mkoa mpya utakuwa na wilaya za Kilindi, Handeni, Lushoto na Korogwe.
Bwana Paul amebainisha kuwa lengo hasa la kuugawa mkoa huo ni kusogeza huduma karibu kwa wananchi kutokana jiografia ya mkoa wa Tanga ulivyo.
Ambapo baadhi ya wananchi wanaoishi mbali na makao makuu ya mijini na wilaya hawanufaiki na huduma za kijamii zinazotolewa na serikali.(CHANZO:FREE AFRICA)

No comments:

Post a Comment