Wednesday, January 2, 2013

HATIMAYE FAMILIA YA SAJUKI YARIDHIA MAREHEMU KUZIKWA DAR SIKU YA IJUMAA

Taarifa ambazo zimeridhiwa na maamuzi ya familia na ndugu wa karibu, zinasema marehemu Juma Kilowoko aka Sajuki atazikwa siku ya ijumaa katika makaburi ya Kisutu.

Taarifa ambazo pia zimetoka kwa msemaji wa Bongo Movie na wahusika wa maandalizi ya mazishi hayo, wanasema ndugu wa Sajuki wameridhia marehemu kuzikwa hapa na sio Songea kama wengine wanavyotangaza. Kuhusu kusogeza mpaka ijumaa, msemaji huyo akasema, ni kutokana na kusubiri ndugu wa marehemu wanaotoka sehemu mbali mbali kuja Dar kwa ajili ya mazishi hayo, wengi wakitokea Songea.

Sajuki ambae alifariki usiku wa kuamkia tarehe 2, atazikwa siku ya ijumaa ya tarehe 4 katika makaburi ya Kisutu, ambapo mazishi hayo yataanza muda wa saa 5 asubuhi.

Mungu ailaze roho ya marehemu Juma Kilowoko (Sajuki) mahala pema peponi, Amen

No comments:

Post a Comment